UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | ZABURI 87-91
Bakia Mahali pa Siri pa Aliye Juu Zaidi
“Mahali pa siri” pa Yehova panatoa ulinzi wa kiroho
Leo, tunapaswa kujitoa kwa Yehova na kubatizwa ili tukae mahali pake pa siri
Watu wenye hawamutumainie Mungu hawajue mahali hapo pa siri
Hakuna mutu ao kitu chenye kinaweza kushawishi wale wenye kuwa mahali pa siri pa Yehova wakose kuwa na imani na wakose kumupenda Mungu
“Mwindaji wa ndege” anajaribu kutukamata katika mutego
Ndege ni waangalifu sana, ni vigumu kuwakamata
Wawindaji wa ndege wanajifunza kwa uangalifu tabia za ndege na wanapanga namna mbalimbali za kuwatega
Kama mwindaji wa ndege, Shetani anachunguza tabia za watu wa Yehova na anawawekea mitego ili kuharibu hali yao ya kiroho
Mitego ine hatari yenye Shetani anatumia:
Kuogopa mwanadamu
Kupenda sana vitu vya kimwili
Mambo ya kujifurahisha yenye haifae
Kukosa kuelewana na wengine