Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb17 Mwezi wa 6 uku. 8
  • Furahia Kutangaza Habari Njema

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Furahia Kutangaza Habari Njema
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Muende Mufanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Habari Njema Iko Nahubiriwa Namna Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • ‘Tumikieni Yehova kwa Furaha’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Shangwe—Sifa Yenye Tunapata Kutoka kwa Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
mwb17 Mwezi wa 6 uku. 8

MAISHA YA MUKRISTO

Furahia Kutangaza Habari Njema

Umekwisha kuona kama ni vigumu kuhubiri? Wengi kati yetu wanaona hivyo. Sababu gani? Pengine katika eneo letu watu hawapendezwe na ujumbe, wanatupinga, ao tunaogopa kuzungumuza na watu wenye hatujue. Kwa kweli, mambo hayo yanaweza kufanya furaha yetu ipunguke. Hata hivyo, Mungu mwenye tunaabudu ni Mungu wa furaha, na anapenda tumutumikie kwa furaha. (Zab 100:2; 1Tim 1:11) Ni sababu gani tatu zinafanya tufurahie kazi yetu ya kuhubiri?

Sababu ya kwanza, tunatangaza ujumbe wa tumaini. Hata kama leo watu wengi hawana tena tumaini, tunaweza kujaza mioyo yao na “habari njema za jambo bora.” (Isa 52:7) Lakini habari njema ya Ufalme wa Mungu inaweza kufanya mioyo yetu ijae furaha. Mbele ya kuenda kuhubiri, tufikiri sana juu ya baraka zenye Ufalme wa Mungu utaletea watu katika dunia.

Sababu ya pili, habari njema yenye tunahubiri inasaidia watu kimwili na kiroho. Wanajifunza kuachana kabisa na tabia za mubaya na wanakuwa na tumaini la kuishi milele. (Isa 48:17, 18; Rom 1:16) Tuone kama tunafanya kazi ya kutafuta watu ili kuokoa uzima wao. Hata kama watu fulani hawapendi kuokolewa, tunaendelea kutafuta wale wanapenda kuokolewa.​—Mt 10:11-14.

Sababu ya tatu, na ya lazima zaidi, kazi yetu ya kuhubiri inamutukuza Yehova. Anaona kazi yetu ya kuhubiri kuwa ya lazima sana. (Isa 43:10; Ebr 6:10) Tena, iko tayari kutupatia roho yake takatifu ili tutimize kazi ya kuhubiri. Kwa hiyo, endelea kumuomba Yehova shangwe (furaha), sehemu moja ya tunda la roho. (Gal 5:22) Kwa musaada wa Yehova, tutapiganisha mahangaiko yetu na tutaweza kuhubiri kwa bidii. (Mdo 4:31) Kwa hiyo, hata kama watu wa eneo letu wanatenda namna gani, tutafurahia kutimiza mugao wetu wa kuhubiri.​—Eze 3:3.

Mawazo tofauti juu ya kazi ya kuhubiri—kukosa furaha na kufurahia

Ungependa kuwa na mawazo gani juu ya kazi ya kuhubiri? Namna gani unaweza kuonyesha furaha?

MUANGALIE VIDEO KUJIFUNZA NA KUTAFAKARI KUTAKULETEA TENA FURAHA, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:

  • Hata kama kila mwezi tunahubiri saa nyingi, sababu gani funzo letu linapaswa kuchukua nafasi ya kwanza?

  • Tunaweza kumuiga Maria namna gani?

  • Ni wakati gani unafikiri sana juu ya Neno la Mungu?

  • Ni nini inakufurahisha wakati unahubiri habari njema?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine