Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp21 na. 3 uku. 9-11
  • Kuwa Mutu Muzuri Kutafanya Ukuwe na Maisha ya Muzuri Wakati Wenye Kuja?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuwa Mutu Muzuri Kutafanya Ukuwe na Maisha ya Muzuri Wakati Wenye Kuja?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • JAMBO YENYE WENGI WANAAMUA KUFANYA
  • MATOKEO NI NINI?
  • Namna Gani Tunaweza Kuwa na Maisha ya Muzuri Wakati Wenye Kuja?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Njia Yenye Kuongoza Kwenye Maisha ya Muzuri ya Wakati Wenye Kuja
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Utangulizi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Wapole Watariti Dunia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
wp21 na. 3 uku. 9-11
Mu bus, mwanamuke moja anaachia fasi yake mwanamuke fulani mwenye kuzeeka.

Kuwa Mutu Muzuri Kutafanya Ukuwe na Maisha ya Muzuri Wakati Wenye Kuja?

Kwa miaka mingi, watu wengi wanawaza kama kuwa mutu muzuri kutafanya wakuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja. Kwa mufano, watu wengi mu Asia wanakubaliana na hii maneno ya filozofe Confucius mwenye kujulikana sana: “Mambo yenye hauwezi penda wakufanyie na weye usiifanyie wengine.”a

JAMBO YENYE WENGI WANAAMUA KUFANYA

Watu wengi wanaendelea kuamini kama, ikiwa wanafanya mambo ya muzuri watakuwa na maisha ya muzuri wakati wenye kuja. Wanajikaza kuonyesha wengine heshima, kuwa na sifa za muzuri, wanatambua daraka yenye wako nayo mu maisha na wanaendelea kuwa na zamiri safi. Linh, mwanamuke moja mwenye kuishi mu Vietnam anasema hivi: “Niliwaza kila mara kama, ikiwa nasema kweli nitakuwa na maisha ya muzuri.”

Ule mwanamuke iko napatia chakula maskini na wenye hawana makao.

Juu ya imani yao, watu fulani wanajikaza kufanya mambo ya muzuri. Hsu-Yun, mwanaume moja mwenye kuishi Taiwan, anasema hivi: “Nilifundishwa kama ikiwa mutu alifanya mambo ya muzuri atakuwa na furaha kisha kufa, lakini kama alifanya mambo ya mubaya atateseka.”

MATOKEO NI NINI?

Ku mwisho wa ile siku, ule mwanamuke iko mwenye kuhuzunika na mwenye kuchoka, anabeba mutoto yake mwanaume.

Kusema kweli, wakati tunatendea wengine muzuri tunapata faida mingi. Lakini, wale wenye wanajikaza kutendea wengine muzuri, mara mingi wanafikiaka kuona kama hawatendewake muzuri sawa vile walitazamia. Shiu Ping mwanamuke moja mwenye kuishi Hong Kong, anasema hivi: “Nilijifunza kupitia mambo yenye nilijionea kama, wale wenye wanakuwaka nafanya mambo ya muzuri mara mingi hawabarikiwake. Nilifanya yangu yote ili kuhangaikia familia yangu na kufanya mambo ya muzuri. Lakini, ndoa yangu iliharibika na bwana yangu aliniacha miye na mutoto wangu mwanaume.”

Watu fulani wamefikia kuona kama, kila mara, dini haifanyake watu wakuwe wazuri. Etsuko, mwanamuke moja mwenye kuishi Japani, anasema hivi: “Nilijiunga na dini fulani na nilianza kuongoza vijana. Nilivunjika moyo sana, wakati niliona kama kulikuwa watu wenye walikuwa na matendo machafu, walipenda mashindano, na walitumia mubaya makuta ya kanisa.”

“Nilifanya yangu yote ili kuhangaikia familia yangu na kufanya mambo ya muzuri. Lakini ndoa yangu iliharibika na bwana yangu aliniacha miye na mutoto wangu mwanaume.”​—SHIU PING, HONG KONG

Watu fulani wenye wanajiingizaka sana mu mambo ya dini na wenye wanajikazaka sana kufanya mambo ya muzuri wamefikia kuvunjika moyo sana wakati mambo ya mubaya imewapata. Ile njo ilifikia Van, mwanamuke moja mwenye kuishi Vietnam. Anasema hivi: “Kila siku nilikuwa natoa matunda, maua, na chakula ku mazabahu kwa ajili ya wazazi wangu wenye walishakakufa na nilikuwa natazamia kama ningepata baraka mingi wakati wenye kuja. Hata kama nilifanya ile mambo yote ya muzuri na nilijikaza kuheshimia desturi za dini kwa miaka mingi, bwana yangu aligonjwa sana. Kisha mutoto yangu mwanamuke mwenye alikuwa na miaka 20 alikufa wakati alikuwa anasoma mu inchi ingine.”

JUU YA NINI HAITOSHE TU KUWA MUTU MUZURI

Ni jambo ya maana kuwa mutu muzuri, lakini ile haitoshe ili kuwa na maisha ya muzuri wakati wenye kuja. Juu ya nini? Fikiria mambo yenye Maandiko Matakatifu inatuambia.

HAIKO KILA MUTU NJO ANACHAGUAKA KUFANYA MAMBO YA MUZURI

“Mutenda-zambi mumoja tu anaweza kuharibu mambo mengi ya muzuri.”​—MUHUBIRI 9:18.

Hata kama unajikaza kuwa mutu muzuri, matendo ya mubaya ya wengine inaweza kufanya maisha yako ya wakati wenye kuja ikuwe na magumu. Kwa mufano, wakati ugonjwa fulani wa kuambukiza unatokea pengine unaweza kufuata shauri ya wenye mamlaka na kuepuka kukaribiana na wengine. Lakini tuseme nini kama watu fulani wanakatala kufanya vile? Kufanya vile kunaweza kutia mu hatari afya ya wale wenye kupenda kujilinda.

WATU WANAWEZA KUWA NA MAONI YENYE HAIFAE JUU YA MAMBO YENYE KUWA SAWA NA YENYE HAIKO SAWA

“Kuko njia yenye inaonekana kuwa sawa mbele ya macho ya mutu, lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.”​—MEZALI 14:12.

Watu wengi walifanya mambo yenye waliwaza kuwa ni ya muzuri lakini kisha, walifikia kutambua kama haikukuwa muzuri. Hata kama waliwaza kuwa walikuwa nafanya mambo ya muzuri wanaaendelea tu kuteseka juu ya maamuzi yao ya mubaya.

HAKUNA MWENYE ANAJUAKA MAISHA YA KESHO

“Hamujue maisha yenu yatakuwa namna gani kesho.”​—YAKOBO 4:14.

Hata mutu mwenye kuwa na roho ya muzuri anaweza kufa bila kutazamia. Kwa mufano, mu kipindi ya coronavirus watu wengi wenye walikuwa na roho ya muzuri walikufa juu walipenda kusaidia wengine. Ao pengine fikiria mufano wa Liting, mwanamuke moja mwenye kuishi Chine, mwenye alipoteza baba yake mu aksida ya gari. Anasema hivi: “Sikuelewa, mutu wa roho ya muzuri sawa yeye anakufa! Baba yangu alikuwa mufanyakazi muzuri, mutu wa kujishusha, na alikuwa anasema kweli. Mu ile gari ni yeye tu njo aliuawa.”

Kama haitoshe tu kuwa mutu muzuri juu tukuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja, sasa nini njo tuko nayo lazima? Ili kupata jibu ya hii ulizo tuko na lazima ya muongozo, ni kusema, habari ya kweli yenye inaweza kujibia maulizo yetu yenye inaweza kutusaidia tukuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja. Ni wapi tunaweza kupata ile muongozo?

a Ili kujua mambo mingi yenye Confucius alifundisha, ona sura ya 7, fungu ya 31-35, ya kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, yenye ilitolewa na Mashahidi wa Yehova na yenye kuwa ku www.jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine