Namna ya Kufaidika na Kikundi Chenu cha Mahubiri
1. Ni faida gani za Funzo la Kitabu la Kutaniko tunazoendelea kupata kupitia vikundi vyetu vya Mahubiri?
1 Je, unakumbuka sehemu fulani za Funzo la Kitabu la Kutaniko? Vikundi vilikuwa na washiriki wachache hivi kwamba walijisikia wenye kutulia zaidi. Hilo lilifanya iwe rahisi kuanzisha urafiki na ndugu na dada, na lilitusaidia kubaki nguvu kiroho. (Met. 18:24) Mwangalizi wa funzo la kitabu alijua hali ya kila mushiriki wa kikundi, kwa hiyo angeweza kumutolea kila mumoja wao kitia moyo. (Met. 27:23; 1 Pet. 5:2, 3) Hata leo kupitia vikundi vyetu vya mahubiri tunaendelea kupata faida kama hizo.
2. Namna gani tunaweza kuchukua hatua ya kuanzisha urafiki wenye kutia moyo pamoja na washiriki wengine wa vikundi vyetu vya mahubiri?
2 Chukua Hatua: Kwa kawaida, hesabu ya watu walio katika vikundi vya mahubiri ni sawa na ile ya watu waliokuwa katika vikundi vya funzo la kitabu. Tunapohubiri “pamoja” na wengine, tunaweza kufanya urafiki nao. (Flp. 1:27) Katika kikundi chenu, wewe umekwisha kuhubiri na watu ngapi? Kuhusiana na hilo, je, unaweza ‘kupanuka’? (2 Kor. 6:13) Pia, wakati fulani tunaweza kualika ndugu ao dada fulani wa kikundi chetu ajiunge nasi katika Ibada yetu ya Familia ya mangaribi ao kuchangia pamoja nasi chakula. Katika makutaniko fulani, kila kikundi kinapewa daraka la kumukaribisha musemaji mugeni. Wakati ni juma la kikundi fulani kumupokea, washiriki wa kikundi hicho wanakula pamoja na kutiana moyo hata ikiwa musemaji hatakula pamoja nao.
3. Tuna nafasi gani za kufaidika na kazi ya uchungaji katika vikundi vyetu vya mahubiri?
3 Hata kama leo washiriki wa kutaniko wanakutana mara mbili tu kwa juma, hilo halimaanishe kama wahubiri hawafaidike kabisa na kazi ya uchungaji. Waangalizi wa vikundi wanawekwa ili kumutolea kila mushiriki wa kikundi kitia moyo na kumuzoeza katika mahubiri. Ikiwa mwangalizi wa kikundi hajapanga kuhubiri pamoja nawe, unaweza kumuambia kwamba unataka kuhubiri pamoja naye. Tena, mara moja kila mwezi, mwangalizi wa utumishi anapanga kuhubiri pamoja na kikundi kimoja mwishoni mwa juma, ni kusema Siku ya Posho na Siku ya Yenga. Katika makutaniko yaliyo na vikundi vichache, mwangalizi wa utumishi anaweza kupanga kutembelea kila kikundi mara mbili kwa mwaka. Je, unapanga programu yako ili kuhubiri wakati mwangalizi wa utumishi anatembelea kikundi chenu?
4. (a) Namna gani mikutano kwa ajili ya mahubiri inapangwa? (b) Sababu gani tufikirie kujitolea ili nyumba yetu itumiwe kwa ajili ya mikutano ya mahubiri?
4 Kwa kawaida, ni vizuri zaidi kila kikundi kikutane peke yake kwa ajili ya mahubiri mwishoni mwa juma. Kuwa na mahali mbalimbali ambapo vikundi vinafanyia mukutano kwa ajili ya mahubiri kwa karibu saa ileile kunaweza kufanya iwe rahisi kwa wahubiri kuenda kwenye mikutano kwa ajili ya mahubiri na labda kwenye eneo. Wahubiri wanaweza kupangwa haraka na kuanza kujielekeza kwenye eneo bila kuchelewa. Pia, ni rahisi zaidi kwa mwangalizi wa kikundi kushugulikia kila mushiriki wa kikundi. Lakini, hali fulani zinaweza kufanya liwe jambo la hekima kuunganisha pamoja vikundi viwili ao zaidi. Ikiwa kutaniko lote linakutana pamoja kwa ajili ya mahubiri Siku ya Posho ya kwanza ya mwezi ao kisha Funzo la Munara wa Mulinzi, kwa kawaida, ni jambo lenye kufaa washiriki wa kila kikundi wakae pamoja na kuachia kila mwangalizi dakika fulani ili kupanga washiriki wa kikundi chake, mbele ya kumalizia na sala mukutano wa mahubiri.—Ona kisanduku “Unaweza Kujitolea ili Nyumba Yako Itumiwe?”
5. Ijapokuwa mupango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko umekwisha, tunaweza kuwa na uhakika gani?
5 Ijapokuwa mupango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko umekwisha, Yehova anaendelea kututolea mambo tunayohitaji ili tufanye mapenzi yake. (Ebr. 13:20, 21) Chini ya ulinzi wa Yehova hatukose chochote. (Zab. 23:1) Tunapata baraka nyingi kupitia vikundi vyetu vya mahubiri. Ikiwa tunachukua hatua ya ‘kupanda kwa wingi,’ “tutavuna pia kwa wingi.”—2 Kor. 9:6.
[Sanduku katika ukurasa wa 6]
Unaweza Kujitolea ili Nyumba Yako Itumiwe?
Katika makutaniko fulani vikundi vya mahubiri vinakutana pamoja mwishoni mwa juma kwa sababu hakuna nyumba za kutosha za kutumia kwa ajili ya mukutano wa mahubiri. Mikutano kwa ajili ya mahubiri ni sehemu ya mipango ya kutaniko. Kwa hiyo, ni pendeleo kabisa ikiwa mikutano hiyo inafanywa katika nyumba yako. Unaweza kukubali nyumba yako itumiwe? Usijizuie kwa sababu nyumba yako ni ndogo. Wazee watafikiria jambo hilo; wataona mahali ambapo nyumba yako inapatikana na kufikiria mambo mengine yanayofanana na yale yaliyofikiriwa wakati wa kuchagua mahali pa kufanyia funzo la kitabu. Ikiwa ungependa nyumba yako itumiwe, ni vizuri umujulishe mwangalizi wa kikundi chenu.