HABARI YA KUJIFUNZA YA 22
WIMBO 15 Tumusifu Muzaliwa wa Kwanza wa Yehova!
Yesu Anaona Jina ya Yehova Kuwa ya Maana Sana
“Nimewajulisha jina lako na nitalijulisha.”—YOH. 17:26.
WAZO KUBWA
Namna Yesu alijulisha jina ya Mungu na namna aliitakasa na kuitetea.
1-2. (a) Yesu alifanya nini busiku mbele bamuue? (b) Tutajibia maulizo gani mu hii habari?
NI MANGARIBI ya Siku ya Ine, tarehe 14 Mwezi wa Nisani, mwaka wa 33. Yesu anamaliza kula chakula ya pekee pamoya na mitume wake waaminifu mu chumba fulani ya juu. Kuko mambo mingi yenye iko karibu kumupata Yesu. Batamusaliti, batamusambisha, batamuhukumu, batamutesa na kumuua. Njo maana kisha kula anaambia mitume wake waaminifu maneno ya mwisho-mwisho ya kubatia moyo. Na mbele batoke mu ile chumba, Yesu anatoa sala ya maana sana. Mutume Yohana aliandika ile sala, inapatikana mu Yohana sura ya 17.
2 Sala ya Yesu inaonyesha kama alikuwa nahangaikia nini mbele akufe? Namna gani ile sala inaonyesha jambo yenye Yesu aliona kuwa ya maana mu utumishi wake wote ku dunia? Tutazungumuzia majibu ya ile maulizo.
“NIMEWAJULISHA JINA LAKO”
3. Yesu alisema nini juu ya jina ya Yehova, na alimaanisha nini? (Yohana 17:6, 26)
3 Yesu alisema hivi mu sala yake: “Nimewajulisha jina lako.” Na haiko mara moya tu njo alisema vile. Alisema mara mbili kama alijulisha banafunzi yake jina ya Yehova. (Soma Yohana 17:6, 26.) Lakini banafunzi ya Yesu balikuwa Bayahudi, kwa hiyo balijua muzuri kama jina ya Mungu ni Yehova juu ilipatikana mara mingi mu Maandiko ya Kiebrania. Sasa, Yesu alimaanisha nini wakati alisema ‘nimewajulisha jina yako’? Yesu hakumaanisha kama ni yeye njo alifundisha banafunzi yake kama jina ya pekee ya Mungu ni Yehova. Lakini, juu yeye njo alimujua Yehova muzuri sana, alipenda kusaidia banafunzi yake bajue Yehova ni Mungu wa namna gani, ni kusema sifa zake, mambo yenye alishafanya, mambo yenye atafanya, na kusudi yake juu ya dunia na banadamu.
4-5. (a) Leta mufano yenye inaonyesha namna jina ya mutu inaweza kuwa ya maana sana kwetu. (b) Ni mu njia gani banafunzi ya Yesu balifikia kujua jina ya Yehova?
4 Juu ya kuelewa ile maneno ya Yesu, tufikirie hii mufano: Tuseme mu kutaniko yenu muko muzee moya mwenye jina yake ni David na ni munganga. Unamujua tangu zamani. Kisha siku moya unagonjwa sana na banakupeleka mbio ku hopitale kwenye ule ndugu anatumikaka. Ule ndugu anakutunza na unapona. Kuanzia pale jina ya ule ndugu itakuwa ya maana sana kwako. Wakati utakuwa nasikia jina David, hautaona tu muzee wa mu kutaniko yenu, utaona pia munganga mwenye alikusaidiaka upone.
5 Banafunzi ya Yesu nabo balijua kama jina ya Mungu ni Yehova. Lakini utumishi wa Yesu ulifanya baone jina ya Yehova kuwa ya maana hata zaidi. Juu ya nini tunasema vile? Juu Yesu alimuiga Baba yake mu mambo yote yenye alisema na kufanya. Kwa hiyo, wakati banafunzi yake balikuwa nasikiliza namna alikuwa nafundisha na kuona namna alikuwa natendea batu, balifikia ‘kujua’ Yehova muzuri.—Yoh. 14:9; 17:3.
“JINA LAKO LENYE UMENIPATIA”
6. Yesu alipenda kumaanisha nini wakati alisema kama amepewa jina ya Mungu? (Yohana 17:11, 12)
6 Mu ile sala yenye Yesu alitoa juu ya banafunzi yake, alisema hivi: “Uwalinde kwa sababu ya jina lako lenye umenipatia.” (Soma Yohana 17:11, 12.) Ni kusema Yehova njo ingekuwa sasa jina ya Yesu? Hapana. Wakati Yesu anazungumuzia jina Yehova, anasema “jina lako.” Kwa hiyo, jina Yehova haikugeuka na kuwa jina ya pekee ya Yesu. Sasa, Yesu alipenda kumaanisha nini wakati alisema kama amepewa jina ya Mungu? Kwanza, Yehova alimutuma Yesu aseme mu jina yake. Yesu alikuya mu jina ya Baba yake na alifanya miujiza mu ile jina. (Yoh. 5:43; 10:25) Tena, jina ya Yesu inamaanisha “Yehova Ni Wokovu.” Kwa hiyo, mu maana ya jina ya Yesu muko jina Yehova.
7. Leta mufano yenye inaonyesha namna iliwezekana Yesu aseme mu jina ya Yehova.
7 Juu ya kuelewa ni mu maana gani Yesu alisema mu jina ya Yehova, fikiria hii mufano. Mufalme anatuma mutu aseme mu jina yake. Wakati ule mutu atasema, maneno yake itakuwa na buzito juu itakuwa sawa vile ni mufalme njo iko nasema. Vilevile, Yesu alikuwa na mamlaka ya kusema mu jina ya Yehova juu Yehova njo alimutuma.—Mt. 21:9; Lu. 13:35.
8. Ni mu maana gani jina ya Yehova ilikuwa “ndani” ya Yesu mbele akuye ku dunia? (Kutoka 23:20, 21)
8 Biblia inamuita Yesu kuwa “Neno” juu Yehova alimutumikisha juu aambie malaika na banadamu mambo yenye anapenda bajue na bafanye. (Yoh. 1:1-3) Inawezekana Yesu njo alikuwa ule malaika mwenye Yehova alituma ahangaikie Baisraeli wakati balikuwa banatoka Misri. Yehova aliambia Baisraeli batii ule malaika, na aliongeza hivi: “Kwa sababu jina langu liko ndani yake.”a (Soma Kutoka 23:20, 21.) Juu ya nini Yehova alisema vile? Yehova alisema kama jina yake iko “ndani” ya Yesu juu Yesu anasema mu jina ya Yehova na ni yeye njo anatetea na kutakasa jina ya Yehova kupita bengine bote.
“BABA, TUKUZA JINA LAKO”
9. Nini inaonyesha kama Yesu aliona jina ya Yehova kuwa ya maana? Fasiria.
9 Sawa vile tumeona, hata mbele Yesu akuye ku dunia aliona jina ya Yehova kuwa ya maana sana. Njo maana mambo yote yenye Yesu alifanya ku dunia ilionyesha kama anaona jina ya Yehova kuwa ya maana. Ku mwisho-mwisho wa utumishi wake, Yesu alimuambia hivi Yehova mu sala: “Baba, tukuza jina lako.” Palepale, kwa sauti kubwa, Baba yake alijibia hivi kutoka mbinguni: “Nimelitukuza na nitalitukuza tena.”—Yoh. 12:28.
10-11. (a) Yesu alitukuza namna gani jina ya Yehova? (Ona pia picha.) (b) Juu ya nini jina ya Yehova inapaswa kutakaswa na kutetewa?
10 Yesu naye alitukuza jina ya Baba yake. Alifanya vile namna gani? Alifundisha bengine sifa za Yehova na mambo ya ajabu yenye Yehova anafanya. Lakini Yesu hakuishia pale. Alifanya mambo ingine juu ya kutukuza jina ya Baba yake. Ilikuwa lazima kutakasa jina ya Yehova na kumutetea.b Yesu alionyesha kama aliona ile kuwa ya maana wakati alifundisha banafunzi yake sala ya Baba yetu. Mu ile sala, alisema hii maneno: “Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe.”—Mt. 6:9.
11 Juu ya nini jina ya Yehova inapaswa kutakaswa na kutetewa? Juu mu bustani ya Edeni, Shetani alisema mambo ya bongo juu ya Yehova Mungu. Shetani alisema kama Yehova ni musema-bongo na kama alikuwa naima Adamu na Eva jambo fulani ya muzuri. (Mwa. 3:1-5) Wakati Shetani alisema vile, alipenda kuonyesha kama namna ya Yehova ya kufanya mambo haiko ya muzuri. Ile mambo ya bongo yenye Shetani alisema ilichafula jina ya Yehova. Ingefanya batu bawaze kama Yehova ni Mungu mubaya. Na Shetani hakuishia pale. Mu wakati wa Yobu, alisema kama bale benye biko namutumikia Yehova banafanya vile juu tu ya kupata faida fulani. Ile mashitaka ya bongo ilipenda kuonyesha kama wakati batu batapata magumu bataacha kumutumikia Yehova juu habamupendi. (Yob. 1:9-11; 2:4) Iliomba wakati juu ya kujua ni nani njo musema-bongo, ni Yehova ao ni Shetani?
Yesu alifundisha banafunzi yake kama ni jambo ya maana kutakasa jina ya Mungu (Ona fungu ya 10)
“NINATOA UZIMA WANGU”
12. Yesu alikuwa tayari kufanya nini juu alipenda jina ya Yehova?
12 Yesu alimupenda sana Yehova. Njo maana alikuwa tayari kufanya yake yote juu ya kutakasa na kutetea jina ya Yehova. Alisema hivi: “Ninatoa uzima wangu.” (Yoh. 10:17, 18) Ile inaonyesha kama Yesu alikuwa tayari hata kufa juu ya jina ya Yehova.c Alikuwa tofauti kabisa na banadamu bakamilifu ba kwanza, Adamu na Eva. Balimuacha Yehova na kujiunga na Shetani. Lakini, Yesu yeye alikuwa tayari kuya hapa ku dunia na kuonyesha kama anamupenda Yehova. Alionyesha vile namna gani? Alimutii Yehova mu mambo yote yenye alisema na kufanya. (Ebr. 4:15; 5:7-10) Aliendelea kuwa muaminifu maisha yake yote mupaka kifo, kifo ya maumivu ku muti wa mateso. (Ebr. 12:2) Kwa kufanya vile, alionyesha kama anapenda Yehova na jina ya Yehova.
13. Juu ya nini Yesu njo alistahili kabisa kuonyesha kama Shetani ni musema-bongo? (Ona pia picha.)
13 Mambo yote yenye Yesu alifanya ilionyesha kama Shetani njo musema-bongo, hapana Yehova! (Yoh. 8:44) Yesu anamujua Yehova muzuri sana kupita batu yote. Kama mu mambo yote yenye Shetani alisema juu ya Yehova mungekuwa hata ka kweli kadogo, Yesu angejua. Lakini juu Yesu alijua kama mambo yote yenye Shetani alisema ilikuwa ya bongo, aliendelea kutetea kwa bidii jina ya Yehova. Yesu alikuwa tayari kufa kuliko kumuacha Baba yake, hata wakati ilionekana sawa vile Baba yake amemuacha.—Mt. 27:46.d
Mambo yenye Yesu alifanya ilionyesha waziwazi kama Shetani njo musema-bongo, hapana Yehova! (Ona fungu ya 13)
“NIMEMALIZA KAZI YENYE ULINIPATIA NIFANYE”
14. Yehova alimubariki Yesu namna gani?
14 Mu sala yenye Yesu alitoa busiku mbele akufe, alikuwa na sheria ya kusema hivi: “Nimemaliza kazi yenye ulinipatia nifanye.” Alikuwa hakika kama Yehova atamubariki juu alibakia muaminifu. (Yoh. 17:4, 5) Na Baba yake alimubariki. Hakumuacha mu kaburi. (Mdo. 2:23, 24) Alimufufula na akamupatia cheo ya yulu sana mbinguni. (Flp. 2:8, 9) Kisha wakati, Yesu akakuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Ule Ufalme utafanya nini? Sehemu ya pili ya sala ya Baba yetu inajibia ile ulizo, inasema hivi: “Ufalme wako ukuje. Mapenzi yako [Yehova] yafanyike duniani kama mbinguni.”—Mt. 6:10.
15. Yesu atafanya nini?
15 Karibuni Yesu atapiganisha maadui wa Mungu na ataharibu batu babaya ku Armagedoni. (Ufu. 16:14, 16; 19:11-16) Kisha tu pale, Yesu atamutupa Shetani mu “abiso,” ni kusema Shetani atakuwa mu hali yenye hawezi kufanya kitu yoyote. (Ufu. 20:1-3) Mu Utawala wake wa Miaka Elfu, Yesu atarudisha amani na atasaidia banadamu bakuwe tena bakamilifu. Atafufula bafu na atageuza dunia yote kuwa paradiso. Kusudi ya Yehova itatimia!—Ufu. 21:1-4.
16. Mambo itakuwa namna gani ku mwisho wa ile Miaka Elfu?
16 Mambo itakuwa namna gani ku mwisho ya ile Miaka Elfu? Zambi na kutokamilika habitakuwa tena. Kwa hiyo, banadamu habatakuwa tena na lazima ya kuomba musamaha wa zambi kwa musingi wa zabihu ya ukombozi. Na juu baweze kuwa na burafiki bwa karibu pamoya na Yehova, habatakuwa tena na lazima ya makuhani wale 144 000, ao Kuhani Mukubwa Yesu Kristo. Pia kifo, “adui wa mwisho,” atakuwa ameharibiwa. Bafu batakuwa balishafufuliwa. Na kila mutu ku dunia atakuwa mukamilifu.—1 Ko. 15:25, 26.
17-18. (a) Ni nini itatokea ku mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu? (b) Yesu atafanya nini ku mwisho ile Miaka Elfu? (1 Wakorinto 15:24, 28) (Ona pia picha.)
17 Ni jambo ingine gani itatokea ku mwisho wa ile Miaka Elfu? Jambo fulani ya ajabu itatokea. Itakuwa ilishaonekana wazi kama jina ya Yehova ni takatifu na kama Yehova ni Mungu mwenye haki. Juu ya nini tunasema vile? Mu bustani ya Edeni Shetani alisema kama Yehova ni musema-bongo na hatawale banadamu muzuri. Tangu ile wakati, batu benye kumuheshimia Yehova bametakasa jina yake tena na tena. Kwa hiyo ku mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu, jina ya Yehova itakuwa ilishatakaswa kabisa-kabisa. Atakuwa ameonyesha waziwazi kama yeye ni Baba wa mbinguni mwenye upendo.
18 Ku mwisho ya ile Miaka Elfu, batu yote batajua kama mambo yenye Shetani alisema juu ya Yehova ni ya bongo. Sasa, Yesu atafanya nini wakati utawala wake utafika ku mwisho? Atamupinga Yehova sawa vile Shetani alifanya? Hapana! (Soma 1 Wakorinto 15:24, 28.) Yesu atarudishia Baba yake Ufalme na atajitiisha ku mamlaka ya Yehova. Tofauti na Shetani, Yesu iko tayari kuacha mamlaka yote juu anamupenda Yehova.
Kwa kujipendea, Yesu anamurudishia Yehova Ufalme ku mwisho wa Miaka Elfu ya Utawala wake (Ona fungu ya 18)
19. Nini inaonyesha kama Yesu anaona jina ya Yehova kuwa ya maana?
19 Haishangaze kuona kama Yehova alikuwa tayari kumupatia Yesu jina yake. Yesu alionyesha kwa ukamili Baba yake ni Mungu wa namna gani. Sawa vile tumejifunza, Yesu anaona jina ya Baba yake kuwa ya maana sana kupita bitu yote. Alikuwa tayari kufa juu ya ile jina, na atakuwa tayari kumurudishia Yehova mamlaka yote ku mwisho wa ile Miaka Elfu. Na siye tunaweza kumuiga Yesu namna gani? Tutapata jibu ya ile ulizo mu habari ya kufuata.
WIMBO 16 Tumusifu Yehova na Mwana Wake Mutiwa-Mafuta
a Wakati fulani bamalaika balikuwa nasema mu jina ya Yehova wakati balikuwa napeleka ujumbe wake. Njo maana, wakati fulani Biblia inasema kama Yehova alikuwa nasema hata kama ni malaika njo mwenye alikuwa nasema. (Mwa. 18:1-33) Kwa mufano, Maandiko inasema kama Yehova njo alimupatia Musa Sheria, lakini maandiko ingine inatusaidia kuelewa kama Yehova alitumia bamalaika juu ya kupatia Musa ile Sheria.—Law. 27:34; Mdo. 7:38, 53; Gal. 3:19; Ebr. 2:2-4.
b MAANA YA MANENO FULANI: “Kutakasa” maana yake kuheshimia, kuona kuwa takatifu. “Kutetea” maana yake kuonyesha kama mutu hana kosa, ao kuonyesha kama mambo yenye balisema juu yake ni ya bongo.
c Kifo ya Yesu ilipatia pia banadamu nafasi ya kupata uzima wa milele.
d Ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 4, 2021, uku. 30-31.