Mungu Anasikiaka Sala Zako?
Wakati unasali, unakuwaka hakika kama Mungu anakusikiaka?
BIBLIA INASEMA NINI?
- Mungu anasikilizaka sala. Biblia inatuhakikishia kama “Yehova iko karibu na wale wote wenye kumuitia, wote wenye kumuitia katika ukweli. . . . Anasikia kilio chao cha kuomba musaada.”—Zaburi 145:18, 19. 
- Mungu anapenda usali kwake. Biblia inatutia moyo hivi: “Katika kila jambo kwa sala na sala ya kumulilia Mungu pamoja na kutoa shukrani, maombi yenu yajulishwe Mungu.”—Wafilipi 4:6. 
- Mungu anakuhangaikia kabisa. Mungu anajua muzuri mahangaiko yetu na magumu yetu, na anapenda kutusaidia. “Mumutupie mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawahangaikia ninyi.”—1 Petro 5:7.