Ona Mema kwa Sababu ya Kazi Yako Ngumu
1. Ni nini kinachoweza kutufanya tupunguze bidii yetu katika mahubiri?
1 Mungu alipomuumba mwanadamu, alikusudia mwanadamu ‘aone mema kwa sababu ya kazi yake ngumu.’ (Mhu. 2:24) Lakini, ikiwa hatupate matokeo mazuri katika mahubiri, tunaweza kuvunjika moyo na hivyo kupoteza furaha yetu na kupunguza bidii yetu. Ni nini kinachoweza kutusaidia tuendelee kuwa na maoni yanayofaa juu ya kazi yetu ya kuhubiri?
2. Sababu gani hatupaswe kufikiri kama watu wote watakubali ujumbe wetu?
2 Usifikiri Kama Watu Wote Watakubali: Kumbuka kwamba hata kama ni watu wachache tu ndio waliokubali mafundisho ya Yesu, bila shaka mahubiri yake yalikuwa na matokeo mazuri. (Yoh. 17:4) Katika mufano wake wa mupandaji, Yesu alitabiri kwamba mwishowe mioyo ya watu wengi zaidi haingekubali ujumbe wa ufalme unaofananishwa na mbegu. (Mt. 13:3-8, 18-22) Hata hivyo, kwa kuwa tunajikaza sana, tunatimiza kazi kubwa.
3. Namna gani tunaweza ‘kuzaa matunda’ iwe watu wanakubali ujumbe wetu ao hapana?
3 Namna ya Kuzaa Matunda Mengi: Kulingana na mufano wa Yesu, wale wanaokubali ujumbe ‘wanazaa matunda.’ (Mt. 13:23) Kisha ngano kuota na kukomaa, haizae muti mudogo wa ngano lakini inazaa mbegu mupya. Kwa hiyo, matunda ambayo Mukristo anazaa hayafananishe tu wanafunzi wapya, lakini yanafananisha kupanda mbegu nyingi za ufalme, ni kusema, kuhubiri kuhusu Ufalme. Kwa kufanya hivyo tunaona “mema” ambayo inaweza kutufurahisha, iwe watu wanakubali ujumbe wetu ao hapana. Tunashiriki katika kulitakasa jina la Yehova. (Isa. 43:10-12; Mt. 6:9) Tuna pendeleo la kutumika pamoja na Mungu. (1 Kor. 3:9) Na “tunda la midomo” yetu linamufurahisha Yehova.—Ebr. 13:15, 16.
4. Huduma yetu inaweza kuwa na matokeo gani mazuri bila sisi kujua?
4 Tena, tujue kama kazi yetu ngumu inaweza kuendelea kuwa na matokeo mazuri ambayo hatuone. Inawezekana watu fulani waliosikiliza mafundisho ya Yesu walifikia kuwa wanafunzi wake kisha yeye kumaliza huduma yake duniani. Vilevile, mbegu tunazopanda zinaweza kuota na kukomaa katika moyo wa mutu baada ya muda, na mutu huyo anaweza kuikubali kweli bila sisi kujua. Kwa kweli, kazi yetu ya kuhubiri inatimiza mambo mengi mema. Kwa hiyo, acheni ‘tuendelee kuzaa matunda mengi’ na kujionyesha kuwa wanafunzi wa Yesu.—Yoh. 15:8.