Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 10
“Niko hakika utakubaliana na mimi kwamba maisha yanaonekana kuwa mafupi sana. Unawaza kwamba siku moja wanadamu wataweza kumaliza magonjwa na hivyo kurefusha maisha ya watu? [Acha mutu ajibu.] Ona wazo lililo katika gazeti hili.” Umupatie musikilizaji Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 10, na muzungumuzie pamoja habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16 na maandiko yaliyo hapo. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili muzungumuzie ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/10/12
“Tunawatembelea kwa sababu watu wengi wanahangaishwa na kuongezeka kwa rushwa (ao kikata-midomo) katika mambo ya biashara na ya serikali. Unawaza ni nini inayoweza kufanywa ili kumaliza jambo hilo? [Acha mutu ajibu.] Ona jinsi Yesu atakavyowatendea wale wanaohangaishwa kwa sababu ya rushwa. [Soma Zaburi 72:12-14.] Gazeti hili linaonyesha jinsi karibuni rushwa itakwisha.”
Amkeni! Mwezi wa 10
“Wazazi wengi wanataka watoto wao wapate elimu nzuri. Wewe unafikiri vijana wanaomaliza masomo siku hizi wanatayarishwa vizuri ili kupambana na matatizo ya maisha? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema kuhusu umaana wa kupata ujuzi na hekima. [Soma Mhubiri 7:12.] Gazeti hili linaonyesha mambo matano ya kufanya ili kuwasaidia vijana waweze kuwa na elimu nzuri.”