MAISHA YA MUKRISTO
Upendo Unatambulisha Wakristo wa Kweli—Tufurahi Pamoja na Kweli
SABABU GANI NI LAZIMA: Tunapaswa kumuiga Yesu kwa kutoa ushahidi kwa ajili ya ile kweli kuhusu mipango ya Mungu. (Yoh 18:37) Tunapaswa pia kufurahi pamoja na kweli, kusema kweli, na kuendelea kufikiria mambo yote yenye kuwa ya kweli, hata kama tunaishi mu ulimwengu wenye kujaa uwongo na ukosefu wa haki.—1Ko 13:6; Flp 4:8.
NAMNA YA KUFANYA:
Ukamate uamuzi wa kukataa kusikiliza ao kusambaza porojo zenye kuumiza.—1Te 4:11
Usifurahie mateso ya wengine
Furahia mambo ya muzuri, mambo yenye kujenga
MUANGALIE VIDEO “MUKUWE NA UPENDO KATI YENU”—USIFURAHIE UKOSEFU WA HAKI, LAKINI UFURAHI PAMOJA NA KWELI, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Namna gani Déborah ‘alifurahia ukosefu wa haki’?
Namna gani Alice alirudisha mazungumuzo yake na Déborah mu njia ya muzuri?
Ni mambo gani ya muzuri tunaweza kuzungumuzia?
Usifurahie ukosefu wa haki, lakini ufurahi pamoja na kweli