Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi wa 5
“Tunatembelea watu ili kuzungumuzia kwa kifupi ulizo la maana sana. [Onyesha ulizo la kwanza kwenye ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 5.] Wewe unawaza nini?” Acha mutu ajibu. Muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili muzungumuzie ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/05
“Tunatembelea watu kwa wakati mufupi kwa sababu watu wengi wanataka kujua mambo ambayo yatatokea wakati unaokuja. Unajisikia namna gani unapofikiria wakati unaokuja? Unaogopa? [Acha mutu ajibu. Kisha musome andiko moja kati ya maandiko yaliyo katika kisanduku “Mambo Ambayo Mungu Ametufunulia Kuhusu Wakati Unaokuja.”] Gazeti hili linazungumuzia mambo fulani ambayo yatatokea wakati unaokuja na linaeleza sababu gani tunapashwa kuwa hakika kwamba yatatokea.”
Amuka! Mwezi wa 5
“Tunatembelea watu kwa wakati mufupi ili kuwasaidia wajue namna ya kupambana na wasiwasi ao mahangaiko. Unakubali kwamba leo watu wana mahangaiko mengi kuliko yale waliyokuwa nayo wakati uliopita? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi wametambua kwamba mashauri ya Biblia yamewasaidia kupambana na mahangaiko yao. Kwa mufano. [Soma Mathayo 6:34.] Gazeti hili linazungumuzia mambo mane yanayotokeza mahangaiko, na linaeleza namna kanuni za Biblia zinaweza kutusaidia kupambana nayo.”
Tangazo: Wafanya-biashara wanaweza kupendezwa sana na gazeti hili.