MAISHA YA MUKRISTO
Mafundisho ya Mungu Yanamaliza Chuki
Yehova hana ubaguzi. (Mdo 10:34, 35) Anakubali watu wa ‘mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga.’ (Ufu 7:9) Kwa hiyo, katika tengenezo la Kikristo hamuna nafasi kwa Chuki na upendeleo. (Yak 2:1-4) Kufundishiwa na Mungu kunatusaidia kuishi katika paradiso ya kiroho, mwenye tunaona namna watu wanabadilisha tabia zao. (Isa 11:6-9) Wakati tunajikaza kabisa kuondoa alama yoyote ya chuki katika mioyo yetu, tunaonyesha kama tunamuiga Mungu.—Efe 5:1, 2.
MUANGALIE VIDEO JOHNY NA GIDEON: ZAMANI WALIKUWA MAADUI, SASA NI NDUGU. KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:
Sababu gani mafundisho ya Mungu ni ya hali ya juu kuliko mambo yenye wanadamu wanafanya ili kumaliza ubaguzi na chuki?
Kuhusu undugu wetu wa duniani pote, ni nini inakufurahisha?
Wakati tunaendeleza umoja wetu wa Kikristo, namna gani kufanya hivyo kunamutukuza Yehova?