Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi wa 7
“Unafikiri Mungu anaona namna gani sala zetu? Unawaza kwamba anaona sala zetu kuwa za maana ao anaziona kuwa hazina maana?” Acha mutu ajibu. Umuonyeshe ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 7, na muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
MUNARA WA MULINZI 01/07/14
“Kwa kuwa Mungu ni Mweza-Yote, unafikiri kwamba yeye ndiye anatokeza mambo yote mabaya yanayotendeka duniani? [Acha mutu ajibu. Kisha soma andiko la Yakobo 1:13.] Gazeti hili linaeleza sababu gani mambo mabaya yanatokea na Mungu atafanya nini ili kumaliza uovu na kuteseka.”
Amuka! Mwezi wa 7
“Kila mutu anaweza kupatwa na aina fulani ya musiba, kama vile musiba wa asili, magonjwa hatari, ao kifo cha mutu ambaye tunapenda. Wakati misiba hiyo inatokea, unafikiri kwamba ni jambo la lazima tusivunjike moyo? [Acha mutu ajibu.] Biblia imewasaidia watu wengi wanapopambana na misiba. [Soma Waroma 15:4.] Gazeti hili linaeleza namna gani Biblia inaweza kutusaidia wakati tunapata musiba.”