Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi wa 8
“Karibu kila mutu anasali wakati fulani. Hata watu fulani ambao hawamuamini Mungu wanasali wanapokuwa katika magumu. Unawaza Mungu anasikiliza sala zote?” Acha mutu ajibu. Umuonyeshe ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 8, na muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Tangazo: Kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri wa tarehe 3 Mwezi wa 8, mutafanya onyesho mukitumia pendekezo lililo hapa juu.
Munara wa Mulinzi 01/08/13
“Tunawatembelea ili kuzungumuza nanyi kwa muda mufupi. Watu wengi wana wasiwasi kwa sababu mambo ya ponografia (picha ao habari za ngono) yameenea sana. Wengine wanaona hakuna hatari yoyote kutazama ponografia. Unawaza nini? [Acha mutu ajibu.] Yesu alisema kwamba tunaweza kujua ikiwa jambo fulani ni nzuri kupitia matokeo ao matunda yake. [Soma Mathayo 7:17.] Gazeti hili linazungumuzia matokeo mabaya ya kutazama ponografia. Inatoa pia mapendekezo yenye kusaidia kuhusu namna ya kuacha kabisa kutazama mambo ya ponografia.”
Amuka! Mwezi wa 8
“Kwa kawaida kila mutu anataka kuishi maisha marefu. Je, unawaza ufundi ambao wanadamu wanaendelea kupata katika mambo ya sayansi utatuwezesha kuishi milele? [Acha mutu ajibu.] Ona ahadi hii yenye kushangaza. [Soma 1 Wakorintho 15:26.] Lakini Mungu atatimiza ahadi hiyo namna gani, je, ni kupitia sayansi ao njia ingine? Na sababu gani leo tunazeeka na kufa? Gazeti hili linatoa majibu ya Biblia kwa maulizo hayo.”