Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w21 Mwezi wa 10 uku. 29-31
  • 1921—Kumepita Sasa Miaka Mia Moja

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 1921—Kumepita Sasa Miaka Mia Moja
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • WAHUBIRI WENYE UHODARI
  • IBADA YA FAMILIA NA YA KIPEKEE
  • KITABU YA MUPYA!
  • KULIKUWA KUNGALI KAZI
  • Kufanya Mambo Yenye Yehova Anaomba Kunaleta Baraka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • 1922—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Uriti Wenye Umepitishwa kwa Vizazi Saba
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • 1923—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
w21 Mwezi wa 10 uku. 29-31

1921—Kumepita Sasa Miaka Mia Moja

GAZETI Munara wa Mulinzi wa Tarehe 1 Mwezi wa 1, 1921 iliuliza hii ulizo wanafunzi wa Biblia: “Ni kazi gani tunaweza kutazamia hii mwaka?” Kisha ikaleta jibu kwa kutaja Isaya 61:1, 2, yenye iliwakumbusha kazi ya kuhubiri yenye walipewa. Inasema hivi: “Yehova alinitia mafuta ili nitangazie wapole habari njema . . . , kutangaza mwaka wa nia njema ya Yehova na siku ya kisasi ya Mungu wetu.”

WAHUBIRI WENYE UHODARI

Ili kutimiza kazi yao ya kuhubiri, wanafunzi wa Biblia walipaswa kuwa na sifa ya uhodari. Walipaswa pia kuwa na lazima ya kutangazia “habari njema” wapole, lakini pia kutangazia waovu “siku ya kisasi.”

Ndugu J. H. Hoskin, mwenye aliishi Kanada, alitoa ushahidi kwa uhodari ijapokuwa upinzani. Mu mwaka wa 1921, alikutana na pastere moja wa kanisa ya Metodiste. Ndugu Hoskin alianza mazungumuzo kwa kusema hivi: “Tunapaswa kuwa na mazungumuzo ya muzuri kuhusu Biblia, na hata kama hatukubaliane kuhusu mambo fulani, tunaweza kumalizia mazungumuzo yetu kwa amani na kuendelea kuwa marafiki.” Lakini mambo haikufanyika vile. Ndugu Hoskin anakumbuka hivi: “Kisha tu kuzungumuza na ule pastere kwa dakika kidogo, akapiga mulango nguvu sana na nikawaza kama kioo ya ile mulango itapasuka.”

Kisha ule pastere akatomboka kwa kusema hivi: “Juu ya nini hauende kuongea na wenye hawako Wakristo?” Ndugu Hoskin hakumujibia kitu, kisha akaondoka na wakati alikuwa mu njia akawaza hivi, ‘Niliwaza nilikuwa naongea na mwenye haiko Mukristo. Kumbe alikuwa Mukristo!’

Siku ya kufuata ule pastere alikuwa mu kanisa yake. Kisha akasema mambo ya mubaya kuhusu ndugu Hoskin. Ndugu Hoskin anakumbuka hivi: “Aliambia watu kama hakuna mutu muongo sawa miye mwenye alishakafika mu ile muji na kama nilipaswa kuuawa.” Lakini ile haikumufanya aache, aliendelea kuhubiri na kuzungumuza na watu wengi. Anasema hivi: “Nafurahiaka kuhubiri sana. Watu fulani walishangazwa na hata walisema hivi, ‘tunajua kama uko mutu wa Mungu!’ Na waliniuliza kama wanaweza kunisaidia ikiwa nilikosewa jambo fulani.”

IBADA YA FAMILIA NA YA KIPEKEE

Ili kusaidia watu waelewe Biblia muzuri zaidi, kila mara Wanafunzi wa Biblia walitoa maulizo fulani kuhusu Biblia na majibu mu gazeti L’Âge d’Or.a Kulikuwa maulizo fulani ya Biblia kwa ajili ya vijana na yenye wazazi wangezungumuza pamoja na watoto wao. Wazazi wangeuliza watoto wao maulizo na kuwasaidia kupata majibu mu Biblia. Maulizo kama vile, “Biblia iko na vitabu ngapi?” ilifundisha mambo ya musingi ya maana. Ulizo ingine kama vile, “Je, kila Mukristo wa kweli anapaswa kutazamia mateso?” ilitayarisha vijana ili wakuwe wahubiri wenye uhodari.

Kulikuwa pia maulizo fulani ya Biblia na majibu kwa ajili ya wenye tayari walikuwa wanajua mambo mingi kuhusu Biblia. Majibu fulani ingeweza kupatikana mu buku ya kwanza ya kitabu Études des Écritures. Wasomaji wengi walijfunza mambo mingi kupitia ile maulizo. Lakini kisha pale, L’Âge d’Or ya tarehe 1 Mwezi wa 12, 1921, ilitangaza kama ile maulizo haingetolewa tena. Juu ya nini kulikuwa ile mabadiliko yenye haikutazamiwa?

KITABU YA MUPYA!

Kitabu La Harpe de Dieu

Karte yenye kuwa na mugao wa kusoma

Karte yenye kuwa na maulizo

Wale wenye walikuwa wanaongoza waliona kama wanafunzi wapya wa Biblia walipaswa kujifunza kweli za musingi mu njia yenye kupangwa muzuri zaidi. Juu ya kufikia ile kusudi, kitabu La Harpe de Dieu ilitolewa mu Mwezi wa 11, 1921. Wale wenye walikubali ile kitabu waliandikishwa ku masomo fulani. Ile masomo ya kipekee ilisaidia wasomaji “kutambua kusudi ya Mungu ya kupatia wanadamu uzima wa milele.” Ile masomo ilikuwa inafanywa namna gani?

Wakati mutu alikubali ile kitabu, walikuwa wanamupatia karte fulani ya kidogo yenye ilimuambia ni ukurasa gani alipaswa kusoma mu ile kitabu. Juma yenye ilifuata, alipata karte ingine yenye ilikuwa na maulizo mingi kuhusu mambo yenye alikuwa amesoma. Ku mwisho ya ile karte kulikuwa pia mugao wa kusoma kwa ajili ya juma yenye ilifuata.

Kila juma na kwa muda wa majuma 12, mwanafunzi alipata karte ya mupya kutoka kwa kutaniko. Mara mingi, ni wale wenye walikuwa wazee-wazee mu kutaniko ao wale wenye hawangeweza kuenda kuhubiri nyumba kwa nyumba njo walikuwa wanatuma zile karte. Kwa mufano, Anna K. Gardner, wa Millvale, mu Pennsylvanie, Inchi ya Amerika, alisema hivi: “Wakati kitabu La Harpe de Dieu ilitolewa, ilipatia dada yangu mwenye alikuwa na magumu ya kutembea, mwenye aliitwa Thayle, kazi mingi yenye angeweza kufanya, ni kusema, kutuma kila juma karte za maulizo.” Wakati mutu alimaliza ile masomo, mutu fulani wa mu kutaniko alimutembelea ili kumusaidia ajifunze mambo mingi zaidi juu ya Biblia.

Thayle Gardner akiwa mu kiti yake ya vilema

KULIKUWA KUNGALI KAZI

Ku mwisho wa mwaka, Ndugu Joseph Rutherford alitumia makutaniko yote barua. Na alionyesha kama “ushahidi wenye ulitolewa hii mwaka kuhusu Ufalme ulifikia kusaidia watu wengi zaidi kuliko miaka yenye ilipita.” Kisha aliongezea hivi: “Kungali kazi mingi ya kufanya. Muendelee kutia wengine moyo ili wajiunge mu hii utumishi yenye imebarikiwa.” Wanafunzi wa Biblia walifuata kabisa mambo yenye alisema. Mu mwaka wa 1922 wahubiri, walihubiri kwa uhodari kuhusu Ufalme mu njia ya kushangaza sana.

Marafiki Wenye Uhodari

Wanafunzi wa Biblia walionyeshana upendo kati yao kwa kusaidiana. Walikuwa marafiki wenye uhodari wenye ‘walizaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.’ Habari yenye kufuata inaonyesha vile.​—Mez. 17:17.

Siku ya Pili, tarehe 31 Mwezi wa 5, 1921 mu muji wa Tulsa kule Oklahoma mu Inchi ya Amerika, kulitokea ile yenye ilifikia kuitwa mauaji ya Tulsa. Mwanaume moja mweusi alifungwa na alishitakiwa kama aliua mwanamuke moja muzungu. Wakati kikundi ya zaidi ya wanaume 1 000 wenye walikuwa wazungu walipigana na kikundi ingine kidogo ya wanaume weusi, ile ugomvi ilitawanyika haraka mupaka ikafika mu eneo kwenye kulikuwa kunaishi weusi wengi. Ile eneo iliitwa Greenwood. Ile ugomvi ilifanya nyumba zaidi ya 1 400 na pia fasi zingine za biashara zilunguzwe na pia vitu fulani viibwe. Wakubwa wa serikali walisema kama watu wenye walikufa walikuwa watu 36, lakini inawezekana mamia ya watu njo walikufa.

Ndugu Richard J. Hill, mwanafunzi wa Biblia mwenye alikuwa mweusi na mwenye alikuwa anaishi Greenwood alieleza vile mambo ilikuwa: “Ilikuwa usiku, tulikuwa tuko tunafanya funzo yetu ya Biblia kama kawaida na njo wakati ile mapigano ilianza. Wakati tulimaliza funzo tulikuwa tunasikia makelele ya masasi. Na hata wakati tulienda kulala tuliendelea kusikia ile makelele. Siku ya Tatu asubui, tarehe 1 Mwezi wa 6, hali iliendelea kuwa mubaya tena zaidi. Ndugu Richard anasema tena hivi: “Watu fulani walikuja na walituambia kama, ikiwa tungependa kulindwa, tulipaswa kuenda ku majengo fulani ya serikali yenye ilikuwa mu muji.” Kwa hiyo, ndugu Hill pamoja na bibi yake na watoto wao tano walienda ku ile majengo. Inasemekana kama wanaume na wanamuke weusi 3 000 hivi walikuwa mu ile majengo na kisha walikuwa wanalindwa na jeshi ya serikali yenye iliitwa ili kurudisha utaratibu.

Wakati ileile, ndugu Arthur Claus, mwenye alikuwa muzungu, alikamata kwa uhodari uamuzi fulani, anasema hivi: “Wakati nilisikia kama kulikuwa ugomvi mu Greenwood, na kama watu waliiba vitu fulani mu manyumba na vingine vililunguzwa, niliamua kuenda kumuona rafiki yangu Ndugu Hill ili kujua habari yake.”

Ndugu Arthur Claus alisaidia watoto 14 wajifunze mingi zaidi kuhusu Biblia kwa kutumia kitabu La Harpe de Dieu

Wakati nilifika ku nyumba ya Ndugu Hill nilikuta jirani yake moja muzungu mwenye alikuwa na bunduki ku mukono. Ule jirani alikuwa pia rafiki ya Ndugu Hill na aliwaza kama nilikuwa kati ya watu wenye walikuwa wanaleta fujo. Akanilalamikia hivi: “Unakuya kufanya nini hapa?”

Arthur anasema tena hivi: “Kama singemupatia tu jibu ya muzuri kabisa angenipiga masasi. Nikamuhakikishia kama na miye nilikuwa rafiki ya Ndugu Hill na nilikuwa nakuya sana kumuangalia.” Arthur na ule jirani walilinda nyumba ya Hill juu isiharibishwe na wale watu wenye walikuwa wanaleta fujo.

Bila kukawia, Arthur alipata habari kama Ndugu Hill na familia yake walikuwa ku ile majengo ya serikali. Kisha Arthur akapata habari kama watu weusi hawangeweza kutoka mu ile majengo bila ruhusa ya Jenerali Barrett, mwenye alikuwa anasimamia ile makao. Arthur anaeleza hivi: “Ilikuwa nguvu sana kufikia kuzungumuza na ule Jenerali. Lakini wakati nilimuambia mambo yenye nilipenda kufanya aliniuliza hivi: ‘Utaweza kulinda ile familia na kuwatimizia mahitaji yao?’ Nikamuambia kwa furaha ndiyo.”

Kisha Arthur kupata ruhusu akaenda mara moja ku ile makao. Akaonyesha ule askari mwenye alikuwa pale dokima ya ruhusa yenye alipata. Ule askari akasema hivi: “Ah! Hii iko na sinyatire ya Jenerali mwenyewe! Unajua kama weye njo mutu wa kwanza leo mwenye atatosha mutu fulani mwenye kuwa ndani?” Kisha Arthur na ule askari wakaenda kumutafuta Ndugu Hill na familia yake. Wote wakatoka na wakaingia mu gari ya Arthur na kurudia ku nyumba.

“Hakuna mwenye alijiona kuwa wa maana sana kuliko wengine kati ya watu wa Mungu”

Ndugu Claus alihakikisha kama Ndugu Hill na familia yake walikuwa salama. Mufano wake muzuri wa uhodari ulikuwa na matokeo ya muzuri sana. Arthur anasema hivi: “Ule jirani mwenye alitusaidiaka kuchunga nyumba ya Ndugu Hill alipendezwa tena zaidi na kweli. Na watu fulani pia walipendezwa na ujumbe wa Ufalme sababu waliona kama watu wa Mungu hawakuacha mambo ya rangi ya ngozi iwagawanye na hakuna mwenye alijiona kuwa wa maana sana kuliko wengine kati ya watu wa Mungu.”

a L’Âge d’Or ilibadilishwa na kuitwa Consolation mu 1937 na kisha ikaitwa Amuka! mu 1946.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine