Tunapaswa Kujitayarisha ili Tufundishe Muzuri
Kwa karibu mara mbili, watu walimuuliza Yesu kuhusu uzima wa milele, lakini alijibia kila mutu kulingana na mahitaji yake. (Lu. 10:25-28; 18:18-20) Kwa hiyo, hata kama tunajua muzuri mambo yenye kuwa katika kichapo cha funzo, tunapaswa kujitayarisha mbele ya wakati tukifikiria mahitaji ya mwanafunzi. Ni mambo gani mwanafunzi anaweza kuwa na magumu ya kuelewa ao kukubali? Tutasoma naye maandiko gani? Tutajifunza naye mafungu ngapi? Tunaweza kutayarisha mufano, mafasirio, ao maulizo fulani ili kumusaidia mwanafunzi aelewe muzuri kabisa habari hiyo. Zaidi ya hilo, kwa sababu Yehova ndiye anakomalisha mbegu ya kweli katika moyo wa mutu, tunapaswa kumuomba atubariki wakati tunajitayarisha kwa ajili ya funzo, abariki mwanafunzi, na atupatie uwezo wa kumusaidia kiroho.—1 Kor. 3:6; Yak. 1:5.