Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb22 Mwezi wa 9 uku. 5
  • Ndoa​—Kifungo ya Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ndoa​—Kifungo ya Maisha
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2022
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Biblia Inasema Nini Juu ya Ndoa na Juu ya Kubakia Bila Kuoa ao Kuolewa?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Ndoa ni Zawadi Iliyotoka kwa Mungu Mwenye Upendo
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Ndoa Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Maisha ya Kisha Siku ya Ndoa
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2022
mwb22 Mwezi wa 9 uku. 5
Bibi na bwana wako wanahubiri pamoya.

MAISHA YA MUKRISTO

Ndoa​—Kifungo ya Maisha

Ndoa za Kikristo zenye kuwa muzuri zinamupatia Yehova heshima na kufanya bibi na bwana wakuwe na furaha. (Mk 10:9) Wakristo wanapaswa kufuata kabisa kanuni za Biblia wakati wa kuchagua mutu wa kuona naye; ile itafanya ndoa yao ikuwe na furaha na ifanye wakati murefu.

Anzisha uchumba kama tu ‘ulishapita mwanzo wa kipindi cha ujana,’ wakati wenye hamu kubwa ya ngono inaweza kufanya ikuwe nguvu kwako kukamata maamuzi ya muzuri. (1Ko 7:36) Mbele ya kuoa ao kuolewa, ujikaze kwanza kufanya urafiki wako pamoya na Mungu ukuwe nguvu na kukomalisha sifa za Kikristo. Ile itasaidia ufanye mambo mingi yenye itafanya ndoa yenu ikuwe na furaha.

Mbele ya kuamua kuoa ao kuolewa, uchukue wakati wa kutosha juu ufikie kujua “ule mutu wa siri wa ndani ya moyo” wa mwenye unapenda kuoana naye. (1Pe 3:4) Kama unakuwa na mashaka sana, muizungumuzie pamoya na ule mwenye unafikiria kuoana naye. Sawa vile inakuwaka tu kati ya marafiki, mu ndoa inaomba kujikaza zaidi kutoa kuliko kupokea. (Flp 2:3, 4) Kama unajikaza kufuata kanuni za Biblia mbele ya kuoa ao kuolewa, utakuwa umeweka musingi muzuri kwa ajili ya maisha ya ndoa yenye kuwa na furaha.

MUANGALIE VIDEO NAMNA YA KUJITAYARISHA KWA AJILI YA NDOA​—SEHEMU YA 3: “KUHESABIA GARAMA,” NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Urafiki kati ya ule dada na Shane ulikuwa namna gani ku mwanzo?

  • Ni mambo gani yenye ule dada alifikia kuvumbua wakati urafiki ulikuwa unaendelea?

  • Wazazi wake walimusaidia namna gani, na alikamata uamuzi gani wa hekima?

Ndugu mwenye iko mu urafiki wa kimapenzi pamoya na dada fulani anaweza kujiuliza hii maulizo:

Iko na sifa gani za Kikristo? Ni nini inonyesha kama anatanguliza kwanza Ufalme? Anaheshimiaka Biblia na miongozo yenye tengenezo inatupatia? Anahangaikiaka wengine?

Dada mwenye iko mu urafiki wa kimapenzi pamoya na ndugu fulani anaweza kujiuliza hii maulizo:

Iko na sifa gani za Kikristo? Anaonaka ibada na madaraka yenye iko nayo mu kutaniko kuwa ya maana zaidi kuliko kazi, makuta, michezo, na mambo ingine ye kujifurahisha? Anatendeaka namna gani familia yake? Anahangaikiaka wengine?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine