Mwenendo Unaomutukuza Mungu
1. Sababu gani watu wanatambua kwa urahisi kwamba Mashahidi wa Yehova wana mukusanyiko wa wilaya?
1 Watu wanatambua kwa urahisi kwamba tuna mukusanyiko wa wilaya. Katika miji mingi ambamo Mashahidi wa Yehova wanafanyia mikusanyiko ya wilaya, wapasha-habari wanajulisha watu jambo hilo, na watu wanaoishi katika miji hiyo wanawatambua wageni wengi kupitia kadi za utambulisho wanazovaa. Hapa chini kuna vikumbusho fulani vitakavyotusaidia kumutukuza Mungu kupitia mwenendo wetu tunapokuwa katika muji ambamo mukusanyiko utafanywa.—1 Pet. 2:12.
2. Namna gani tunaweza kumutukuza Mungu kwa kuvalia kwa kiasi tunapokuwa katika muji ambamo mukusanyiko unafanywa?
2 Kuvalia kwa Kiasi: Mara nyingi, namna yetu ya kuvalia kwa kiasi tunapohuzuria mukusanyiko inawavutia wale wanaotutazama. Hata hivyo, namna yetu ya kuvalia wakati mwengine, kwa mufano, tunapokula kwenye restora ao tunaponunua vitu, inaweza kuwavutia hata zaidi watu wanaotutazama. Hata kama wakati wote hatuhitaji kuvalia kama kwenye mikutano, mavazi yetu yanapaswa kuwa yenye kiasi, yenye kuheshimisha, na yasiyo ya ovyoovyo. Watu wanaotutazama wanapaswa kuona tofauti kati yetu na wasio Mashahidi. (Rom. 12:2) Pia, ni lazima tuvae kadi zetu za utambulisho, kwa sababu zinaweza kusaidia watu wajue kwamba tuna mukusanyiko, zinatutolea nafasi za kuhubiri na kututambulisha kwa watu wengine wanaohuzuria mukusanyiko.
3. Namna gani tunaweza kuonyesha uvumilivu na adabu?
3 Uvumilivu na Adabu: Katika nyakati hizi ambamo watu wengi wanajifikiria wenyewe na hawana shukrani, uvumilivu wetu na adabu yetu vitawavutia watu watakaotutazama, kwa mufano watu wanaotumika kwenye hoteli ao restora! (2 Tim. 3:1-5) Tunapowachungia wengine nafasi ya kukaa ao tunapokuwa kwenye mustari ili kupokea vichapo vipya kwenye mukusanyiko, tunapaswa kutafuta, si faida yetu wenyewe, lakini faida ya watu wengine. (1 Kor. 10:23, 24) Kisha kuhuzuria mukusanyiko kwa mara ya kwanza, mwanaume mumoja mwenye kupendezwa alisema, “Sikumbuke hata hotuba moja iliyotolewa siku hiyo, jambo ninalokumbuka ni mwenendo wa Mashahidi wa Yehova.”
4. Sababu gani tufikirie kujitolea kufanya kazi kwenye mukusanyiko ikiwa hali yetu inaturuhusu?
4 Wafanyakazi wa Kujitolea: Wakristo wa kweli wanajulikana kupitia roho yao ya kujitolea. (Zab. 110:3) Je, unaweza kujitolea ili kusaidia kufanya kazi kwenye mukusanyiko? Mahali fulani ambapo mukusanyiko ulifanywa, ndugu na dada karibu 600 walijitolea ili kufanya usafi mbele mukusanyiko uanze. Wafanyakazi wa hapo walisema: “Hatujaona jambo kama hilo! Ni vigumu kukubali kwamba watu hao wote ni wafanyakazi wa kujitolea.” Tunangojea kwa hamu mikusanyiko ya wilaya ya 2013 na nafasi ambazo tutakuwa nazo za kumusikiliza Mungu, kujifunza juu yake, na pia kumutukuza.
[Sanduku katika ukarasa wa 3-6]
Vikumbusho Kuhusu Mukusanyiko wa Wilaya wa 2013
◼ Saa: Siku zote tatu programe itaanza pa saa 2:20 (8h20) asubuhi. Lakini, katika miji mikubwa ifuatayo: Brazzaville, Goma, Kananga, Kikwit, Kinshasa, Kisangani, Kolwezi, Likasi, Lodja, Lubumbashi, Matadi, Mbandaka, Mbuji-Mayi, Mwene Ditu, Pointe Noire na Tshikapa, programe itaanza kila siku asubuhi pa saa 3:20 (9h20). Milango itafunguliwa asubuhi pa saa 1:00 (7h00) ao saa 2:00 (8h00), kulingana na mahali. Wakati muziki wa kufungua utakapoanza, sisi wote tunapaswa kukaa ili programe iweze kuanza kwa utaratibu. Siku ya Tano na Siku ya Posho programe itamalizika mangaribi pa saa 9:55 (15h55) na Siku ya Yenga itamalizika pa saa 8:40 (14h40). Programe itamalizika saa moja baadaye katika miji mikubwa iliyotajwa.
◼ Kuwachungia Wengine Nafasi ya Kukaa: Munaweza kuchungia viti wale tu munaoishi nao, wale munaosafiri nao katika motokari moja ao wale munaojifunza pamoja nao Biblia kwa sasa.—1 Kor. 13:5.
◼ Chakula cha Midi: Inapendekezwa kwamba kila mutu alete kitu fulani cha kula kisicho kizito lakini cha kujenga mwili, kwa mufano: mikate ao keki, matunda, kalanga, vitumbua ao ndazi. Vinywaji kama vile maji, kahawa ao chai vinapaswa kutiwa katika vyombo visivyoweza kuvunjika ili kuepuka aksida. Hairuhusiwe kuleta pombe kwenye mukusanyiko. Ikiwa tunaleta chakula na kinywaji chetu, hatutahitaji kununua vyakula kwa wale wanaouzisha chakula inje. Kuepuka kununua vyakula kwa watu hao kunasaidia kuonyesha kama sisi ni watu safi. (Tafazali, Mujue kama wale wanaouzisha chakula inje hawaruhusiwe kuingia katika eneo la mukusanyiko wakati wowote.—Yoh 2:13-17.)
◼ Usafi: Imeonekana mara nyingi kama wale wanaonunua vyakula inje wanatupa chini makaratasi ao masashe. Hivyo, eneo lote linajaa makaratasi, masashe, machupa ya plastiki, na kazalika. Ikiwa mutu anaamua kununua chakula inje (kwa mufano: bombo, biskwiti, ndazi ao vitumbua, samaki ao chakula kingine) anapaswa kutupa makaratasi ya kufungia vyakula katika chombo cha kutupia uchafu kuliko kuyatupa chini. Tukiona mutu fulani ametupa kipande cha karatasi ao cha plastiki chini, tunapaswa kukiokota na kukitia katika chombo cha kutupia uchafu. Tafazali, tujikaze sana ili kulinda mahali petu pa mukusanyiko na eneo la kandokando vikiwa safi. Kila mutu anayehuzuria anapaswa kuhangaikia usafi. Ikiwa kila mutu anatimiza sehemu yake, mwishoni mwa kila siku, mahali pa mukusanyiko pataachwa pakiwa safi. Tunapenda kuonyesha katika maisha yetu sifa za Mungu mutakatifu ambaye tunaabudu.—1 Pet. 1:15, 16; Kut. 19:10; Kum. 23:14.
◼ Michango: Tunaweza kuonyesha shukrani yetu kwa ajili ya mipango ya mukusanyiko kwa kutoa michango ya kujipendea mahali pa mukusanyiko, ili kutegemeza kazi ya duniani pote. Sheke zote zinazotolewa kwenye mukusanyiko zinapaswa kuandikwa kwa jina « Association ‘Les Témoins de Jéhovah.’ »
◼ Aksida na Mambo Yanayoomba Kutenda kwa uharaka: Ikiwa kunatokea jambo linaloomba kutenda kwa uharaka kwenye mukusanyiko, tafazali unaweza kumuelezea ndugu mukaribishaji aliye karibu ambaye, bila kuchelewa, atajulisha ndugu wanaoshugulika na Matunzo ya Haraka ili waamue ikiwa hali inaomba kutoa musaada unaohitajiwa.
◼ Dawa: Ikiwa unatumia dawa ulizoagizwa na daktari, tafazali usisahau kubeba dawa zako kwa kuwa hazitapatikana kwenye mukusanyiko. Kwa kuwa shindano za wale wanaogonjwa diabete ni zenye hatari, zinapaswa kutupwa mahali panapofaa; hazipaswe kutupwa katika chombo cha kutupia uchafu kwenye mukusanyiko.
◼ Kukamata Picha: Ukikamata picha kwenye mukusanyiko wakati wa kipindi, tafazali usitumie mwangaza (flash). Tafazali, usiwaite mahali pa mukusanyiko wale wanaofanya kazi ya kukamata picha. Ikiwa unawaona wakitafuta mutu wa kukamata picha, usikubali wakukamate picha.—Yoh 2:13-17.
◼ Fomu Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43): Ukikutana na mutu yeyote anayependezwa wakati wa mukusanyiko, unapaswa kutumia fomu Tafadhali Fuatia Upendezi ili kutoa habari kumuhusu mutu huyo. Wahubiri wanapaswa kubeba fomu moja ao mbili kwenye mukusanyiko. Unaweza kuwaachia ndugu kwenye Biro ya Vitabu fomu ulizojaza ili zishugulikiwe, ao umupe mwandishi wa kutaniko lenu unaporudi nyumbani.—Soma Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 11, 2009, ukurasa wa 4
◼ Restora: Fanya jina la Yehova liheshimiwe kupitia mwenendo wako muzuri unapokuwa kwenye restora. Ikiwa ni kawaida kwenu kumupatia mufanyakazi wa restora matabishi kidogo, unaweza kufanya hivyo.
◼ Mahali Ambapo Tunapangishwa:
(1) Usiwe na watu wengi zaidi katika chumba ao nyumba kuliko inavyoruhusiwa ao kukubaliwa na mutu aliyekupangisha kwake.
(2) Ikiwa utavunja ombi lako la kupangishwa, fanya hivyo bila kukawia.
(3) Mbele ya kupika chakula, uliza mwenye nyumba ao ndugu wanaoshugulika na upangishaji kwenye Jumba la Ufalme ili ujue kile kinachohitajiwa ili kuepuka hatari yoyote.
(4) Usipitishe kiasi unapotumia vitu vyovyote vinavyotolewa kwa ajili ya wageni. Kanuni ya mwenendo ni kuwa mwenye kiasi na mwenye usawaziko.
(5) Kila siku, acha mahali ulipopangishwa pakiwa na utaratibu, pakiwa safi. Hilo linahusu pia Jumba la Ufalme, ambalo linaweza kutumiwa kuwa mahali pa kupangisha ndugu waliotoka katika makutaniko ya mbali.
(6) Onyesha tunda la roho unaposhugulika na wengine, iwe ni mwenye nyumba ao ndugu wengine Wakristo ambao labda munapangishwa pamoja nao—Gal. 5:22, 23.
◼ Kazi ya Kujitolea: Yeyote anayetaka kufanya kazi anapaswa kujulisha Biro ya Wafanyakazi Wanaojitolea Kufanya Kazi kwenye mukusanyiko. Watoto walio na miaka chini ya 16 wanaweza kutumika chini ya uongozi wa wazazi wao ao mutu aliyemuleta ao mutu mwengine mwenye kukomaa aliyekabiziwa mutoto huyo na wazazi wake.