Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w22 Mwezi wa 10 uku. 18-23
  • Hekima ya Kweli Inaita Kwa Sauti Kubwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Hekima ya Kweli Inaita Kwa Sauti Kubwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • KUMUJUA YEHOVA KUNATUSAIDIA TUKUWE NA HEKIMA
  • JUU YA NINI WATU WANAKATALA HEKIMA YA KWELI?
  • HEKIMA YA KWELI INATULETEA FAIDA
  • Faida ya Kuendelea Kumuogopa Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
w22 Mwezi wa 10 uku. 18-23

HABARI YA KUJIFUNZA YA 43

Hekima ya Kweli Inaita Kwa Sauti Kubwa

“Hekima ya kweli inaita kwa sauti kubwa katika barabara. Inaendelea kupandisha sauti yake katika viwanja vya watu wote.”​—MEZ. 1:20.

WIMBO 88 Unijulishe Njia Zako

KIFUPI YA HABARIa

1. Watu wengi wanatenda namna gani kuhusu mashauri yenye hekima ya Biblia? (Mezali 1:20, 21)

MU INCHI za mingi, mara mingi tunaonaka ndugu na dada wamesimama fasi kwenye watu wengi wanapita. Wanaonyesha sura ya kicheko na kutolea watu vichapo vya kusoma. Na weye ulishakafanya vile? Kama ni vile, pengine ile imekufanya ufikirie maneno ya mufano yenye kupatikana mu kitabu ya Mezali, yenye kuzungumuzia hekima yenye inaita kwa sauti kubwa mu viwanja vya watu wote ili watu wasikilize mashauri yake. (Soma Mezali 1:20, 21.) Biblia na vichapo vyetu viko na “hekima ya kweli,” ni kusema, hekima ya Yehova. Njo hekima yenye watu wako nayo lazima kabisa juu waweze kupata uzima wa milele. Tunafurahiaka sana wakati mutu anakubali vichapo vyetu. Lakini, haiko kila mutu njo anaitikaka vichapo vyetu. Wamoja hawapendi kujua mambo yenye Biblia inasema, na wengine wanatucheka. Wanawaza kama Biblia ni kitabu ya zamani sana. Na wengine wanachambua-chambua mambo yenye Biblia inasema kuhusu mwenendo, na wanasema kama wenye kuifuata ni wakali na wanajiona kuwa wenye haki. Lakini, Yehova anaendelea kupatia watu wote hekima ya kweli. Namna gani?

2. Ni wapi njo tunaweza kupata hekima ya kweli leo? Lakini, watu wengi wanaamua kufanya nini?

2 Njia moya yenye Yehova anatumia juu watu wapate hekima ya kweli ni Neno yake, Biblia. Karibu kila mutu anaweza kupata Biblia. Tuseme nini kuhusu vichapo vyetu vyenye vinategemea Biblia? Kwa musaada wa Yehova, vinapatikana mu luga zaidi ya 1 000. Wale wenye wanasikiliza, ni kusema, wale wenye wanasoma na kutumikisha mambo yenye wanajifunza, watapata faida. Lakini, watu wengi wanakatala kusikiliza sauti ya hekima ya kweli. Wakati wanataka kukamata maamuzi, wanajitegemea wao wenyewe ao wanasikiliza mawazo ya wanadamu wenzao. Wanaweza hata kutuzarau juu tunachagua kufuata mambo yenye Biblia inasema. Hii habari itaonyesha juu ya nini watu wanatendaka vile. Tuone kwanza namna tunaweza kupata hekima ya Yehova.

KUMUJUA YEHOVA KUNATUSAIDIA TUKUWE NA HEKIMA

3. Hekima ya kweli inamaanisha nini?

3 Hekima inaweza kumaanisha uwezo wa kutumia mambo yenye tunajua ili kukamata maamuzi ya muzuri. Lakini, hekima ya kweli inamaanisha mambo mingi zaidi. Biblia inasema hivi: “Kumuogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima, na kumujua Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi ni uelewaji.” (Mez. 9:10) Kwa hiyo, wakati tunataka kukamata maamuzi ya maana, tunapaswa kufikiria kwanza mawazo ya Yehova, ni kusema, kujiuliza kama maamuzi yetu itaonyesha kuwa ‘tunamujua Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi.’ Tunaweza kufanya vile kwa kujifunza Biblia na vichapo vyetu vyenye vinategemea Biblia. Wakati tunafanya vile, tunaonyesha kama tuko na hekima ya kweli.​—Mez. 2:5-7.

4. Juu ya nini tunaweza kusema kama hekima ya kweli inatoka tu kwa Yehova?

4 Ni Yehova tu njo anaweza kutupatia hekima ya kweli. (Ro. 16:27) Juu ya nini tunaweza kusema kama hekima ya kweli inatoka tu kwake? Kwanza, juu Yehova njo Muumbaji, anajua na kuelewa muzuri sana vitu vyote vyenye aliumba. (Zb. 104:24) Pili, vitu vyote vyenye Yehova aliumba vinaonyesha kama iko na hekima. (Ro. 11:33) Tatu, mashauri yenye hekima ya Yehova sikuzote inaleteaka faida wale wenye wanaitumikisha. (Mez. 2:10-12) Kama tunapenda kupata hekima ya kweli, tunapaswa kukubali zile sababu tatu na kuziacha zituongoze wakati tunatafuta kukamata maamuzi na wakati tunatafuta kufanya jambo fulani.

5. Matokeo imekuwa nini juu watu wamekatala kukubali kama hekima ya kweli inatoka tu kwa Yehova?

5 Watu wengi wenye tunakutana nao mu mahubiri wanakubali kama vitu vyenye kuwa mu ulimwengu ni vya ajabu sana. Lakini, hawakubali kama kuko Muumbaji na wanasema kama vile vitu vilijitokeza. Wengine wenye tunakutana nao wanaamini kama kuko Mungu, lakini wanaona kanuni za Biblia kuwa za zamani sana, na wanachagua kufanya mambo yenye wanapenda. Matokeo imekuwa nini? Dunia imekuwa fasi ya muzuri zaidi juu watu wanategemea hekima yao wenyewe kuliko kutegemea hekima ya Mungu? Wako na furaha ya kweli? Wako na tumaini? Mambo yenye tuko najionea inaonyesha kama hii mawazo ni ya kweli: “Hakuna hekima, wala utambuzi wowote, wala shauri katika kumupinga Yehova.” (Mez. 21:30) Ile inatuchochea tuendelee kumuomba Yehova atupatie hekima ya kweli. Jambo ya kuhuzunisha, watu wengi hawafanye vile. Juu ya nini?

JUU YA NINI WATU WANAKATALA HEKIMA YA KWELI?

6. Taya vikundi vya watu wenye wanakatalaka kusikiliza hekima ya kweli kulingana na Mezali 1:22-25.

6 Watu wengi wanakatala kusikiliza wakati hekima ya kweli “inaita kwa sauti kubwa katika barabara.” Kulingana na Biblia, kuko vikundi tatu vya watu wenye wanakatala hekima. Kuko “wenye kukosa uzoefu,” “wazihaki,” na “wapumbavu.” (Soma Mezali 1:22-25.) Tuone juu ya nini wale watu wanakatalaka hekima ya Mungu, na pia namna tunaweza kuepuka kutenda kama wao.

7. Juu ya nini watu fulani wanachagua kuendelea kuwa “wenye kukosa uzoefu?”

7 “Wenye kukosa uzoefu” ni wale wenye wanaamini mambo yote yenye wanasikia, na ni mwepesi kuwashawishi, ao kuwadanganya. (Mez. 14:15, maelezo ya chini) Mara mingi tunakutanaka na watu wa vile mu mahubiri. Kwa mufano, fikiria mamilioni ya wale wenye wamedanganywa na viongozi wa dini ao wa politike. Wamoja wanajisikia mubaya sana wakati wanatambua kama wale viongozi waliwadanganya. Lakini, wale wenye kuzungumuziwa mu Mezali 1:22 wanachagua kuendelea kukosa uzoefu juu wanapenda kubakia vile. (Yer. 5:31) Wanafurahia kufanya mambo yenye wanapenda na hawapendi kujifunza mambo yenye Biblia inasema ao kutii sheria zake. Wengi wako na mawazo sawa ile ya mwanamuke fulani mu muji wa Quebec, Kanada, mwenye kupenda sana mambo ya dini, mwenye aliambiaka hivi Shahidi wa Yehova: “Kama Padri wetu alishatudanganya, ni kosa yake, haiko kosa yetu!” Bila shaka, hatupendi kuwa kama wale wenye wanakatala kimakusudi kusikiliza hekima ya Yehova.​—Mez. 1:32; 27:12.

8. Nini njo itatusaidia tukuwe na uzoefu wenye kufaa?

8 Biblia iko na sababu ya muzuri ya kututia moyo tusiendelee kuwa sawa vile wale wenye hawana uzoefu, lakini, ‘tukuwe watu wazima katika uelewaji wetu.’ (1 Ko. 14:20) Tunapataka uzoefu wenye kufaa kwa kutumikisha kanuni za Biblia mu maisha yetu. Wakati tunafanya vile, tunaona namna Biblia inatusaidia kuepuka magumu, na kukamata maamuzi yenye hekima. Ni muzuri tukuwe najichunguza kuhusu ile jambo. Kama tumejifunza Biblia, na tumehuzuria mikutano kwa wakati fulani, ni muzuri tujiulize juu ya nini hatuyakamata uamuzi wa kujitoa kwa Yehova na kubatizwa. Kama tulishabatizwa, tuko najikaza ili kuwa wahubiri na walimu wazuri zaidi wa habari njema? Maamuzi yetu inaonyesha kama tunaongozwa na kanuni za Biblia? Tuko natendea wengine sawa vile Yesu angewatendea? Kama inaomba tufanye mabadiliko, tunapaswa kufikiri sana kuhusu vikumbusho vya Yehova vyenye ‘vinafanya mwenye hana uzoefu akuwe na hekima.’​—Zb. 19:7.

9. “Wazihaki” wanaonyesha namna gani kama wanakatala hekima ya Mungu?

9 Kikundi ya pili ya watu wenye wanakatala hekima ya Mungu ni ya “wazihaki.” Wakati fulani, tunakutanaka na watu wa vile mu mahubiri. Wanapendaka kuchekelea wengine. (Zb. 123:4) Biblia ilisemaka kama mu siku za mwisho kungekuwa wazihaki wengi. (2 Pe. 3:3, 4) Kama vile wana-wakwe wa loti mwenye haki, leo watu fulani hawapendi kusikiliza maonyo yenye Mungu anatutolea. (Mwa. 19:14) Wengi wanachekelea wale wenye wanaishi kulingana na kanuni za Biblia. Wanafanya vile juu wanapenda kufuata “tamaa zao” ili kufanya “mambo ya kukosa kumuogopa Mungu.” (Yud. 7, 17, 18) Maelezo yenye Biblia inatoa juu ya wazihaki inapatana kabisa na tabia ya waasi-imani na wengine wenye wamemukatala Yehova!

10. Kama vile Zaburi 1:1, tunaweza kufanya nini juu tusifikie kuwa wazihaki?

10 Tunaweza kufanya nini juu tusifikie kuwa wazihaki? Tunapaswa kuepuka wale wenye kuwa na tabia ya kunungunika-nungunika kuhusu kila jambo. (Soma Zaburi 1:1.) Ile inamaanisha kama hatupaswe kusikiliza, ao kusoma mambo ya waasi-imani. Tunapaswa kuwa waangalifu ili tusianze kuwa na tabia ya kunungunika-nungunika kuhusu kila jambo na kuanza kuwa na mashaka juu ya namna ya Yehova ya kufanya mambo na juu ya maagizo yenye tengenezo yake inatupatia. Juu tuepuke ile tabia, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Nakuwaka kila mara mutu wa kunungunika-nungunika wakati tunapewa maagizo ao mafasirio fulani ya mupya? Nakuwaka mutu wa kuona tu makosa ya wale wenye wanatuongoza?’ Kama tunaacha haraka kufanya vile, tutamufurahisha Yehova.​—Mez. 3:34, 35.

11. “Wapumbavu” wanaona namna gani kanuni za Yehova za mwenendo?

11 Kikundi ya tatu ya watu wenye wanakatala hekima ni ya “wapumbavu.” Ni wapumbavu juu wanakatala kuishi kulingana na sheria za Mungu za mwenendo. Wanafanya mambo yenye wanaona kuwa sawa. (Mez. 12:15) Wapumbavu wanamukatala Yehova, Chanzo ya hekima. (Zb. 53:1) Wakati tunakutanaka nao mu mahubiri, mara mingi wanatuchambua-chambua juu tunatii kanuni za Biblia. Lakini, hawawezi kutusaidia mu maisha. Biblia inasema hivi: “Mupumbavu hawezi kupata hekima ya kweli; hana jambo la kusema katika mulango mukubwa wa muji.” (Mez. 24:7) Wapumbavu hawana mashauri yenye hekima yenye wanaweza kutupatia. Njo maana, Yehova anatuambia ‘tukae mbali na mutu mupumbavu’!​—Mez. 14:7.

12. Nini njo itatusaidia tusitende sawa vile wapumbavu?

12 Hatuko sawa vile wale wenye wanachukia mashauri ya Mungu. Lakini, tunajifunza kupenda mawazo ya Mungu, kutia ndani sheria zake. Jambo yenye itatusaidia tupende kabisa mawazo ya Mungu ni kufikiria matokeo ya kumutii Mungu na matokeo ya kutomutii. Fikiria magumu yenye watu wanajiletea juu ya kukatala kwa upumbavu mashauri yenye hekima ya Yehova. Kisha, ufikirie namna maisha yako imekuwa muzuri zaidi juu ya kumutii Mungu.​—Zb. 32:8, 10.

13. Yehova anatulazimisha kutii mashauri yake yenye hekima?

13 Yehova anatolea watu wote hekima yake. Lakini, halazimishe mutu yeyote kuikubali. Jambo yenye anafanya ni kutuonyesha mambo yenye itapata wale wenye wanakatala kusikiliza hekima yake. (Mez. 1:29-32) Wale wenye wanakatala kumutii Yehova, bipande bishuke “watapata matokeo ya njia yao.” Watapata magumu na mateso juu ya matendo yao, na ku mwisho Yehova atawaharibu. Kwa upande mwingine, Mungu anaahidi hivi wale wenye wanasikiliza mashauri yake yenye hekima na kuitumikisha: “Ule mwenye kunisikiliza ataishi kwa usalama na hatasumbuliwa na woga wa musiba.”​—Mez. 1:33.

HEKIMA YA KWELI INATULETEA FAIDA

Ndugu fulani anatoa maelezo ku mukutano.

Kutoa maelezo ku mikutano kunatusaidia tukuwe nguvu kiroho (Ona fungu ya 15)

14-15. Mezali 4:23 inatufundisha nini?

14 Tunapataka tu faida wakati tunatumikisha hekima ya Mungu. Sawa vile tumeona, Yehova anafanya ikuwe mwepesi kwa watu kupata mashauri yake yenye hekima. Kwa mufano, mu kitabu ya Mezali, Yehova anatupatia mashauri yenye itatusaidia sikuzote tukuwe na maisha ya muzuri ikiwa tunaitumikisha. Tuzungumuzie mashauri ine tu yenye hekima.

15 Ulinde moyo wako wa mufano. Biblia inasema hivi: “Linda moyo wako kuliko vitu vyote vyenye unalinda, kwa maana ni mule munatoka chemchemi za uzima.” (Mez. 4:23) Fikiria mambo yenye tunapaswa kufanya juu ya kulinda moyo wetu halisi. Tunapaswa kula chakula ya muzuri, kufanya mazoezi, na kuepuka tabia za mubaya. Tunapaswa kufanya jambo fulani ya vile ili kulinda moyo wetu wa mufano. Kila siku tunapaswa kulisha moyo wetu Neno ya Mungu. Tunapaswa kutayarisha, kuhuzuria, na kutoa maelezo ku mikutano ya Kikristo. Tunapaswa kuzoeza moyo wetu kwa kuhubiri kwa ukawaida. Na juu tusifikie kuwa na tabia za mubaya, tunapaswa kuepuka jambo yoyote yenye inaweza kuchafua akili yetu, sawa vile mambo ya kujifurahisha yenye kuonyesha uasherati na pia marafiki wabaya.

Watu wa familia fulani ni wenye furaha na wako inje ya nyumba yao ya kidogo. Mama anatia ku moto chakula ya mwepesi. Pembeni yake, baba anatumia kitabu “Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia” juu ya kujifunza na watoto wao.

Kuwa na mawazo yenye kusawazika juu ya makuta kunatusaidia tutosheke na mambo yenye tuko nayo (Ona fungu ya 16)

16. Juu ya nini maneno ya Mezali 23:4, 5 inaweza kutusaidia sana leo?

16 Utosheke na mambo yenye uko nayo. Biblia inatoa hii shauri: “Usijichokeshe ili kupata utajiri. . . . Wakati unautupia jicho, hauko pale, kwa maana hakika utaota mabawa kama tai na kuruka mbali katika anga.” (Mez. 23:4, 5) Mali inaishaka. Lakini, leo matajiri na maskini wanatafuta sana makuta. Na ile inafanya mara mingi wajiendeshe mu njia yenye itaharibisha sifa yao, uhusiano wao na wengine, na hata afya yao. (Mez. 28:20; 1 Ti. 6:9, 10) Kwa upande mwingine, hekima inatusaidia tukuwe na usawaziko kuhusu makuta. Na ile inatusaidia tusikuwe na pupa, lakini tutosheke na kufurahia mambo yenye tuko nayo.​—Muh. 7:12.

Dada iko napiga porojo mbele ya dada wengine wa mu kutaniko yake. Dada wawili wanasikiliza kwa uangalifu wakati mwingine iko nafikiri juu ya mambo yenye iko nasikia.

Kufikiri mbele ya kusema kunatusaidia tusiumize wengine kupitia maneno yetu (Ona fungu ya 17)

17. Tunaweza kufanya nini juu tukuwe na “ulimi wa mwenye hekima” wenye kuzungumuziwa mu Mezali 12:18?

17 Ufikiri mbele ya kusema. Kama hatuko waangalifu, tunaweza kuumiza wengine sana kupitia maneno yetu. Biblia inasema hivi: “Maneno yenye kusemwa bila kufikiri yanatoboa kama upanga, lakini ulimi wa mwenye hekima unaponyesha.” (Mez. 12:18) Tunalinda uhusiano muzuri na wengine wakati tunaepuka kupiga porojo kuhusu makosa ya wengine. (Mez. 20:19) Juu maneno yetu iponyeshe kuliko kuumiza, tunapaswa kujaza mu moyo wetu ujuzi wa Neno ya Mungu. (Lu. 6:45) Kama tunafikiri sana juu ya mambo yenye Biblia inasema, maneno yetu itakuwa sawa vile “chemchemi ya hekima” yenye inatia moyo wengine.​—Mez. 18:4.

Dada fulani iko anaandika mawazo fulani wakati iko naangalia video kuhusu namna ya kuanzisha mazungumuzo ya mukutano wa katikati ya juma. Pembeni ya buku yake ya kuandikia kuko trakti fulani na telefone yenye kuwa na JW Library yenye kufunguliwa.

Kufuata maagizo ya tengenezo kunatusaidia tupate matokeo ya muzuri mu kazi yetu ya kuhubiri (Ona fungu ya 18)

18. Namna gani kutumikisha shauri yenye kupatikana mu Mezali 24:6 kunatusaidia tupate matokeo ya muzuri mu kazi ya kuhubiri?

18 Ufuate maagizo ya tengenezo. Biblia inatupatia hii shauri ya maana: “Utapigana vita yako kwa muongozo wenye hekima, na kupitia washauri wengi kuko ushindi.” (Mez. 24:6, maelezo ya chini) Fikiria namna kutumikisha ile shauri kunatusaidia tupate matokeo ya muzuri mu kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha. Kuliko kuhubiri na kufundisha namna tunapenda, tunajikazaka kufuata maagizo yenye tunapewa. Tunapata muongozo wenye hekima ku mikutano yetu ya Kikristo. Kule washauri wenye uzoefu wanatoa hotuba, vipindi, na maonyesho yenye kutegemea Biblia ili kutuzoeza. Tena, tengenezo ya Yehova inatutolea vyombo vyenye kufaa, ni kusema, vichapo na video vyenye vinaweza kusaidia watu waelewe Biblia. Uko najifunza namna ya kutumia muzuri vile vyombo?

19. Unaona namna gani hekima yenye Yehova anatutolea? (Mezali 3:13-18)

19 Soma Mezali 3:13-18. Tuko wenye shukrani sana juu ya mashauri yenye hekima yenye inapatikana mu Neno ya Mungu! Maisha yetu ingekuwa namna gani bila ile mashauri? Mu hii habari, tumejikumbusha mashauri fulani yenye hekima yenye inapatikana mu kitabu ya Mezali. Kwa kweli, Yehova ametutolea mashauri yenye hekima mu Biblia yote. Tuazimie basi kutumikisha hekima ya Yehova mu kila sehemu ya maisha yetu. Watu wengi hawasamini hekima ya Mungu. Lakini siye tuko hakika kama “wale wenye kuishika sana [hekima] wataitwa wenye furaha.”

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Tunapata namna gani hekima ya kweli?

  • Juu ya nini wengi wanakatala kusikiliza hekima ya kweli, na matokeo inakuwa nini?

  • Ni shauri gani ya kitabu ya Mezali yenye unaona kama inaweza kutusaidia sana?

WIMBO 36 Tulinde Moyo Wetu

a Hekima yenye Yehova anatutolea ni ya muzuri zaidi kuliko hekima yenye ulimwengu unaweza kututolea. Mu hii habari, tutazungumuzia maneno ya mufano yenye kupendeza yenye inapatikana mu kitabu ya Mezali. Ile maneno inazungumuzia hekima yenye inaita kwa sauti kubwa mu kiwanja ya watu wote ya muji. Tutazungumuzia namna tunaweza kupata hekima ya kweli, juu ya nini watu fulani hawapendi kusikiliza hekima ya Yehova na faida yenye tutapata kama tunasikiliza hekima ya Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine