Utoaji Mbalimbali
Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 9
“Watu wa mahali pote na walio na dini mbalimbali wanasali kila siku. Je, unafikiri kwamba Mungu anasikiliza na kujibu sala zote?” Acha mutu ajibu. Kisha umtolee Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1 mwezi wa 9 na muchunguze pamoja habari iliyo kwenye kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16 na musome andiko moja hivi kati ya maandiko yanayotajwa. Tolea mutu magazeti, na ufanye mipango ya kurudia ili kuendelea na ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/09/11
Onyesha mutu gazeti, kisha uliza hivi: “Namna gani unaweza kujibu ulizo hili? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema. [Soma 1 Yohana 5:19.] Kulingana na andiko hilo, dunia inatawaliwa na “yule mwovu,” ao Shetani. Lakini hilo linatokeza maulizo fulani. Shetani alitoka wapi? Je, ni mutu ambaye anaishi kabisa? Mungu atamuruhusu kutawala mpaka wakati gani? Utapata majibu ya Biblia katika gazeti hili.”
Amkeni! Mwezi wa 9
“Watu wengi leo hawajue la kufanya kwa sababu ya matatizo ya kupata feza. Unafikiri kwa nini ni vigumu kupata feza za kutosha ili kutosheleza mahitaji yetu? [Acha mutu ajibu.] Biblia ina mashauri yenye hekima ambayo imesaidia wengi wajue jinsi ya kutumia feza zao vizuri. [Soma andiko moja kati ya maandiko yaliyo kwenye ukurasa wa 8-9.] Gazeti hili linatoa mapendekezo yenye kufaa kwa ajili ya wale walio na madeni.”