HABARI YA KUJIFUNZA YA 29
WIMBO 121 Tukomalishe Sifa ya Kujizuia
Mukuwe Waangalifu ili Musiingie Katika Jaribu
“Muendelee kukesha na kusali bila kuacha, ili musiingie katika jaribu.”—MT. 26:41.
WAZO KUBWA
Kutusaidia kuelewa juu ya nini ni jambo ya maana kuepuka kufanya zambi na kuepuka mambo yenye inaweza kutuongoza kwenye zambi.
1-2. (a) Yesu alipatia wanafunzi wake onyo gani? (b) Juu ya nini wanafunzi walimuacha Yesu? (Ona pia picha.)
“KWA kweli, roho inataka lakini mwili ni muzaifu.”a (Mt. 26:41b) Kupitia ile maneno, Yesu alionyesha kama alielewa hali yetu ya kutokamilika. Lakini maneno yake iko pia na onyo fulani: Tuepuke kujitumainia sana. Uleule usiku, wanafunzi walisema kwa uhakika kama wataendelea kushikamana na mwalimu wao. (Mt. 26:35) Walikuwa na nia ya muzuri. Lakini hawakutambua kama ingekuwa mwepesi kwao kukosa nguvu wakati wa jaribu. Njo maana Yesu aliwaonya hivi: “Muendelee kukesha na kusali bila kuacha, ili musiingie katika jaribu.”—Mt. 26:41a.
2 Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba wanafunzi hawakuendelea kukesha. Wakati Yesu alikamatwa, je, walishikamana naye ao waliangukia mu jaribu na kukimbia? Juu hawakukuwa waangalifu, wanafunzi walifanya jambo yenye walisema kama hawatafanyaka: Walimuacha Yesu.—Mt. 26:56.
Yesu alishauria wanafunzi wake waendelee kukesha na wakuwe waangalifu ili wasiangukie mu jaribu, lakini walimuacha (Ona fungu ya 1-2)
3. (a) Ili kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova, juu ya nini tunapaswa kuepuka kujitumainia sana? (b) Tutazungumuzia nini mu hii habari?
3 Tunapaswa kuepuka kabisa kujitumainia sana. Kwa kweli, tumeazimia kuepuka kufanya jambo yoyote yenye itatutenganisha na Yehova. Lakini hatukamilike na ni mwepesi kwetu kuangukia mu jaribu. (Ro. 5:12; 7:21-23) Bila kutazamia, tunaweza kujikuta mu hali yenye inaweza kutuongoza kufanya jambo fulani ya mubaya. Ili kubakia washikamanifu kwa Yehova na Mwana wake, tunapaswa kufuata shauri ya Yesu ya kuendelea kuwa waangalifu ili tusiangukie mu jaribu ya kufanya zambi. Hii habari itatusaidia kufanya vile. Kwanza, tutaona ni mu mambo gani tunapaswa kuwa waangalifu sana. Kisha, tutaona namna tunaweza kuwa waangalifu ili tusiangukie mu jaribu. Na ku mwisho, tutaona namna ya kuendelea kuwa waangalifu.
TAMBUA UZAIFU WAKO
4-5. Juu ya nini tunapaswa kuwa waangalifu ili kuepuka hata zambi za kidogo-kidogo?
4 Hata zambi zenye zinaonekana kuwa za kidogo-kidogo zinaweza kuharibu uhusiano wetu pamoya na Yehova. Pia, zinaweza kutufanya tuangukie mu zambi nzito.
5 Siye wote tunajaribiwa kufanya zambi. Lakini kila mumoja wetu iko na uzaifu wake. Inaweza kuwa uzaifu wa kuangukia mu zambi nzito, kuangukia mu mwenendo fulani muchafu, ao kuwa na mawazo ya ulimwengu. Kwa mufano, pengine mutu fulani iko napiganisha jaribu ya kuangukia mu uasherati. Pengine mwingine iko na muelekeo wa kuwa na matendo machafu, sawa vile kugusa-gusa viungo vya uzazi ili kutimiza tamaa ya ngono ao kuangalia pornografia. Pengine mwingine uzaifu wenye iko napiganisha ni kuogopa wanadamu, kutegemea mawazo yake mwenyewe, kukasirika haraka, ao jambo ingine. Sawa vile Yakobo alionyesha, “kila mutu anajaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe.”—Yak. 1:14.
6. Hatupaswe kujidanganya juu ya jambo gani?
6 Unawaza inaweza kuwa mwepesi kwako kuangukia mu jaribu gani? Ni hatari sana kujidanganya na kusema kama hatuna uzaifu fulani ao kusema kama tuko na nguvu sana na hatuwezi kuangukia mu zambi. (1 Yo. 1:8) Paulo alisema kama hata wale wenye kuwa na “sifa za kustahili kiroho” wanaweza kuangukia mu jaribu kama hawaendelee kuwa waangalifu. (Gal. 6:1) Hatupaswe kujidanganya, na tunapaswa kukubali uzaifu wenye tuko nao.—2 Ko. 13:5.
7. Ni mu mambo gani tunapaswa kuwa waangalifu zaidi? Toa mufano.
7 Wakati unatambua jaribu yenye inaweza kuwa mwepesi kwako kuangukia ndani, unapaswa kufanya nini? Unapaswa kutumika sana ili uweze kushinda ile jaribu. Kwa mufano, zamani milango njo ilikuwa sehemu ya kuta ya muji yenye ilikuwa mwepesi kushambulia. Kwa hiyo, milango njo ililindwa sana. Vilevile, tunapaswa kuwa waangalifu sana mu mambo yenye tunajua kuwa tuko wazaifu.—1 Ko. 9:27.
NAMNA YA KUENDELEA KUWA WAANGALIFU
8-9. Kijana mwenye kuzungumuziwa mu Mezali sura ya 7 angefanya nini ili kuepuka kuangukia mu zambi nzito? (Mezali 7:8, 9, 13, 14, 21)
8 Namna gani tunaweza kujilinda? Tuchunguze mufano wa kijana mwenye kuzungumuziwa mu Mezali sura ya 7, na tuone mufano wake unaweza kutufundisha nini. Alifanya uasherati na mwanamuke mwasherati. Mustari wa 22 unasema kama ule kijana alifuata ule mwanamuke “mara moja” ao kwa kushitukia. Lakini mistari yenye kutangulia inaonyesha kama mbele ya pale, alikuwa amekamata hatua mbalimbali zenye zilimuongoza pole kwa pole kwenye zambi.
9 Ni nini ilimuongoza kwenye zambi? Kwanza, mangaribi “alipita katika . . . njia yenye kupeleka kwa mwanamuke [mwasherati].” Kisha, akaanza kuenda kwenye nyumba ya ule mwanamuke ilikuwa. (Soma Mezali 7:8, 9.) Na kisha, wakati aliona ule mwanamuke, hakugeuka na kubadilisha njia. Lakini alikubali ule mwanamuke amubusu na alisikiliza wakati alikuwa nazungumuzia zabihu za ushirika zenye alikuwa ametoa. Pengine alizungumuzia ile jambo juu afanye ule kijana awaze kama hakukuwa mutu mubaya. (Soma Mezali 7:13, 14, 21.) Kama ule kijana angeepuka hatari zenye zilimuongoza kwenye zambi, angejilinda ili asiangukie mu jaribu na asifanye zambi.
10. Namna gani leo mutu anaweza kufanya makosa yenye ule kijana alifanya?
10 Ule mufano wenye Sulemani alitoa unaonyesha jambo yenye inaweza kufikia muabudu yeyote wa Yehova. Anaweza kuangukia mu zambi nzito na kuwaza kama mambo ilitokea “mara moja” ao kwa kushitukia. Ao anaweza kusema, “nilishituka tu nilishafanya zambi.” Lakini, kama anafikiri juu ya mambo yenye ilitokea, anaweza kutambua kama alichukua hatua fulani za mubaya zenye zilimuongoza kwenye zambi. Pengine alikuwa na marafiki wabaya, alianza kujifurahisha na mambo yenye haifae, alikuwa naenda fasi zenye kuwa hatari, ao kuingia mu site zenye kuwa hatari. Pia, pengine alikuwa ameacha kusali, kusoma Biblia, kuenda ku mikutano, na kuhubiri. Sawa ule kijana mwenye kuzungumuziwa mu Mezali, inawezekana hakuangukia mu zambi kwa kushitukia tu.
11. Ili tusiangukie mu zambi, tunapaswa kuepuka nini?
11 Tunajifunza nini? Hatupaswe tu kuepuka zambi, tunapaswa pia kuepuka mambo yote yenye inaweza kutuongoza kwenye zambi. Kisha tu kuzungumuzia habari ya ule kijana na mwanamuke mwasherati, Sulemani anakazia pia ile wazo. Kuhusu ule mwanamuke, anasema hivi: “Musipotee njia na kufuata njia zake.” (Mez. 7:25) Anasema pia hivi: “Mukae mbali naye; musikaribie muingilio wa nyumba yake.” (Mez. 5:3, 8) Kwa kweli, tunajilinda ili tusifanye zambi kwa kuepuka hali zenye zinaweza kufanya tuangukie mu zambi.b Ile inamaanisha kama tunapaswa kuepuka mambo ao hali fulani zenye Wakristo hawakatazwe lakini zenye tunajua zinaweza kutuingiza mu jaribu.—Mt. 5:29, 30.
12. Yobu aliazimia kufanya nini, na namna gani azimio yake ingemulinda ili asiangukie katika jaribu? (Yobu 31:1)
12 Ili kuepuka hali zenye zinaweza kutuongoza kwenye zambi, tunapaswa kuazimia kabisa kuwa waangalifu. Vile njo Yobu alifanya. ‘Alifanya agano pamoja na macho yake,’ aliamua kama hataangalia kwa tamaa mwanamuke mwingine. (Soma Yobu 31:1.) Kushikamana na ile azimio kungemusaidia asiangukie hata siku moya katika uzinifu. Siye pia tunapaswa kuepuka jambo yoyote yenye inaweza kutuingiza mu jaribu.
13. Juu ya nini tunapaswa kulinda mawazo yetu? (Ona pia picha.)
13 Tunapaswa kulinda mawazo yetu. (Kut. 20:17) Watu fulani wanawaza kama haiko mubaya kwa mutu kuwazia-wazia mambo machafu kama tu hafanye ile mambo. Lakini mawazo ya vile haiko ya muzuri. Kama mutu anaendelea kuwaza juu ya mambo yenye haifae, atapenda sana kufanya ile mambo. Ni sawa vile iko najiletea yeye mwenyewe jaribu, na itamuomba sasa apiganishe ile jaribu. Kusema kweli, wakati fulani mawazo ya mubaya inakuyaka mu akili. Lakini jambo ya kufanya ni kukataa kabisa ile mawazo na kuanza kuwaza mambo ya muzuri. Wakati tunafanya vile, tunazuia mawazo ya mubaya kufikia kuwa tamaa yenye itakuwa nguvu kupiganisha na yenye inaweza hata kutuongoza ku zambi nzito.—Flp. 4:8; Kol. 3:2; Yak. 1:13-15.
Tunapaswa kuepuka jambo yoyote yenye inaweza kutuingiza mu jaribu (Ona fungu ya 13)
14. Ni nini ingine inaweza kutusaidia tujilinde ili tusiangukie mu jaribu?
14 Tunapaswa kufanya nini ingine ili kujilinda juu tusiangukie mu jaribu? Tunapaswa kuwa hakika kabisa kama kutii sheria ya Yehova kunatuleteaka tu faida. Wakati fulani inaweza kuomba kujikaza sana ili mawazo yetu na tamaa yetu ipatane na mambo yenye Mungu anakubali. Lakini tukijikaza kufanya vile, tutapata amani ya akili ya mingi sana, yenye hatuwezi kulinganisha na kitu.
15. Namna gani kujikaza kuwa na tamaa ya kufanya mambo ya muzuri kutatulinda tusiangukie mu jaribu?
15 Tunapaswa kukomalisha tamaa ya kufanya mambo ya muzuri. Kama tunajifunza ‘kuchukia mambo ya mubaya, na kupenda mambo ya muzuri,’ tutatia nguvu azimio yetu ya kufanya mambo yenye kuwa sawa na kuepuka hali zenye zinaweza kutuongoza kwenye zambi. (Amo. 5:15) Tamaa ya kufanya mambo ya muzuri itatusaidia pia kukamata maamuzi ya muzuri wakati tunajikuta mu hali yenye inatujaribu kufanya mambo ya mubaya, hali yenye hatukutazamia ao hatungeweza kuepuka.
16. Namna gani kufanya mambo ya kiroho kunaweza kutusaidia tuendelee kuwa waangalifu? (Ona pia picha.)
16 Tunaweza kukomalisha namna gani tamaa ya kufanya mambo ya muzuri? Tunapaswa kuwa na mambo mengi ya kiroho ya kufanya. Wakati tuko ku mikutano ao mu mahubiri, haikuwake mwepesi kujaribiwa kufanya mambo ya mubaya. Mikutano na mahubiri inatusaidiaka tukuwe na tamaa ya kumufurahisha Yehova. (Mt. 28:19, 20; Ebr. 10:24, 25) Wakati tunasoma na kujifunza Neno ya Mungu na kutafakari sana juu ya mambo yenye tunajifunza, tunapenda sana kufanya mambo ya muzuri na tunachukia zaidi mambo ya mubaya. (Yos. 1:8; Zb. 1:2, 3; 119:97, 101) Kumbuka kama Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: ‘Musali bila kuacha, ili musiingie katika jaribu.’ (Mt. 26:41) Wakati tunazoea kusali kwa Baba yetu wa mbinguni, tunamupatia nafasi ya kutusaidia na ya kutia nguvu azimio yetu ya kumufurahisha.—Yak. 4:8.
Kuwa na programu ya muzuri ya kiroho kunaweza kutusaidia kuepuka majaribu (Ona fungu ya 16)c
ENDELEA KUWA MUANGALIFU
17. Petro aliangukia mu uzaifu gani zaidi ya mara moya?
17 Inaweza kuwa mwepesi kushinda kabisa uzaifu fulani. Lakini kuko uzaifu wenye pengine inaomba tuendelee kupiganisha kwa muda murefu zaidi. Fikiria mufano wa mutume Petro. Aliangukia mu mutego wa kuogopa wanadamu wakati alimukana Yesu mara tatu. (Mt. 26:69-75) Ilionekana kama Petro alishinda uzaifu wake wa kuogopa wanadamu wakati alitoa ushahidi kwa uhodari mbele ya Sanhedrini. (Mdo. 5:27-29) Lakini, miaka fulani kisha pale, juu ya “kuogopa wale wa kikundi cha wenye kutahiriwa,” kwa wakati fulani aliacha kula na Wakristo wa mataifa. (Gal. 2:11, 12) Uzaifu wa kuogopa wanadamu wenye Petro alikuwa nao ulirudia. Pengine haukukuwa umeisha kabisa-kabisa.
18. Kuhusu uzaifu fulani, ni nini inaweza kutokea?
18 Tunaweza kujikuta mu hali sawa ya Petro. Namna gani? Uzaifu fulani wenye tuliwaza kama tumeshinda unaweza kurudia na kutujaribu tena. Kwa mufano, ndugu moya anasema hivi: “Niliweza kuepuka kuangalia pornografia kwa miaka kumi, na nilijisadikisha kama sikukuwa tena na ule uzaifu. Lakini uzaifu wangu ulikuwa sawa vile munyama hatari mwenye kujificha, mwenye iko nangoya wakati wenye kufaa ili kushambulia.” Jambo ya kufurahisha ni kwamba, ule ndugu aliendelea kujikaza. Alitambua kama alipaswa kujikaza kila siku ili kushinda uzaifu wake, pengine alipaswa kufanya vile maisha yake yote mu huu ulimwengu wa Shetani. Kwa musaada wa bibi yake na wa wazee, alikamata hatua zingine ili kuendelea kushinda jaribu ya kuangalia pornografia.
19. Tunapaswa kufanya nini kama tuko na uzaifu fulani wenye haupendi kuisha?
19 Namna gani tunaweza kupiganisha uzaifu wenye haupendi kuisha ili tusiangukie mu jaribu ya kufanya jambo ya mubaya? Kwa kufuata hii shauri yenye Yesu alitoa kuhusu majaribu: “Muendelee kukesha.” Hata mu wakati wenye unajisikia uko na nguvu, uendelee kuepuka hali zenye zinaweza kukuingiza mu jaribu. (1 Ko. 10:12) Endelea kutumikisha mambo yenye ilikusaidia kupiganisha uzaifu wako. Mezali 28:14 inasema hivi: “Mwenye furaha ni mutu mwenye kuwa muangalifu sikuzote.”—2 Pe. 3:14.
BARAKA YA KUENDELEA KUWA WAANGALIFU
20-21. (a) Tutapata baraka gani kama tunaendelea kuwa waangalifu ili tusiingie mu jaribu? (b) Kama tunafanya sehemu yetu, Yehova atatufanyia nini? (2 Wakorinto 4:7)
20 Tunaweza kuwa hakika kama tutapata baraka mingi kama tunaendelea kuwa waangalifu ili tusiangukie mu jaribu. ‘Furaha ya muda’ yenye zambi inaweza kuleta, haiko kitu tukiilinganisha na furaha ya mingi sana yenye tunapata wakati tunafuata kanuni za Yehova. (Ebr. 11:25; Zb. 19:8) Tunasema vile juu tuliumbwa ili tuishi namna Mungu anapenda. (Mwa. 1:27) Kama tunafanya vile, tutakuwa na zamiri safi na tutaendelea kuwa na tumaini ya kuishi milele.—1 Ti. 6:12; 2 Ti. 1:3; Yud. 20, 21.
21 Ni kweli kwamba “mwili ni muzaifu,” lakini ile haimaanishe kama hatuna kitu ya kufanya. Yehova iko tayari kutupatia nguvu yenye tuko nayo lazima. (Soma 2 Wakorinto 4:7.) Ona kwamba nguvu yenye Yehova anatupatia, ni nguvu yenye kupita ile ya kawaida. Lakini, siye wenyewe tunapaswa kwanza kutumia nguvu yetu ya kawaida kila siku ili kupiganisha uzaifu wetu. Kama tunafanya sehemu yetu, tukuwe hakika kama Yehova atajibia sala yetu na kutuongezea nguvu yenye tuko nayo lazima. (1 Ko. 10:13) Kwa kweli, kwa musaada wa Yehova tunaweza kuendelea kuwa waangalifu ili tusiangukie katika jaribu.
WIMBO 47 Usali kwa Yehova Kila Siku
a MAFASIRIO YA MANENO FULANI: “Roho” yenye kuzungumuziwa mu Matayo 26:41 ni nguvu yenye kuwa ndani yetu yenye inafanya tujisikie ao tutende mu njia fulani. “Mwili” ni hali yetu ya kutokamilika. Tunaweza kuwa kabisa na nia ya kufanya mambo ya muzuri, lakini kama hatuko waangalifu, tunaweza kuangukia mu jaribu ya kufanya mambo yenye Biblia inakataza.
b Mutu mwenye ameangukia mu zambi nzito anaweza kupata musaada mu kitabu Furahia Maisha Milele!, somo ya 57 nukta ya 1-3, na mu habari “Uendelee ‘Kuangalia Mbele’” mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 11, 2020, uku. 27-29, fu. 12-17.
c MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu iko nasoma andiko ya siku asubui, anasoma Biblia wakati wa mapumuziko, na iko nahuzuria mikutano mangaribi.