Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/13 uku. 1
  • Neno la Mungu ni Lenye Faida kwa Kufundisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Neno la Mungu ni Lenye Faida kwa Kufundisha
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kusanyiko Lipya La Pekee La Siku Moja
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Linda Akili Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • ‘Mapenzi ya Mungu Yatendeke’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Neno la Mungu Lina Nguvu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2013
km 8/13 uku. 1

Neno la Mungu ni Lenye Faida kwa Kufundisha

1. Mukusanyiko wa muzunguko wa mwaka wa utumishi wa 2014 una kichwa gani, na ni ulizo gani litakalojibiwa kwenye mukusanyiko huo?

1 Yehova, ‘Mufundishaji wetu Mukubwa,’ ndiye mwalimu muzuri zaidi katika ulimwengu wote. (Isa. 30:20, 21) Yehova anatufundisha namna gani? Ametutolea kitabu kizuri zaidi kuliko vitabu vingine vyote, Neno lake lililoongozwa na roho, Biblia. Namna gani mafundisho ya Mungu yanaweza kutufaidi kimwili, kiakili, kihisia, na kiroho? Ulizo hilo litajibiwa kwenye mukusanyiko wetu wa muzunguko wa mwaka wa utumishi wa 2014. Kichwa cha mukusanyiko huo ni “Neno la Mungu Ni Lenye Faida kwa Kufundisha;” kinategemea andiko la 2 Timotheo 3:16.

2. Mambo makubwa ya programu yatatolewa kupitia majibu ya maulizo gani?

2 Tafuta Mambo Makubwa: Mambo makubwa ya programu yatatolewa kupitia majibu ya maulizo yafuatayo:

• Mafundisho ya Mungu yanatusaidia namna gani katika maisha? (Isa. 48:17, 18)

• Ikiwa tunajikaza kufanya mabadiliko ili tuweze kufanya utumishi wa wakati wote, tunaweza kuwa na uhakika gani? (Mal. 3:10)

• Tunapaswa kufanya nini tunapokutana na “mafundisho yaliyo mageni”? (Ebr. 13:9)

• Namna gani tunaweza kuiga ‘njia ya Yesu ya kufundisha’? (Mt. 7:28, 29)

• Sababu gani walimu katika kutaniko wanapaswa kujifundisha wenyewe? (Rom. 2:21)

• Neno la Mungu ni lenye faida katika mambo gani? (2 Tim. 3:16)

• ‘Kutikiswa’ kwa mataifa kunakuwa na matokeo gani juu ya watu? (Hag. 2:6, 7)

• Yehova ana uhakika gani juu yetu? (Efe. 5:1)

• Sababu gani tunapaswa kujikaza sana ili kubaki katika mafundisho ya Yehova? (Lu. 13:24)

3. Sababu gani ni lazima tufike kwenye mukusanyiko huo na kusikiliza kwa uangalifu?

3 Katika 2 Timotheo sura ya 3, mbele ya kuandika maneno yanayofanyiza kichwa cha mukusanyiko huo, Paulo alieleza hali ngumu ambazo zingetokea katika siku za mwisho. Aliandika hivi: ‘Watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi, wakipotosha na kupotoshwa.’ (2 Tim. 3:13) Kwa hiyo, ili tusipotoshwe, ni lazima kwetu kusikiliza na kutumia mafundisho ya Yehova katika maisha yetu. Basi, na tuazimie kufika kwenye mukusanyiko huo na kusikiliza kwa uangalifu programu hiyo ambayo imetayarishwa kwa wakati unaofaa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine