Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb17 Mwezi wa 4 uku. 5
  • Unaweza Kutia Moyo Wahubiri Wenye Hawatende Tena

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unaweza Kutia Moyo Wahubiri Wenye Hawatende Tena
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Msisahau Wale Ambao Wameacha Kutenda
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • “Munirudilie”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Tuwasaidie Watumikie Tena
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kisanduku cha maulizo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
mwb17 Mwezi wa 4 uku. 5

MAISHA YA MUKRISTO

Unaweza Kutia Moyo Wahubiri Wenye Hawatende Tena

Muchungaji anajaribu kusaidia kondoo mwenye amepotea

Kila mwaka, wahubiri wengi wenye hawatende tena wanahuzuria Ukumbusho. Walianza kukimbia shindano la mbio la uzima lakini wameregeza mwendo kwa sababu mbalimbali; sababu fulani zinapatikana katika broshua Umurudilie Yehova. (Ebr 12:1) Lakini, kwa sababu Yehova aliwanunua kwa damu ya Mutoto yake, wangali wa lazima sana kwake. (Mdo 20:28; 1Pet 1:18, 19) Namna gani tunaweza kuwasaidia wamurudilie Yehova?

Muchungaji anatafuta kwa uangalifu kondoo mwenye amepotea; vilevile wazee wanajikaza sana kutafuta na kusaidia wahubiri wenye hawatende tena. (Lu 15:4-7) Hilo linaonyesha kama Yehova anawahangaikia sana. (Yer 23:3, 4) Sisi wote tunaweza kutia moyo Wahubiri hao, haiko wazee tu. Yehova anafurahi wakati anaona tunajikaza sana ili kuwaonyesha wema na kujitia pa nafasi yao; na hilo linaweza kutuletea baraka nyingi sana. (Met 19:17; Mdo 20:35) Kwa hiyo, fikiria Wahubiri wenye unaweza kutia moyo, na usikawie kuwasaidia!

Dada Laura iko mbele ya dirisha, dada Abbey anasali, dada Abbey na dada Laura wanakumbatiana na wanakamata picha

MUANGALIE VIDEO TUTIE MOYO WAHUBIRI WENYE HAWATENDE TENA, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:

  • Dada Abbey alifanya nini wakati alikutana na Shahidi mwenye hajue?

  • Kama tunapenda kusaidia muhubiri fulani mwenye hatende tena, sababu gani tunapaswa kwanza kuona wazee?

  • Namna gani dada Abbey alijitayarisha ili kumutembelea tena Laura?

  • Namna gani dada Abbey aliendelea kuonyesha uvumilivu na upendo wakati alikuwa anajaribu kumusaidia Laura?

  • Mufano wa Yesu katika Luka 15:8-10 unaweza kutufundisha nini?

  • Dada Abbey alipata Baraka gani kwa kujikaza kumusaidia Laura?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine