Sikiliza na Ujifunze
1. Sababu gani ni lazima tujikaze sana ili tusikilize na kujifunza kwenye mukusanyiko wa wilaya?
1 Karibuni mikusanyiko ya wilaya ya 2013 itaanza. Kazi kubwa imefanywa ili kutayarisha programe itakayotosheleza mahitaji ya kiroho ya watu duniani pote. Je, umefanya mipango ili kuhuzuria siku zote tatu? Mikusanyiko inayokusanya watu wengi sana inaweza kuwa na mambo mengi yenye kukengeusha, kwa hiyo, ni lazima kujikaza sana ili kukazia uangalifu programe. Kwa kuwa mikusanyiko inachukua muda murefu kuliko mikutano, ni lazima kukaza akili kwa muda murefu zaidi. Zaidi ya hayo, safari na mambo mengine yanaweza kuchosha. Ni nini kitakachotusaidia tubaki macho ili tusikilize na kujifunza?—Kum. 31:12.
2. Namna gani tunaweza kutayarisha moyo wetu kwa ajili ya mukusanyiko unaokuja?
2 Mbele Mukusanyiko Uanze: Adresi yetu ya Internete, www.jw.org, inatoa programe ya mukusanyiko iliyo na vichwa vya hotuba; na kila kichwa kinategemea andiko moja ao maandiko mawili ya Biblia. Ikiwa unaweza kutumia Internete, chunguza programe hiyo mbele ya wakati, hilo linaweza kukusaidia utayarishe moyo wako kwa ajili ya mambo yatakayofundishwa. (Ezra 7:10) Wakati wa Ibada yenu ya Familia ya mangaribi, munaweza kutumia wakati ili kuzungumuzia programe ya mukusanyiko unaokuja ili kila mumoja aungojee kwa hamu.
3. Ni nini kitakachotusaidia tusikilize kwa uangalifu?
3 Wakati wa Mukusanyiko: Ikiwezekana, uende ku choo mbele ya programe kuanza. Uzime telefone yako ili usikengeushwe na watu wanaokuita ao wanaokutumia ujumbe ao ili usishawishiwe kutumia watu wengine ujumbe wakati wa mukusanyiko. Ikiwa ni lazima uache telefone yako wazi, uitie katika hali isiyoweza kukengeusha wengine ikiwa mutu anakuita. Ikiwa unatumia chombo kingine cha kielektroniki wakati wa mukusanyiko, ufanye hivyo bila kuwakengeusha wengine. Epuka kula wakati wa mukusanyiko. (Mhu. 3:1) Kazia macho musemaji. Andiko linaposomwa, fuata katika Biblia yako. Andika mambo machache.
4. Namna gani wazazi wanaweza kuwasaidia watoto wao wasikilize na kujifunza?
4 Tunataka pia watoto wetu wasikilize na kujifunza. Methali 29:15 inasema: ‘Muvulana aliyeachiliwa atamuletea mama yake aibu.’ Kwa hiyo, ni vizuri familia ikae pamoja ili wazazi wahakikishe kwamba watoto wao wanafuata programe kwa uangalifu, kuliko kuzungumuza, kutumiana ujumbe, ao kutembeatembea. Hata ikiwa ni wadogo sana hivi kwamba hawawezi kuelewa mambo yote yanayozungumuziwa, watoto wanaweza kuzoezwa kubaki macho na kukaa kimya.
5. Sababu gani ni vizuri kurudilia programe, na namna gani tunaweza kufanya hivyo?
5 Kila Siku Kisha Programe: Urudi nyumbani mapema. Lala mbele ya wakati ili upumuzike vya kutosha. Kurudilia mambo uliyosikiliza kutakusaidia kuyakumbuka kwa muda murefu. Kwa hiyo, ni vizuri kuchukua dakika chache ili kuzungumuzia programe katika familia kila mangaribi. Ikiwa unapitisha wakati pamoja na marafiki, unaweza kuchukua mambo uliyoandika na kuzungumuzia jambo moja ao mambo mawili ambayo ulifurahia sana. Mukusanyiko unapokwisha, wakati wa Ibada yenu ya familia ya mangaribi, munaweza kuzungumuzia namna munavyoweza kutumikisha mambo ambayo mulijifunza kwenye mukusanyiko. Munaweza pia kuchukua wakati kila juma ili kuchunguza vichapo vipya vilivyotolewa.
6. Je, inatosha tu kufika kwenye mukusanyiko? Eleza.
6 Watu wanafaidika na karamu ikiwa wanakula chakula na chakula hicho kinatumika katika miili yao. Ni hivyo pia kuhusu karamu yetu ya kiroho kwenye mukusanyiko wa wilaya. Acheni basi tufaidike kwa kuhuzuria kila sehemu ya programe, kwa kusikiliza kwa uangalifu, na kwa kutumikisha mambo tutakayojifunza.