Tumia Adresi Yetu ya Internete Inayokubaliwa Kisheria kwa Ajili ya Funzo la Pekee ao Ibada ya Familia
Soma Magazeti ya Hivi Karibuni Kwenye Internete: Soma Munara wa Mulinzi na Amkeni! kwenye Internete majuma mengi mbele magazeti hayo yafike katika kutaniko. Sikiliza usomaji uliorekodiwa wa magazeti.—Fungua “Vichapo/Magazeti.”
Soma Habari Zinazopatikana tu Kwenye Internete: Soma habari kama vile, “Kwa Ajili ya Vijana,” “Ninajifunza Biblia,” “Mazungumzo ya Familia,” na “Vijana Wanauliza;” kwa sasa habari hizo zinapatikana tu kwenye Internete. Fungua jw.org, na chunguza habari fulani kati ya hizo unapofanya funzo lako la pekee ao wakati wa ibada ya familia.—Fungua neno “Mafundisho ya Biblia/Watoto” ao “Mafundisho ya Biblia/Vijana.”
Pata Habari za Sasa: Soma habari zenye kutia moyo na mambo yaliyotokea na utazame video zinazoonyesha jinsi kazi yetu inavyoenea duniani pote. Habari fulani kuhusu misiba na kuteswa kwa ndugu zetu zinaweza kutusaidia kutaja matatizo ya ndugu zetu waliopatwa na misiba tunapowaombea. (Yak. 5:16)—Fungua neno “Habari.”
Tafuta Habari Ukitumia Neno Maktaba Kwenye Internete: Ikiwa maktaba hiyo inapatikana katika luga yako, tumia ordinatere ao telefone ya mukononi iliyo na internete ili kusoma andiko la siku ao ili kutafuta habari katika vichapo fulani vya hivi karibuni.—Fungua neno “Vichapo/Maktaba Kwenye Internete,” ao andika www.wol.jw.org mahali palipotayarishwa ili kuandika adresi ya Internete ambayo mutu angetaka kufungua.
[Muchoro kwenye ukurasa wa 4]
(Ili kuona maelezo hayo, ona kitabu)
Jaribu kutumia jw.org
1 Finyanga kwenye picha ao kwenye neno “chukua.” Picha inaonyeshwa katika aina PDF. Uichapishe na utolee mutoto wako karatasi hiyo ili ajibu na kujifunza kutokana nayo.
2 Finyanga alama ya kufungua ili kutazama video.