Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/02/11
“Je, unafikiri kwamba inawezekana kabisa kujua jinsi Mungu alivyo? [Acha mutu ajibu.] Nina wazo lenye kupendeza kuhusu ulizo hilo.” Soma na kuzungumzia habari iliyo chini ya ulizo la 2 kwenye ukurasa wa 16 na andiko moja kati ya maandiko yanayoonyeshwa. Umtolee gazeti na ufanye mpango wa kumrudilia ili kuzungumzia habari iliyo chini ya ulizo la 3.
Amkeni! Mwezi wa 2
“Kwa kuwa Biblia iliandikwa zamani sana, watu fulani wanafikiri kwamba haipatane na sayansi. Wewe una wazo gani? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi wanashangaa kuona kwamba Biblia inasema hivi. [Soma Isaya 40:22.] Habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 22 inatoa jibu kwa ulizo, Je, Biblia inapatana na sayansi?”
Mnara wa Mlinzi 01/03/11
“Mashahidi wa Yehova wanajulikana kwa sababu ya kazi yao ya kuhubiri. Je, umekwisha kujiuliza kwa nini tunafanya kazi hiyo? [Acha mutu ajibu.] Ona jinsi andiko hili linavyosema. [Soma Mathayo 24:14.] Gazeti hili linatoa majibu kwa maulizo haya: Hii habari njema ni nini? Ufalme ni nini? Na ule mwisho utakaokuja ni nini?”
Amkeni! Mwezi wa 3
“Kwa kuwa watu wengi wanapambana na magonjwa, tunazungumza na watu kuhusu andiko hili lenye kutia moyo. [Soma Isaya 33:24.] Andiko hili litakapotimia, unafikiri maisha yatakuwa namna gani? [Acha mutu ajibu.] Tunapongojea Mungu alete mabadiliko hayo, kuna mambo ya maana ambayo kila mmoja wetu anapaswa kufanya ili kuwa na afya nzuri. Gazeti hili linazungumzia mambo hayo.”