Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/13 uku. 4-7
  • Namna ya Kutumia Broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kutumia Broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tutangaze Habari Njema Ya Ufalme Kwa Msaada Wa Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tutumie Broshua Mbalimbali Katika Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tumwige Yehova Kwa Kuhangaikia Kwelikweli Wengine
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kufundisha kwa Kutumia Broshua Habari Njema
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2013
km 3/13 uku. 4-7

Namna ya Kutumia Broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!

Broshua Mupya ili Kutusaidia Kurudilia Watu na Kuanzisha Mafunzo ya Biblia

1. Ni broshua gani mupya iliyotolewa kwenye Mukusanyiko wa Wilaya “Linda Moyo Wako!” ili kutusaidia kurudilia watu na kuanzisha mafunzo ya Biblia?

1 Kwenye Mukusanyiko wa Wilaya “Linda Moyo Wako!” tulifurahi kupokea broshua mupya ili kutusaidia kurudilia watu na kuanzisha mafunzo ya Biblia. Broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu! imechukua nafasi ya broshua Mungu Anataka. Broshua hiyo inafanana na broshua Mungu Anataka kwa kuwa ina masomo mafupimafupi. Hilo litatusaidia kupata matokeo mazuri tunapoanzisha mafunzo ya Biblia kwenye mulango. Tofauti kati ya broshua hizo mbili ni kwamba, broshua Mungu Anataka inazungumuzia mambo yanayoombwa kwa Mukristo ambayo inaweza kuwa vigumu kwa wanafunzi wapya kukubali, lakini broshua hiyo mupya inakazia habari njema inayopatikana katika Biblia.—Mdo. 15:35.

2. Sababu gani broshua Habari Njema ilichapishwa?

2 Sababu gani ilichapishwa? Ulimwenguni pote, ndugu wamekuwa wakiomba kichapo rahisi ambacho kinaweza kuwavuta watu kwenye kweli na kuwaongoza kwenye kitabu Biblia Inafundisha, kitabu chetu cha funzo. Mara nyingi watu wanaoogopa kujifunza kwa sababu ya ukubwa wa kitabu wanapendelea kujifunza Biblia kupitia broshua. Pia, ni rahisi kutafsiri broshua katika luga nyingi zaidi.

3. Namna gani broshua hii ni tofauti na vitabu vingine vya funzo?

3 Namna Inavyopangwa: Vichapo vingi vya funzo vya Mashahidi wa Yehova vinaandikwa ili watu wavisome na kuielewa kweli ya Biblia, hata bila musaada wa mutu mwengine. Broshua hii ni tofauti. Ili kuielewa, inaomba kuwe mwalimu. Kwa hiyo, unapoitolea mutu, ni vizuri zaidi musome na kuzungumuzia fungu moja ao mafungu mawili. Mafungu ni mafupimafupi, kwa hiyo yanaweza kuzugumuziwa kwenye mulango ao mahali pa biashara. Hata ikiwa ni vizuri kuanzia funzo kwenye somo la 1, tunaweza kuanzisha funzo haizuru kwenye somo gani katika broshua.

4. Namna gani broshua hii inatusaidia kufundisha moja kwa moja mambo yanayotoka katika Biblia?

4 Katika vichapo vyetu vingi, majibu ya maulizo yanaweza kupatikana katika mafungu. Lakini katika broshua hii, majibu yanapatikana zaidi sana katika Biblia. Watu wengi zaidi wanataka kujifunza kupitia Biblia kuliko kujifunza kupitia vichapo vyetu. Kwa hiyo, karibu maneno ya maandiko yote yaliyo katika broshua hii hayatajwe moja kwa moja. Yanapaswa kusomwa katika Biblia. Hilo linasaidia wanafunzi watambue kwamba yale wanakujifunza ni maneno ya Mungu.—Isa. 54:13.

5. Sababu gani ni lazima mwalimu atayarishe kila funzo vizuri?

5 Broshua hii haifasirie kila andiko. Sababu gani? Imekusudiwa ili kumuchochea mwanafunzi aulize maulizo na kumuwezesha mwalimu atumie ufundi wake wa kufundisha. Kwa hiyo, ni lazima mwalimu atayarishe vizuri kila funzo. Angalisho: Usiseme mambo mengi. Tunapenda kufasiria Maandiko. Lakini tunatimiza mengi zaidi kwa kumuomba mwanafunzi atoe mawazo yake kuhusu andiko analosoma. Kwa kutumia maulizo kwa busara, tunaweza kumusaidia afikiri kuhusu maana ya kila andiko.—Mdo. 17:2.

6. Namna gani tunaweza kutumia broshua hii: (a) mahali ambapo watu wana mashaka juu ya Mungu na Biblia? (b) tunapohubiri nyumba kwa nyumba? (c) ili kuanzisha mafunzo ya Biblia mara tu tunapokutana na mutu kwa mara ya kwanza? (d) tunapowarudilia watu?

6 Kama vichapo vingine tunavyotumia kwa ajili ya funzo, broshua hii inaweza kutolewa wakati wowote, hata ikiwa si toleo la mwezi. Wahubiri wengi watafurahia kuanzisha funzo la Biblia kwenye mulango mara tu wanapokutana na mutu kwa mara ya kwanza. Zaidi ya hilo, kama ilivyoonyeshwa kwenye mukusanyiko wa wilaya, kuitumia tunapowarudilia wale waliopendezwa “kunaweza kabisa kufanya ziara ya kurudia iwe yenye kufurahisha!”—Ona visanduku kwenye ukurasa wa 5-7.

7. Namna gani unaweza kuongoza funzo la Biblia unapotumia broshua hiyo?

7 Namna ya Kuongoza Funzo: Unaweza kuanza mazungumuzo kwa kusoma maulizo yenye kuandikwa kwa maandishi meusi mazito. Kisha, usome fungu na andiko ao maandiko yaliyo na neno “soma.” Kwa busara, tumia maulizo ili kumusaidia mwanafunzi aelewe maandiko. Mbele ya kuanza sehemu inayofuata, umuombe musikilizaji ajibu maulizo yanayoandikwa kwa maandishi meusi mazito ili uhakikishe kwamba ameelewa mambo anayojifunza. Ziara za kwanza kwanza, ni vizuri zaidi uzungumuzie tu moja ya maulizo yanayoandikwa kwa maandishi meusi mazito. Baada ya muda, munaweza kuzungumuza wakati murefu zaidi na hivyo kujifunza somo nzima.

8. Namna gani tunaweza kutanguliza maandiko, na kwa sababu gani?

8 Maandiko yaliyo na neno “soma” ndiyo yanayotoa moja kwa moja majibu ya maulizo yanayoandikwa kwa maandishi meusi mazito. Unapotanguliza andiko, epuka kusema, “Mutume Paulo aliandika” ao, “Ona yale ambayo Yeremia alitabiri.” Musikilizaji anaweza kufikiri kwamba tunasoma maneno ya wanadamu kama sisi. Itakuwa vizuri zaidi kusema, “Neno la Mungu linasema” ao, “Ona yale ambayo Biblia ilitabiri.”

9. Je, maandiko yote yanapaswa kusomwa wakati wa funzo?

9 Je, tunapaswa kusoma maandiko yote ao yale tu yaliyo na neno “soma”? Hilo litategemea hali. Maandiko yote yanayopatikana katika somo yako hapo kwa kusudi fulani. Kila andiko lina habari ya maana inayoombwa kuzungumuziwa. Lakini, wakati fulani wanafunzi wanakosa wakati, hawapendezwe, ao uwezo wao wa kusoma unaweza kutufanya tusome tu maandiko yaliyo na neno “soma.”

10. Tunaweza kuhamishia funzo katika kitabu Biblia Inafundisha wakati gani?

10 Wakati wa Kuhamishia Funzo Katika Kitabu Biblia Inafundisha: Kisha kuzungumuzia mara nyingi broshua hiyo na ikiwa funzo limefanywa kwa ukawaida, tunaweza kuhamishia funzo hilo katika kitabu Biblia Inafundisha ao kuendelea na broshua Habari Njema mupaka mwisho. Wahubiri watatumia akili ili kuamua ni wakati gani hasa wanaweza kuhamishia funzo katika kitabu Biblia Inafundisha. Tunapofanya hivyo, je tunapaswa kuanza funzo mwanzoni mwa kitabu Biblia Inafundisha? Hakuna sheria yoyote kuhusu jambo hilo. Watu wanatofautiana. Lakini, wanafunzi wengi zaidi watafaidika wanapojifunza tena katika kitabu Biblia Inafundisha habari walizojifunza katika broshua Habari Njema.

11. Sababu gani tunapaswa kutumia vizuri broshua hii mupya?

11 Katika dunia inayojaa habari mbaya, tuna pendeleo kubwa la kutangaza habari nzuri zaidi—kwamba Ufalme wa Mungu unatawala na kwamba karibuni utaanzisha Dunia mupya ambamo mutakuwa uadilifu! (Mt. 24:14; 2 Pet. 3:13) Tuko hakika kwamba wengi ambao wanasikiliza ujumbe huo watakubaliana na maneno hayo yenye kuongozwa na roho: ‘Jinsi inavyopendeza juu ya milima miguu ya yeye anayeleta habari njema, yeye anayetangaza amani, yeye anayeleta habari njema za jambo bora, yeye anayetangaza wokovu, yeye anayeuambia Sayuni: Mungu wako amekuwa mufalme!’ (Isa. 52:7) Acheni basi tutumie broshua hii mupya ili kuwaletea watu wenye kiu cha neno la Mungu walio katika eneo letu habari njema inayotoka kwa Mungu!

[Sanduku katika ukurasa wa 5]

Mahali Ambapo Watu Wana Mashaka juu ya Mungu na Biblia:

● Katika maeneo fulani, wahubiri wametambua kwamba maneno “Mungu” na “Biblia” yanawafanya watu wapinge ujumbe wao. Katika maeneo kama hayo, unapomutembelea mutu kwa mara ya kwanza, inaweza kuwa vizuri zaidi kuzungumuzia mambo ambayo watu wanahangaikia, kwa mufano, ulazima wa kuwa na serikali nzuri, mahali pa kupata musaada unaofaa kwa ajili ya familia, na mambo tunayotazamia wakati ujao. Labda, unaweza kuwaonyesha watu broshua Habari Njema baada ya kuzungumuza nao mara nyingi kuhusu namna tunavyojua kwamba Mungu iko, na sababu gani Biblia ni kitabu chenye kutumainika.

[Sanduku katika ukurasa wa 6]

Tunapohubiri Nyumba kwa Nyumba:

● “Nawatembelea ili kuwaonyesha namna inaweza kuwa rahisi kutambua mambo ambayo Mungu amekusudia wanadamu wakati ujao. Je, umekwisha kujiuliza ikiwa Mungu ataondoa mambo yanayotuletea mateso? [Acha mutu ajibu.] Broshua hii inaonyesha mahali ambapo unaweza kupata jibu la ulizo hilo katika Biblia. [Umutolee broshua, na usome fungu la kwanza katika somo la 1, na andiko la Yeremia 29:11.] Kutokana na hilo, wewe unaona ni jambo lenye akili kufikiri kama Mungu anataka watu wawe na maisha mazuri zaidi wakati ujao? [Acha mutu ajibu.] Ukitaka, nitakuachia broshua hii. Nitakapokuja, tutazungumuzia fungu la pili ili tupate jibu la Biblia kwa ulizo hili, ‘Namna gani Mungu ataondoa mambo yanayowaletea wanadamu mateso?’” Ikiwa musikilizaji anaonekana ana wakati mwingi unapomutembelea kwa mara ya kwanza, unaweza kusoma na kuzungumuzia fungu la pili na maandiko matatu yaliyo ndani. Ufanye mipango ya kumurudilia ili muzungumuzie ulizo la pili katika somo hilo.

● “Watu wengi wanapenda kusali, zaidi sana wakati wana magumu. Je, wewe pia unasali wakati fulani? [Acha mutu ajibu.] Je, unafikiri kwamba Mungu anasikiliza sala zote, ao tunaweza kusema kwamba sala fulani hazimupendeze? [Acha mutu ajibu.] Nina broshua hapa inayoonyesha namna ya kupata majibu ya Biblia kwa maulizo hayo. [Umutolee broshua, na muzungumuzie pamoja fungu la kwanza la somo la 12 na maandiko yenye neno “soma.”] Hauone ni ajabu kwamba Mungu iko tayari kutusikiliza? Lakini ili tufaidike zaidi na sala, ni lazima tumujue Mungu vizuri. [Fungua somo la 2 la broshua na umuonyeshe vichwa vidogovidogo.] Ukipenda, ninaweza kukuachia broshua hii, na siku ingine tunaweza kusoma majibu ya Biblia kwa maulizo hayo yenye kupendeza.”

● “Nafika hapa kwa sababu watu wanajiuliza ulimwengu huu unaendea wapi. Wewe unafikiri hali zitakuwa nzuri wakati fulani? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi wanashangaa wanapojifunza kwamba Biblia ina habari njema inayotupatia tumaini. Ona maulizo fulani ambayo Biblia inajibu.” Umutolee broshua, na umuombe achague ulizo moja kati ya maulizo yaliyo kwenye ukurasa wa mwisho wa broshua ambalo linamupendeza zaidi. Kisha, fungua mahali palipo somo hilo, na umuonyeshe jinsi tunavyojifunza na watu broshua hiyo. Ufanye mipango ili kurudia na kuzungumuzia ulizo linalofuata katika somo hilo.

[Sanduku katika ukurasa wa 7]

Jaribu Kuanzisha Funzo Unapomuhubiria Mutu kwa Mara ya Kwanza:

● “Nawatembelea ili kuwaelezea kwa muda mufupi kuhusu funzo mupya la Biblia. Broshua hii ina masomo 15 yanayoonyesha mahali ambapo unaweza kupata majibu kwa maulizo ya maana katika Biblia. [Umuonyeshe ukurasa wa kwanza na wa mwisho.] Je, umekwisha kujaribu kuielewa Biblia? [Acha mutu ajibu.] Acha nikuonyeshe, utaona kwamba ni rahisi kujifunza masomo hayo. [Zungumuzia fungu la kwanza la ulizo la 3 katika somo la 3, na musome Ufunuo 21:4, 5. Ikiwa inafaa, muzungumuzie fungu linalofuata na maandiko yenye neno “soma.”] Ukipenda, ninaweza kukuachia broshua hii. Tunakuomba ujaribu kujifunza Biblia kupitia broshua hii hata mara moja. Ikiwa unaipenda, unaweza kuendelea. Nitakapokuja, tunaweza kuzungumuzia somo la kwanza. Ona kwamba somo hilo lina ukurasa mumoja tu.”

[Sanduku katika ukurasa wa 7]

Umuonyeshe Mutu Broshua Hiyo Unapomurudilia:

● Unapomurudilia mutu aliyependezwa unaweza kusema: “Nafurahi kukuona tena. Nilikuletea broshua hii; inatoa majibu ya Biblia kwa maulizo yenye kupendeza. [Umutolee broshua, na umuombe atazame ukurasa wa mwisho.] Ni habari gani inayokupendeza zaidi? [Acha mutu ajibu. Kisha, fungua somo alilochagua.] Acha nikuonyeshe namna unavyoweza kutumia broshua hii ili kupata majibu ya Biblia.” Umuonyeshe namna tunavyojifunza broshua hiyo na watu kwa kuzungumuzia fungu moja ao mafungu mawili na maandiko yenye neno “soma.” Tayari umeanzisha funzo la Biblia! Umuachie musikilizaji broshua, na ufanye mipango ili kumurudilia. Unapomaliza somo hilo, unaweza kuzungumuzia somo lingine ambalo musikilizaji alichagua ao kuanza mwanzoni mwa broshua.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine