‘Tupende Ushirika Muzima wa Akina Ndugu’
Maneno haya yaliyoongozwa na roho na yanayofanyiza kichwa cha habari hii yaliandikwa kumepita karibu miaka elfu mbili. (1 Pet. 2:17) Hata hivyo, ni lazima tuyatumie leo kuliko wakati mwengine wowote! Inawezekana namna gani kuwapenda ndugu walio duniani pote? Katika dunia hii ambamo watu hawapendane, tunaweza kufanya nini ili kuhakikisha kwamba upendo wetu haupoe hata kidogo? (Mt. 24:12) Ona ikiwa unaweza kujibu maulizo yanayofuata unapotazama video Toute la communauté des frères (Ushirika Muzima wa Ndugu Zetu).
(1) Ni wakati gani tuliingia katika ushirika wa duniani pote wa ndugu zetu Wakristo? (2) Mashahidi wa Yehova wote duniani pote wanashiriki katika mambo gani matatu? (3) Namna gani ndugu zetu wanaonyesha kama wameazimia kuhubiri (a) katika eneo kubwa la Alaska, (b) katika bandari (port) kubwa za Ulaya, na (c) katika misitu mikubwa ya Peru? (4) Sababu gani hatupaswe kuwaza hata kidogo kama kuhubiri ni kazi ya kawaida tu? (5) Toa mifano inayoonyesha namna ambavyo Mashahidi wa Yehova wamefariji wenzao na kutegemezana (a) kisha matetemeko ya udongo, (b) kisha upepo mukali, na (c) wakati wa vita vya wanainchi wenyewe kwa wenyewe? (6) Kila mumoja wetu anaweza kufanya nini ili kuonyesha ile alama inayotutambulisha kuwa wakristo wa kweli? (Yoh. 13:35) (7) Ni faida gani tunazopata ikiwa tunatumika pamoja tunapojenga Majumba yetu ya Ufalme? (8) Namna gani ndugu zetu katika Ulaya ya Mashariki na Russie walibaki waaminifu kwa Yehova wakati serikali ilikataza kazi yetu? (9) Mashahidi wengi wanajikaza kadiri gani ili kuhuzuria mikusanyiko, na wanafanya hivyo sababu gani? (10) Namna gani video hii imekusaidia uazimie zaidi (a) kumuabudu Yehova kwenye mikutano ya Kikristo kwa umoja pamoja na ndugu na dada, (b) kuwasaidia wengine wakati wana lazima ya musaada, na (c) kuhubiri kwa uaminifu wakati wowote na kwa namna yoyote unavyoweza? (11) Tunaweza kutumia video hii katika mahubiri wakati gani na namna gani?
Sababu yetu kubwa ya kuwa katika ushirika wa duniani pote wa ndugu zetu Wakristo ni upendo wetu kwa Yehova. Kwa hiyo, tunapenda kujifunza juu ya Yehova na kuwafundisha wengine juu yake. Tena tunawapenda watu ambao Yehova anapenda. Wakati tunawasaidia wanapokuwa na lazima ya musaada, hatutazamie Mungu atushukuru. Badala yake, tunamushukuru Mungu kwa sababu tunaona ushirika wa duniani pote wa ndugu zetu Wakristo kuwa zawadi kutoka kwake. Kwa kuwa mwisho wa dunia hii ambamo watu hawapendane unakaribia, acheni tuendelee kupenda ushirika muzima wa ndugu zetu!