MAISHA YA MUKRISTO
Tuonyeshe Sifa Zenye Kumupendeza Mungu—Unyenyekevu
SABABU GANI NI JAMBO LA LAZIMA:
Unyenyekevu unafanya tukuwe marafiki wa sana pamoja na Yehova.—Zab 138:6
Unyenyekevu unafanya tuishi muzuri pamoja na wengine.—Flp 2:3, 4
Kiburi kinaleta matokeo ya mubaya. —Met 16:18; Eze 28:17
NAMNA YA KUFANYA:
Uombe mashauri na uitumikishe. —Zab 141:5; Met 19:20
Fanyia wengine kazi za hali ya chini. —Mt 20:25-27
Usiache mapendeleo yako ao uwezo wako mbalimbali ukuletee kiburi.—Rom 12:3
Ninapaswa kuonyesha unyenyekevu zaidi katika mambo gani?
MUANGALIE VIDEO EPUKA MAMBO YENYE KUHARIBU USHIKAMANIFU—KIBURI, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:
Namna tunatenda wakati tunashauriwa inaonyesha nini juu yetu?
Namna gani sala inatusaidia tuonyeshe unyenyekevu?
Ni katika njia gani mbalimbali tunapaswa kuonyesha unyenyekevu?