UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MAMBO YA WALAWI 1-3
Kusudi ya Matoleo
Zabihu ao matoleo yenye Sheria ya Musa iliomba Waisraeli watoe, ilikuwa inamufurahisha Yehova na ilikuwa inafananisha Yesu na zabihu ya ukombozi ao baraka zenye ile zabihu ingeletea watu.—Ebr 8:3-5; 9:9; 10:5-10.
Vile tu wanyama wote wenye walipaswa kutolewa walipaswa kuwa safi na bila kilema, na njo vile Yesu alitoa mwili wake wenye kukamilika na wenye haukukuwa na kilema.—1Pe 1:18, 19; ona picha ku ukurasa wa kwanza
Vile tu matoleo ya kuteketezwa ilitolewa yote ya muzima kwa Mungu, na njo vile Yesu alijitoa kikamili kwa Yehova
Vile tu wale wenye walitoa zabihu ya ushirika walikuwa na amani pamoja na Mungu, na njo vile watiwa mafuta wenye wanatumia Chakula cha Mangaribi cha Bwana wako na amani pamoja na Mungu