Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Tujikaze Kuwa na Watu wa Kupelekea Magazeti kwa Ukawaida
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Watu wengi wanafurahia kusoma magazeti yetu lakini hawapendi tujifunze nao Biblia. Pengine wanatosheka na dini yao, ao wanaona kwamba hawana wakati wa kujifunza. Hata hivyo, kwa sababu wanasoma magazeti yetu kwa ukawaida, wanaweza kufikia kuwa na hamu kwa ajili ya Neno la Mungu. (1 Pet. 2:2) Wanaweza kuguswa moyo na habari fulani ya pekee, ao hali zao zinaweza kubadilika. Kuwatembelea kwa muda mufupi na kwa ukawaida kutafanya wajisikie muzuri kuwa pamoja nasi na kutatusaidia tujue mambo yenye wanapenda na matatizo yao. Mwishowe, tunaweza kuanza nao funzo la Biblia.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
Andika majina ya watu wenye unaweza kutolea magazeti kwa ukawaida. Uwatolee magazeti ya sasa, na uwaambie kwamba utawaletea magazeti ya mwezi unaokuja.