Uendelee Kukaza Akili Yako Juu ya Kazi ya Kufanya Wanafunzi
1. Ili watu waokolewe, tunapaswa kufanya nini?
1 Ripoti ya mwaka wa utumishi wa 2014 inaonyesha kwamba watumishi wa Mungu walihubiri habari njema ya Ufalme kwa bidii sana. (Mt. 24:14) Kupitia mahubiri ya nyumba kwa nyumba, kampanye za kutoa trakte na mialiko, na mipango ya kuhubiri mahali pa watu wengi, tunawatangazia watu wengi zaidi ujumbe wa Biblia. Lakini, ili watu waokolewe, tunapaswa kuwasaidia wakuwe wanafunzi wa Yesu kwa kujifunza Biblia pamoja nao.—1 Tim. 2:4.
2. Kila mumoja anapaswa kujiuliza maulizo gani yenye inaweza kumusaidia akuwe tayari kuanzisha funzo la Biblia?
2 Kila Mara, Ukuwe Tayari Kuanzisha Funzo la Biblia: Wakati mutu fulani anapendezwa na ujumbe wa Ufalme, unajikaza kupata adresi na programu yake na kumurudilia bila kukawia ili kuanzisha funzo la Biblia? Ni wakati gani kwa mara ya mwisho ulijikaza kuanzisha funzo la Biblia wakati ulimutembelea mutu fulani kwa mara ya kwanza? Ni wakati gani kwa mara ya mwisho ulianzisha funzo la Biblia na watu wenye unapelekea magazeti kwa ukawaida? Umekwisha kuonyesha video Sababu gani Ujifunze Biblia? na Namna Gani Tunajifunza Biblia na Watu? kwa watu wenye unafanya nao kazi, wanafunzi wenzako, jirani, watu wa jamaa yako, na watu wengine wenye unazoea kuonana nao? Wakati unatumia meza ya kutilia vichapo ili kuhubiri, unajikaza kuambia wale wenye kukamata kichapo cha funzo kwamba tunatumia kichapo hicho ili kujifunza na watu Biblia bila kulipa?
3. Inaomba nini ili tupate matokeo mazuri katika kazi yetu ya kufundisha watu kweli?
3 Yehova na Yesu Wanatusaidia: Yesu alianza na neno ‘muende’ wakati alitoa amri ya ‘kufanya wanafunzi.’ Kwa kuanza na neno hilo, alionyesha kwamba tunapaswa kujikaza na kutafuta nafasi za kufanya wanafunzi. Hata hivyo, hakutuacha tufanye hivyo kwa nguvu yetu wenyewe, lakini alitupatia ahadi kwamba atakuwa pamoja na sisi. (Mt. 28:19, 20) Zaidi ya hilo, Yehova ametupatia roho yake takatifu na pia mazoezi na vyombo mbalimbali vyenye tuko navyo lazima ili tuweze kufundisha watu kweli. (Zek. 4:6; 2 Kor. 4:7) Tunaweza kumuomba atupatie “nia” na nguvu ya kufanya kazi hii ya maana.—Flp. 2:13.
4. Sababu gani tunapaswa kuendelea kukaza akili yetu juu ya kazi ya kufanya wanafunzi?
4 Kazi ya kuhubiri habari njema inatuletea furaha nyingi. Lakini, furaha yetu inaongezeka wakati tunafundisha mutu fulani kweli na kumusaidia atembee pamoja na sisi katika “barabara inayoongoza kwenye uzima.” (Mt. 7:14; 1 Tes. 2:19, 20) Jambo la maana zaidi ni kwamba, wakati tunaendelea kukaza akili yetu juu ya kazi ya kufanya wanafunzi, tunamufurahisha Yehova ambaye “hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.”—2 Pet. 3:9.