Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w23 Mwezi wa 2 uku. 8-13
  • Mambo ya Kufanya juu Ufaidike na Usomaji Wako wa Biblia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo ya Kufanya juu Ufaidike na Usomaji Wako wa Biblia
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • SOMA JUU UELEWE
  • SOMA JUU UPATE MALI YA KIROHO
  • SOMA ILI UBADILIKE
  • KUSOMA NENO YA MUNGU KUNAFURAHISHA
  • “Mukuwe Watendaji wa Neno”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Unaweza Kufanya Nini Juu Upate Faida Wakati Uko Nasoma Biblia
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • ‘Neno la Mungu . . . Liko na Nguvu’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Namna ya Kufaidika Kabisa na Usomaji wa Biblia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
w23 Mwezi wa 2 uku. 8-13

HABARI YA KUJIFUNZA YA 7

Mambo ya Kufanya juu Ufaidike na Usomaji Wako wa Biblia

“Wewe unasoma namna gani?”​—LU. 10:26.

WIMBO 97 Uzima Wetu Unategemea Neno ya Mungu

KIFUPI YA HABARIa

1. Ni nini inaonyesha kama Yesu alipenda sana Maandiko?

WAZIA namna watu walikuwa najisikia wakati Yesu alikuwa nafundisha. Mara mingi alikuwa anataya Maandiko yenye alikuwa alishaweka mu akili. Kusema kweli, Yesu alitosha mu Maandiko maneno ya kwanza yenye alisema kisha kubatizwa na maneno fulani ya mwisho yenye alisema mbele akufe.b (Kum. 8:3; Zb. 31:5; Lu. 4:4; 23:46) Na mu miaka tatu na nusu ya utumishi wake hapa ku dunia, kisha kubatizwa, na mbele akufe, mara mingi Yesu alikuwa nasoma Maandiko mbele ya watu, alikuwa anaitaya na kuifasiria.​—Mt. 5:17, 18, 21, 22, 27, 28; Lu. 4:16-20.

Picha: Yesu angali mutoto, iko nasikiliza wakati wazazi wake wako naongea naye. 2. Sasa anakuwa kijana, yeye pamoya na familia yake wako nasikiliza kwa uangalifu wakati Maandiko iko nasomwa ku sinagogi. 3. Sasa Yesu anakomala, iko nasoma kitabu ya kukunjwa.

Yesu alionyesha mu maisha yake yote kama alipenda Maandiko na aliacha iongoze matendo yake (Ona fungu ya 2)

2. Wakati Yesu alikuwa anakomala, nini njo ilimusaidia ajue muzuri Maandiko? (Ona picha ku jalada.)

2 Miaka fulani mbele aanze utumishi wake, Yesu alisoma na kusikiliza Neno ya Mungu tena na tena. Bila shaka, wakati Yesu alikuwa ku nyumba, pamoya na wazazi wake Maria na Yosefu, alikuwa nasikia wanataya Maandiko mu mazungumuzo yao ya familia ya kila siku.c (Kum. 6:6, 7) Tunaweza kuwa hakika kama Yesu alikuwa naenda ku sinagogi kila Sabato pamoya na familia yake (Lu. 4:16) Kule, alikuwa nasikiliza kwa uangalifu wakati watu walikuwa nasoma Maandiko. Ku mwisho, alianza kujisomea ile Maandiko Matakatifu. Ile ilimusaidia ajue muzuri Maandiko, aipende na aache iongoze matendo yake. Kwa mufano, kumbuka jambo yenye ilitokea ku hekalu wakati Yesu alikuwa tu na miaka 12. Walimu wenye walikuwa kule, wenye walijua muzuri sana Sheria ya Musa ‘walishangazwa na uwezo wake [Yesu] wa kuelewa na majibu yake.’​—Lu. 2:46, 47, 52.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Na siye tunaweza kufikia kujua na kupenda Neno ya Mungu kama tuko naisoma kwa ukawaida. Lakini, tunapaswa kufanya nini ili tufaidike na usomaji wetu wa Biblia? Mambo yenye Yesu aliambia wale wenye walijua muzuri Sheria, kutia ndani waandishi, Wafarisayo na Wasadukayo inaweza kutufundisha mambo fulani. Mara mingi wale viongozi wa dini walikuwa nasoma maandiko. Lakini, hawakufaidika na mambo yenye walikuwa nasoma. Yesu alizungumuzia mambo tatu yenye wale wanaume walipaswa kufanya juu wafaidike na usomaji wao wa Biblia. Maneno yenye aliwaambia itatusaidia tujue muzuri zaidi namna ya (1) kuelewa mambo yenye tuko nasoma, (2) kupata mali ya kiroho, na (3) kuacha Neno ya Mungu itubadilishe.

SOMA JUU UELEWE

4. Kulingana na Luka 10:25-29, kusudi yetu inapaswa kuwa nini wakati tuko nasoma Biblia?

4 Tunapenda kuelewa maana ya mambo yenye tunasoma mu Neno ya Mungu. Kama hatufanye vile, pengine usomaji wetu wa Biblia hautatuletea faida kabisa. Kwa mufano, fikiria mazungumuzo ya Yesu pamoya na “mutu fulani mwenye kujua sana Sheria.” (Soma Luka 10:25-29.) Wakati ule mwanaume alimuuliza mambo yenye alipaswa kufanya juu apate uzima wa milele, Yesu alimusaidia apate jibu mu Neno ya Mungu kwa kumuuliza hivi: “Ni nini imeandikwa katika Sheria? Wewe unasoma namna gani?” Ule mwanaume alitoa jibu ya muzuri. Alisema mambo yenye kuwa mu Maandiko yenye inasema kama inaomba kumupenda Mungu na kupenda jirani. (Law. 19:18; Kum. 6:5) Lakini, ona mambo yenye alisema kisha pale: “Kwa kweli jirani yangu ni nani?” Ile ilionyesha kama ule mwanaume hakuelewa kabisa maana ya mambo yenye alisoma. Kwa hiyo, hakujua namna ya kutumikisha muzuri ile maandiko mu maisha yake.

Tunaweza kukomalisha ufundi wetu wa kusoma ili kuelewa

5. Kusali na kusoma kwa mwendo wa polepole vinaweza kutusaidia namna gani?

5 Juu tuelewe muzuri zaidi Neno ya Mungu, tunapaswa kuwa na programu ya muzuri ya usomaji wa Biblia. Ona mapendekezo fulani yenye inaweza kukusaidia. Sali mbele uanze kusoma. Tuko na lazima ya musaada wa Yehova ili tuelewe Maandiko. Kwa hiyo, tunapaswa kumuomba roho yake takatifu ili itusaidie kukaza akili juu ya mambo yenye tuko nasoma. Kisha soma kwa mwendo wa polepole. Ile itakusaidia kuelewa mambo yenye unasoma. Kama unapenda unaweza kusoma kwa sauti ao kufuatana na usomaji wa Biblia wenye kurekodiwa. Kama uko nafuatana na usomaji wenye kurekodiwa mu Biblia yako, ile itakusaidia uelewe, ukumbuke na ujifunze mambo mingi zaidi. (Yos. 1:8) Wakati unamaliza kusoma sali tena ili kumushukuru Yehova juu alikupatia Neno yake, na umuombe akusaidie utumikishe mambo yenye ulisoma.

Picha: 1. Dada moya iko naandika mawazo fulani juu aitie mu Biblia yake. 2. Ndugu moya anatia alama ku maelezo na anaandika mawazo fulani ndani ya habari yenye iko najifunza yenye kuwa mu tablete yake. 3. Dada moya anatia alama ku maelezo na anaandika mawazo fulani mu Biblia yake kwa kutumia application “JW Library.”

Juu ya nini kuandika kwa kifupi mawazo fulani kunaweza kukusaidia uelewe na ukumbuke mambo yenye ulisoma? (Ona fungu ya 6)

6. Juu ya nini ni muzuri kujiuliza maulizo fulani na kuandika kwa kifupi mawazo fulani wakati uko nasoma Biblia?(Ona pia picha.)

6 Ona mapendekezo ingine mbili yenye inaweza kukusaidia uelewe muzuri zaidi mambo yenye uko nasoma mu Biblia. Ujiulize maulizo fulani juu ya mambo yenye unasoma. Wakati uko nasoma jambo fulani mu Biblia ujiulize hii maulizo: ‘Nani njo anazungumuziwa mu hii habari? Nani njo iko nasema? Iko nasema na nani na juu ya nini? Ile jambo ilitokea wapi na wakati gani?’ Ile maulizo itakusaidia ufikiri na kufuatana muzuri na mawazo makubwa yenye uko nasoma. Tena, wakati uko nasoma andika kwa kifupi mawazo fulani. Wakati unafanya vile, itaingia kabisa mu akili yako na utaielewa muzuri zaidi. Kuandika kutakusaidia pia ukumbuke mambo yenye unasoma. Unaweza kuandika maulizo fulani, mambo yenye ulipata kisha kufanya utafiti, unaweza kuandika kwa kifupi mawazo makubwa na namna unaweza kuitumikisha, ao kuandika tu mambo fulani juu ya namna uko najisikia kuhusu ile habari. Kuandika ile mambo kutakusaidia uone Neno ya Mungu sawa vile ujumbe wenye uliandikwa kwa ajili yako.

7. Wakati tuko nasoma Neno ya Mungu tuko na lazima ya sifa gani na juu ya nini? (Matayo 24:15)

7 Yesu alionyesha sifa ya maana sana yenye itatusaidia tuelewe mambo yenye tuko nasoma mu Neno ya Mungu. Ile sifa ni utambuzi. (Soma Matayo 24:15.) Utambuzi njo nini? Utambuzi ni uwezo wa kuelewa namna wazo fulani inapatana ao inatofautiana na ingine na kuelewa mambo yenye haionyeshwe waziwazi. Zaidi ya ile, sawa vile Yesu alisema, tuko na lazima ya utambuzi juu ya kuelewa matukio yenye inatimiza unabii wa Biblia. Tuko pia na lazima ya ile sifa juu mambo yote yenye tuko nasoma mu Biblia ituletee faida.

8. Namna gani tunaweza kutumia utambuzi wakati tuko nasoma?

8 Yehova anapatia watumishi wake utambuzi. Kwa hiyo, tunapaswa kusali kwake na kumuomba atusaidie tukomalishe ile sifa. (Mez. 2:6) Unaweza kufanya nini ili kutenda kulingana na sala yako? Uchunguze kwa uangalifu mambo yenye unasoma na uone namna gani inapatana na mambo ingine yenye unajua. Juu ya kufanya vile, tafuta habari mu vichapo vya kutusaidia kujifunza Biblia, sawa vile kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova. Vile vyombo vitakusaidia uelewe maana ya mambo yenye uko nasoma mu Biblia na uone namna unaweza kuitumikisha mu maisha yako. (Ebr. 5:14) Kutumia utambuzi wakati uko nasoma kutakusaidia uelewe muzuri zaidi Maandiko.

SOMA JUU UPATE MALI YA KIROHO

9. Ni kweli gani ya maana sana yenye kuwa mu Neno ya Mungu yenye Wasadukayo hawakukubali?

9 Wasadukayo walijua muzuri kabisa vitabu tano vya kwanza vya Maandiko ya Kiebrania. Lakini, hawakukubali kweli zenye zilikuwa mu vile vitabu vyenye viliongozwa na roho ya Mungu. Kwa mufano, fikiria namna Yesu alijibia Wasadukayo wakati walimuuliza kuhusu ufufuo. Aliwauliza hivi: “Hamukusoma katika kitabu cha Musa, katika habari kuhusu ule muti mudogo wa miiba, kwamba Mungu alimuambia: ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo’?” (Mk. 12:18, 26) Hata kama Wasadukayo walisoma ile andiko mara mingi, ulizo yenye Yesu aliwauliza ilionyesha kama hawakukubali kweli ya maana sana yenye kuwa mu Neno ya Mungu, ni kusema, fundisho juu ya ufufuo.​—Mk. 12:27; Lu. 20:38.d

10. Tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu nini wakati tuko nasoma?

10 Ile inaweza kutufundisha nini? Wakati tuko nasoma tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu mambo yote yenye andiko ao habari fulani yenye kuwa mu Biblia inaweza kutufundisha. Zaidi tu ya kuelewa mafundisho ya musingi, tunapenda pia kuelewa mafundisho mazito na kanuni zenye kuwa mu Biblia, zenye ziko sawa vile mali yenye kufichwa juu haiko mwepesi kuzipata.

11. Kulingana na 2 Timoteo 3:16, 17, unaweza kufanya nini ili upate mali ya kiroho wakati uko nasoma Biblia?

11 Unaweza kufanya nini ili kupata mali ya kiroho wakati uko nasoma Biblia? Fikiria mambo yenye 2 Timoteo 3:16, 17 inasema. (Soma.) Hii andiko inasema kama “kila Andiko liko . . . na faida” kwa(1) kufundisha, (2) kukaripia, (3) kunyoosha mambo, na (4) kutia nizamu. Unaweza kupata faida mu ile mambo ine hata kwa kuchunguza vitabu fulani vya Biblia vyenye hautumiake mara mingi. Chunguza kila habari yenye uko nasoma na uone mambo yenye inakufundisha juu ya Yehova, juu ya kusudi yake ao juu ya kanuni zenye zinatoka kwa Mungu. Uone ni mu njia gani iko na faida kwa kukaripia. Ufanye vile kwa kuchunguza namna ile habari inaweza kukusaidia utambue na uepuke muelekeo ao mutazamo mubaya, na uendelee kuwa muaminifu kwa Yehova. Uchunguze namna ile habari yenye kuwa mu Biblia inaweza kutumiwa ili kunyoosha mambo ao kurekebisha mawazo fulani ya mubaya yenye pengine mutu fulani mu mahubiri alitaya. Na utafute kila nizamu yenye inazungumuziwa mu andiko, yenye inaweza kukuzoeza ili ufikie kuanza kuona mambo sawa vile Yehova anaiona. Wakati unatia mu akili ile mambo ine utapata mali ya kiroho yenye itakuletea faida zaidi mu usomaji wako wa Biblia.

SOMA ILI UBADILIKE

12. Juu ya nini Yesu aliuliza Wafarisayo hii ulizo “Je, hamukusoma?”

12 Yesu aliuliza tena hii ulizo “Je, hamukusoma?” Aliuliza ile ulizo ili kuonyesha kama Wafarisayo walikuwa na mawazo yenye haifae juu ya Maandiko. (Mt. 12:1-7)e Ile wakati, Wafarisayo walikuwa nasema kama wanafunzi wa Yesu walivunjaka sheria ya Sabato. Juu ya kuwajibu, Yesu alitumia mifano mbili ya Maandiko na alizungumuzia mambo fulani yenye kuwa mu andiko ya Hosea juu ya kuonyesha kama Wafarisayo hawakuelewa sababu yenye ilifanya Sabato ikuwe, na ili kuonyesha kama hawakukuwa na rehema. Juu ya nini mambo yenye wale wanaume walikuwa nasoma mu Neno ya Mungu haikuwabadilisha? Ni juu walikuwa nachambua mambo yenye walikuwa nasoma na juu walikuwa na kiburi. Ile njo ilifanya washindwe kuelewa mambo yenye walikuwa nasoma.​—Mt. 23:23; Yoh. 5:39, 40.

13. Tunapaswa kuwa na mutazamo gani wakati tuko nasoma Biblia, na juu ya nini?

13 Mambo yenye Yesu alisema inatufundisha kama tunapaswa kuwa na mutazamo muzuri wakati tuko nasoma Biblia. Tofauti na Wafarisayo, tunapaswa kuwa wanyenyekevu na tayari kujifunza. Tunapaswa ‘kupokea kwa upole kupandwa kwa lile neno.’ (Yak. 1:21) Kama tuko wapole, Neno ya Mungu itatubadilisha. Mambo yenye Biblia inafundisha kuhusu rehema, huruma, na upendo itatusaidia kama tu tunaepuka kuwa na kiburi ao kama tunaepuka kuchambua mambo yenye kuwa mu Biblia.

Tunaweza kujua namna gani kama tuko naacha Neno ya Mungu itubadilishe? (Ona fungu ya 14)f

14. Ni nini inaweza kuonyesha kama tuko naacha Biblia itubadilishe? (Ona pia picha.)

14 Tunaweza kuonyesha kama tunaacha Neno ya Mungu itubadilishe mu namna yetu ya kutendea wengine. Juu Wafarisayo hawakuacha Neno ya Mungu ibadilishe mutazamo wao walianza ‘kulaumu watu wenye hawana kosa.’ (Mt. 12:7) Vilevile, namna tunaona na kutendea wengine inaonyesha ikiwa tulishaacha Neno ya Mungu itubadilishe. Kwa mufano, tunakuwaka tayari kusema mambo ya muzuri yenye tunaona kwa wengine ao tunakuwaka haraka kusema makosa yao? Tunakuwaka wenye rehema na tayari kusamehe wengine, ao tunachambuaka wengine na kuwawekea kinyongo wakati wanatukosea? Majibu yetu ku ile maulizo inaweza kuonyesha ikiwa tuko naacha mambo yenye tunasoma iongoze mawazo, hisia, na matendo yetu ao hapana.​—1 Ti. 4:12, 15; Ebr. 4:12.

KUSOMA NENO YA MUNGU KUNAFURAHISHA

15. Yesu alikuwa na mutazamo gani juu ya Maandiko Matakatifu?

15 Yesu alipenda Maandiko Matakatifu na maneno yenye kuwa mu Zaburi 40:8 inaonyesha mutazamo wenye Yesu alikuwa nao juu ya Neno ya Mungu. Inasema: “Ee Mungu wangu, ninafurahia kufanya mapenzi yako, na sheria yako iko ndani yangu kabisa.” Ile ilifanya akuwe na furaha na aendelee kumutumikia Yehova. Kama tunasoma Neno ya Mungu na kuipenda, siye pia tutakuwa na furaha na tutaendelea kumutumikia Yehova.​—Zb. 1:1-3.

16. Unaweza kufanya nini ili ufaidike na usomaji wako wa Biblia? (Ona kisanduku “Maneno ya Yesu Inaweza Kukusaidia Uelewe Mambo Yenye Uko Nasoma.”)

16 Tuache basi maneno ya Yesu na mufano wake vitusaidie tukomalishe ufundi wetu wa kusoma Biblia. Kusali, kusoma kwa mwendo wa polepole, kuuliza maulizo, na kuandika kwa kifupi mawazo fulani njo mambo yenye inaweza kutusaidia tuelewe muzuri zaidi mambo yenye tunasoma mu Biblia. Tunaweza kutumia utambuzi kwa kuchunguza kwa uangalifu mambo yenye tunasoma kupitia vichapo vyetu vyenye kutegemea Biblia. Tunaweza kujifunza kutumia muzuri zaidi Biblia, hata Maandiko yenye hatutumiake mara mingi, kwa kutafuta mali ya kiroho yenye kuwa mu habari zenye tuko nasoma. Na tunaweza kuacha Neno ya Mungu itubadilishe kwa kuendelea kuwa na mutazamo muzuri wakati tuko naisoma. Kama tunajikaza kufanya ile mambo yote, tutafaidika na usomaji wetu wa Biblia, na tutamukaribia Yehova zaidi.​—Zb. 119:17, 18; Yak. 4:8.

Maneno ya Yesu Inaweza Kukusaidia Uelewe Mambo Yenye Uko Nasoma

  • Ujikaze kuelewa mambo yenye uko nasoma na ukomalishe sifa ya utambuzi juu ujue namna ya kutumikisha ile mambo.​—Mt. 24:15; Lu. 10:25-37.

  • Chunguza kwa uangalifu habari zenye kuwa mu Biblia juu upate mali ya kiroho.​—Mk. 12:18-27.

  • Acha Neno ya Mungu ikubadilishe na ikuchochee kutendea wengine muzuri.​—Mt. 12:1-8.

WAKATI UKO NASOMA BIBLIA, NI NINI INAWEZA KUKUSAIDIA . . .

  • uelewe mambo yenye uko nasoma?

  • upate mali ya kiroho?

  • uache Neno ya Mungu ikubadilishe?

WIMBO 95 Mwangaza Unaendelea Kuongezeka

a Siye wote wenye kumuabudu Yehova tunajikazaka kusoma Neno yake kila siku. Watu wengi pia wanasomaka Biblia; lakini, hawaelewake kabisa mambo yenye wanasomaka. Ni vile pia ilikuwa kwa watu fulani wakati Yesu alikuwa ku dunia. Wakati tunachunguza maneno yenye Yesu aliambia wale wenye walikuwa nasoma Neno ya Mungu, tutajifunza mambo mbalimbali yenye inaweza kutusaidia tufaidike na usomaji wetu wa Biblia.

b Wakati alibatizwa na kutiwa mafuta kupitia roho takatifu, Yesu alikumbuka maisha yake ya mbinguni mbele akuwe mwanadamu.​—Mt. 3:16.

c Maria alijua muzuri Maandiko na alikuwa anaitaya. (Lu. 1:46-55) Inawezekana Yosefu na Maria hawakukuwa na makuta ya kujiuzia kopi za Maandiko. Kwa hiyo, walikuwa nasikiliza kwa uangalifu wakati watu walikuwa nasoma Neno ya Mungu ku sinagogi ili waweze kuikumbuka kisha.

d Ona habari “Umukaribie Mungu​—‘Yeye Ni Mungu . . . wa Walio Hai’” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 2, 2013.

e Ona pia Matayo 19:4-6. Mule Yesu anauliza tena Wafarisayo hii ulizo: “Je, hamukusoma?” Hata kama walisomaka mambo yenye Biblia inazungumuzia kuhusu uumbaji, hawakukubali mambo yenye inafundisha kuhusu namna Mungu anaona ndoa.

f MAFASIRIO YA PICHA: Wakati wa mukutano ku Jumba ya Ufalme, mumoya kati ya wandugu wenye wanashugulikiaka audio-vidéo anafanya makosa mingi. Lakini, kisha mukutano, wale wandugu wanamupongeza juu ya bidii yake kuliko kukaza akili juu ya makosa yenye alifanya.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine