Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp24 na. 1 uku. 4-5
  • Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Mambo Yenye Kuongoza Watu Wengi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Mambo Yenye Kuongoza Watu Wengi
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2024
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • NAMNA TUNAJISIKIA
  • NAMNA WENGINE WANAWAZA
  • NINI NJO ITAKUSAIDIA UKAMATE MAAMUZI YA MUZURI?
  • Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Ulizo Yenye Siye Wote Tunajiulizaka
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2024
  • Utangulizi
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2024
  • Faida ya Kuongozwa na Kanuni za Mwenendo
    Amuka!—2019
  • Kuwa na Zamiri ya Muzuri Mbele ya Mungu
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2024
wp24 na. 1 uku. 4-5
Ule kijana mwanaume mwenye kuwa mu habari yenye kutangulia iko natumikisha boussole wakati iko natembea. Anajikuta mbele ya shimu.

Namna tunajisikia inakuwaka tu muongozo wenye kutumainika?

Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Mambo Yenye Kuongoza Watu Wengi

Watu wengi wanajua kama matendo fulani inakuwaka tu ya muzuri na ingine inakuwaka tu ya mubaya. Kwa mufano, mauaji, ubakaji, na kutendea watoto mubaya kingono ni matendo yenye inajulikana kuwa ya mubaya. Lakini haki, fazili, na huruma ni mambo yenye kujulikana kuwa ya muzuri. Tuseme nini juu ya mambo ingine sawa vile, nani njo tunapaswa kufanya naye ngono, ikiwa tutasema kweli ao hapana, ao namna tunaweza kukomalisha watoto? Watu wengi wanawazaka kama kila mutu anaweza kufanya mambo yenye anapenda na kama mambo yoyote yenye mutu anapenda kufanya iko tu sawa. Mara mingi, watu wengi wanakamataka maamuzi yenye inategemea namna wanajisikia na namna wengine wanawaza kuhusu jambo fulani. Ni muzuri kufanya vile kila mara?

NAMNA TUNAJISIKIA

Mara mingi tunakamataka maamuzi yenye inategemea namna tunajisikia juu ya kuamua mambo ya muzuri na ya mubaya, na ile njo zamiri. (Waroma 2:​14, 15) Hata watoto, wanajua kutofautisha mambo ya muzuri na ya mubaya. Na wakati wanafanya mambo ya mubaya, wanajisikiaka mubaya. Wakati tulikuwa nakomala, zamiri yetu ilitegemea mambo yenye tulijifunza mu familia yetu, kwa vijana wenzetu, walimu wetu, watu wenye kutuzunguka, mu dini yetu, na mu desturi yetu. Wakati tunakamata maamuzi, zamiri yetu inatuambiaka kama mambo yenye tuliamua ni ya muzuri ao hapana.

Uwezo wetu wa kujua mambo ya muzuri na ya mubaya inaweza kutuchochea kuonyesha huruma, shukrani, kutendea wengine muzuri, na kuwaonyesha faraja. Inaweza pia kutuzuia kufanya mambo yenye inaweza kuumiza wale wenye tunapenda ao kutuzuia kufanya mambo yenye inaweza kutupatisha haya na kufanya tujihukumu.

Kukamata maamuzi yenye inategemea namna tunajisikia inakuwaka tu muongozo wenye kutumainika? Wakati alikuwa kijana, Garrick aliamua kuchagua njia fulani ya maisha, anasema hivi: “Ningeweza kufanya mambo yote yenye ningependa.” Lakini alifikia kuelewa kama, kufanya mambo yenye aliwaza kama ni ya muzuri, haikumuletea matokeo ya muzuri. Alifikia kusema kama maisha yake haikumuletea furaha hata kidogo juu iliyala “uasherati, ulevi, dawa za kulewesha, na jeuri mingi.”

NAMNA WENGINE WANAWAZA

Zaidi ya kukamata maamuzi yenye kutegemea namna tunajisikia, mara mingi tunafikiriaka pia namna wengine wataona maamuzi yetu. Ile inaweza kutusaidia tufaidike na uzoefu na hekima ya wengine. Watu wa familia yetu, marafiki, na watu wenye kutuzunguka, watatuheshimia wakati tunafanya mambo yenye wanawaza kama ni ya muzuri.

Kukamata maamuzi yenye inategemea mawazo ya wengine, inakuwaka tu muongozo wenye kutumainika? Wakati alikuwa kijana, Priscila alifanya mambo yenye marafiki wake waliona kama ni kawaida kufanya, na ile ilimusukuma kufanya ngono mbele ya ndoa. Lakini alifikia kuona kama, kufanya mambo yenye wengine waliona kuwa ya muzuri, haikumuletea furaha. Anasema hivi: “Kufanya mambo yenye watu wote wanafanyaka haikunifanya nijisikie muzuri. Ilinisukuma nifanye mambo ya upumbavu na ya hatari.”

NINI NJO ITAKUSAIDIA UKAMATE MAAMUZI YA MUZURI?

Wakati tunachagula kati ya mambo ya muzuri na ya mubaya, mawazo yetu na ya wengine inakuwaka ya maana. Lakini ile tu haiwezi kutuongoza juu tukuwe napata matokeo ya muzuri kila mara. Wakati fulani tunaweza kujiumiza ao kuumiza wengine juu hatuwezi kujua matokeo ya maamuzi yenye tunakamata. (Mezali 14:12) Hakuna kitu yenye inatuhakikishia kama mambo yenye siye na wengine tunaona kuwa sawa itatuletea matokeo ya muzuri na kama haiwezi kubadilika mu wakati yenye kuya. Kusema kweli, tabia zenye watu walikuwa wanaona kuwa za mubaya zamani, leo ziko naonekana kuwa za muzuri. Na tena matendo yenye ilikuwaka naonekana kuwa ya muzuri zamani, leo iko naonekana kuwa haifae.

Uleule kijana anasimama mu barabara yenye kuwa na pancarte yenye kuonyesha hatari. Watu wengine hawagaikie ile alama.

Kufuata mawazo ya wengine inakuwaka tu muongozo wenye kutumainika?

Kuko muongozo wa muzuri zaidi wenye unaweza kutusaidia kujua mambo ya muzuri na ya mubaya? Ni kanuni gani yenye tunaweza kufuata leo yenye inaweza kutusaidia tusivunjike moyo mu miaka yenye kuya?

Jambo ya kufurahisha ni kama, kuko fasi kwenye tunaweza kupata muongozo wenye kutumainika wenye haubadilikake na wenye unaweza kusaidia kila mutu fasi yote. Habari yenye kufuata, itazungumuzia fasi kwenye tunaweza kupata muongozo wenye kutumainika juu ya kujua mambo ya muzuri na ya mubaya.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine