Kampanye ya Kugawia Watu Mialiko ya Ukumbusho Itaanza Tarehe 2 Mwezi wa 4
1. Ni wakati gani tutaanza kugawia watu mialiko ya Ukumbusho mwaka huu, na kwa nini kampanye hiyo ni ya lazima?
1 Kuanzia tarehe 2 mpaka tarehe 17 mwezi wa 4, tutagawia watu mialiko ya tukio la maana zaidi katika mwaka, yaani, Ukumbusho wa Kifo cha Kristo. Wakati uliopita tulipofanya kampanye hiyo, watu wengi wanaopendezwa walikubali mwaliko huo. Kwa mfano, siku ya Ukumbusho, mwanamke mmoja aliita biro ya tawi kwa njia ya telefone na kusema: “Nimefika nyumbani sasa hivi na nimekuta mwaliko chini ya mlango wangu. Ninapenda kwenda, lakini sijui vizuri ni saa gani tukio hilo litafanyika.” Ndugu wakamuelezea mahali ambapo saa imeonyeshwa kwenye mwaliko. Mwanamke huyo alimalizia mazungumzo kwa kusema, “leo mangaribi nitakuwa kwenye tukio hilo!”
2. Tunaweza kusema nini tunapomtolea mutu mwaliko?
2 Tutafanya Kampanye Hiyo Namna Gani: Kwa kuwa hatuna wakati mwingi ili kutolea kila mkaaji wa eneo letu mwaliko, kwa hiyo ni vizuri kusema kwa kifupi. Tunaweza kusema hivi: “Jambo. Tunapenda kualika familia yako kwenye mwazimisho wa maana sana wa mwaka ambao utafanywa ulimwenguni pote Siku ya Yenga tarehe 17 mwezi wa 4. [Umupe msikilizaji mwaliko.] Ukumbusho wa kifo cha Yesu utafanyika tarehe hiyo. Kutatolewa hotuba ya Biblia bila malipo; hotuba hiyo itaeleza jinsi tunavyoweza kufaidika na ukombozi wa Kristo. Mwaliko huu unaonyesha adresi na saa ya mkutano huo.”
3. Namna gani tunaweza kualika watu wengi iwezekanavyo?
3 Ikiwa kutaniko lenu lina eneo kubwa, wazee wanaweza kuwaomba muache mialiko mahali ambapo hamukute watu nyumbani; mutawaachia mialiko hiyo mahali ambapo haitaonekana na wapita-njia. Musisahau kualika watu munaorudilia, watu wa jamaa, wafanyakazi wenzenu, wanafunzi wenzenu, na watu wengine munaofahamiana nao. Munapogawia watu mialiko miisho ya juma, muwatolee pia magazeti inapowezekana. Je, unaweza kuwa painia msaidizi katika mwezi wa 4 ili ushikiri sana katika kampanye hii yenye kufurahisha?
4. Kwa nini tunataka wale wanaopendezwa na ukweli wahuzurie Ukumbusho?
4 Wale wanaopendezwa na ukweli watakaohuzuria, watapata ushahidi wenye nguvu kabisa! Wataelewa upendo mkubwa wa Yehova uliomsukuma kutoa ukombozi. (Yoh. 3:16) Watajifunza namna Ufalme wa Mungu utakavyoletea wanadamu baraka. (Isa. 65:21-23) Wataombwa pia kuzungumza na wakaribishaji na kuomba funzo la Biblia ikiwa wanapenda kujifunza habari zaidi. Tunasali ili wale walio na mioyo mizuri wakubali mwaliko huu na wajiunge nasi ili tuhuzurie pamoja Ukumbusho!