MAISHA YA MUKRISTO
Utafanya Nini Mu Mwaka wa Ukame?
Imani na kumutegemea Yehova ni mambo mbili yenye kufanana kabisa. Kwa mufano, kuwa na imani yenye nguvu katika Yehova kunatusaidia tumutegemee na tukuwe hakika kama atatulinda na kutuhangaikia. (Zb 23:1, 4; 78:22) Kadiri tunakaribia sana mwisho wa huu mupangilio wa mambo, tunajua kama Shetani atatutesa hata zaidi. (Ufu 12:12) Ni nini itatusaidia?
MUANGALIE VIDEO UTAFANYA NINI MU MWAKA WA UKAME? NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Ni mu maana gani tuko kama “muti” wenye unazungumuziwa mu andiko la Yeremia 17:8?
Taja aina moja ya “joto.”
“Muti” unapatwa na nini, na juu ya nini?
Shetani anapenda kuharibisha nini?
Ni katika njia gani tuko kama watu wenye wamezoea kutembea mu avion?
Juu ya nini tunapaswa kuendelea kumutegemea mutumwa muaminifu na mwenye busara, na ni majaribu gani yenye tutapata?
Juu ya nini tunapaswa kuendelea kutegemea kanuni za Biblia hata kama watu wako wanatucheka?