Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Umutegemeze Yule Unayehubiri Naye
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Yesu alitambua kwamba ni lazima kuhubiri na mutu mwengine. Kwa hiyo, alipowatuma wanafunzi 70 wamutangulie katika mahubiri, aliwatuma wawili-wawili. (Lu. 10:1) Wakati muhubiri fulani anakuwa na tatizo la kueleza jambo ao kujibu ulizo fulani, yule anayehubiri naye anaweza kumusaidia. (Mhu. 4:9, 10) Anaweza kumuelezea yule anayehubiri naye mambo aliyokutana nayo katika mahubiri na wakati fulani kumutolea pendekezo ambalo linaweza kumusaidia awe na ufundi katika mahubiri. (Met. 27:17) Munapotoka kwenye nyumba fulani kuelekea nyumba nyingine, munaweza pia kuwa na maongezi yenye kujenga.—Flp. 4:8.
Namna ya Kufanya:
• Sikiliza muhubiri mwenzako anapotoa ushahidi. (Yak. 1:19) Andiko linaposomwa, fuata katika Biblia yako. Utakuwa tayari kusaidia wakati inaomba kufanya hivyo.
• Utumie hekima ili kujua ikiwa unaweza kusaidia ao wakati ambao unaweza kutoa maelezo yako. (Met. 25:11) Ikiwa mwenzako anaongoza funzo la Biblia, unaweza kutoa maelezo wakati fulani, lakini si kila mara. Hata hivyo, munapohubiri nyumba kwa nyumba, ikiwa ni wakati wa mwengine kuhubiri, umuachie basi mazungumuzo. Ni kweli, ikiwa yeye ni muhubiri mupya ao ikiwa hana uwezo wa kushinda kizuia-mazungumuzo fulani, ni vizuri umusaidie. Lakini, iwe unamushindikiza mwenzako katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba, munawarudilia watu, ao munaongoza mafunzo ya Biblia, usimukatize, usitawale mazungumuzo, ao kuingiza habari tofauti na ile munayozungumuzia.
• Umutolee mapendekezo. Ikiwa, wakati fulani, unaweza kumutolea yule unayehubiri naye pendekezo ili kumusaidia awe na ufundi zaidi katika mahubiri, usijizuie kufanya hivyo. (Met. 3:27) Kwa wakati unaofaa, unaweza kutanguliza hivi: “Unafikiri mahubiri hayo yalikuwa namna gani?” ao “Naweza kukutolea musaada fulani?” ao “Mimi ninafanya hivi.” Lakini, kumbuka kwamba, ijapokuwa wakati fulani watu wanapendezwa na musaada wanaopewa, kuwasaidia kila mara wanapokosea kunaweza kuwavunja moyo.
Tumikisha shauri Hili Katika Mwezi:
• Kisha kuhubiri na ndugu ao dada fulani, umuambie wazo alilotoa ao jambo alilofanya ambalo lilikusaidia kabisa.