Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 6 uku. 26-31
  • Mufundishaji Wetu Mukubwa Ametufundisha Mambo Mingi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mufundishaji Wetu Mukubwa Ametufundisha Mambo Mingi
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MUFANO WENYE BAZAZI YANGU BALINIACHIA
  • NAANZA UTUMISHI WA WAKATI WOTE
  • MAISHA YA UMISIONERE
  • ULAYA KISHA AFRIKA
  • MASHARIKI YA KATI
  • TUNARUDIA AFRIKA
  • Nimeazimia Kama Sitaacha Mikono Yangu Iregee
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Yehova Alinibariki Sana Kupita Vile Niliwazia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Yehova ‘Amenyoosha [Njia] Yangu’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Mambo ya Kufurahisha Yenye Hatukutazamia na Mambo Yenye Tulijifunza mu Utumishi wa Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 6 uku. 26-31
Franco Dagostini.

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Mufundishaji Wetu Mukubwa Ametufundisha Mambo Mingi

INAELEZWA NA FRANCO DAGOSTINI

KUSIMAMISHWA na maaskari wenye kuwa na bunduki, batu kuchoma bitu juu ya kufunga barabara, upepo mukali, vita za wenyewe kwa wenyewe, na batu kukimbia eneo yao. Ile ni kati ya magumu yenye miye na bibi yangu tulikutana nayo mu kazi yetu ya upainia na ya umisionere. Hata kama tulipata ile magumu, tulifurahia uamuzi wenye tulikamata. Mu ile mambo yote Yehova alitutegemeza na kutubariki. Na alitufundisha mambo mingi ya maana juu yeye ni mufundishaji wetu mukubwa.—Yob. 36:22; Isa. 30:20.

MUFANO WENYE BAZAZI YANGU BALINIACHIA

Ku mwisho ya miaka ya 1950, bazazi yangu balitoka Italia na kuhamia Kindersley, Saskatchewan, mu Kanada. Kisha wakati kidogo balijifunza kweli, na kweli ikakuwa jambo ya maana mu maisha yetu. Ninakumbuka wakati nilikuwa mutoto, nilipitisha saa mingi mu mahubiri pamoya na familia yangu. Njo maana saa moya ninafanyaka muzaa na kusema nilikuwaka painia musaidizi na miaka munane!

Franco wakati alikuwa mutoto pamoya na bazazi yake na bandugu yake.

Pamoya na familia yangu, mu 1966 hivi

Hata kama bazazi yangu habakukuwa na makuta mingi, balituachia mufano muzuri ya kujitoa sana kwa ajili ya Yehova. Kwa mufano, mu 1963 baliuzisha bitu yabo mingi juu ya kupata makuta ya kuenda ku Mukusanyiko wa Kimataifa wenye ulifanyika mu Pasadena, Kalifornia, mu Amerika. Mu 1972 tulihamia Trail, Colombie Britanique mu Kanada yenye ilikuwa ku kilometre 1000 juu ya kusaidia benye balikuwa nazungumuza Kiitalia. Baba yangu alikuwa nafanya kazi ya kusafisha manyumba. Alikuwa anakatala kazi zenye kulipa makuta ya mingi juu apate wakati mingi ya kuhangaikia mambo ya kiroho.

Niko mwenye furaha sana juu ya mufano wenye bazazi yangu balituachia miye na bandugu yangu tatu. Mufano yao ilikuwa sehemu ya kwanza ya mazoezi yangu mu utumishi wa Yehova. Balinifundisha hii jambo yenye siwezi kusahabu hata siku moya: Kama ninaweka Ufalme pa nafasi ya kwanza, Yehova atanihangaikia.—Mt. 6:33.

NAANZA UTUMISHI WA WAKATI WOTE

Mu 1980 nilioa Debbie, dada muzuri mwenye alikuwa na miradi ya kiroho. Tulipenda kuanza utumishi wa wakati wote, njo maana Debbie alianza upainia miezi tatu tu kisha ndoa yetu. Mwaka moya kisha kuoana, tulihamia mu kutaniko ya kidogo yenye ilikuwa na lazima ya wahubiri. Ile wakati njo nilijiunga na bibi yangu Debbie mu kazi ya upainia.

Franco na Debbie siku ya ndoa yao.

Siku ya ndoa yetu, 1980

Kisha wakati fulani, tulivunjika moyo na tulipenda kuenda fasi ingine. Lakini tulizungumuza kwanza na mwangalizi wa muzunguko. Kwa upendo alituambia hivi waziwazi: “Nyie wenyewe njo muko nafanya mambo ikuwe nguvu zaidi kwa sababu muko nakazia akili tu magumu yenye muko nayo, lakini kama munakazia akili mambo ya muzuri mutaiona.” Tulikuwa na lazima ya ile shauri. (Zb. 141:5) Tuliitumikisha bila ku kawia na tukaanza kuona kama kulikuwa mambo mingi ya muzuri. Kwa mufano, bandugu na dada ba mingi mu kutaniko, kutia ndani batoto na badada benye ba bwana yabo habakukuwa Mashahidi, balipenda kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova. Ile ilitufundisha hii jambo ya lazima: Kukazia akili mambo ya muzuri na kuwa hakika kama kwa wakati wenye kufaa Yehova atatengeneza mambo. (Mik. 7:7) Furaha yetu ilirudia na mambo iliendelea muzuri.

Baalimu benye balitufundisha ku masomo yetu ya kwanza ya upainia balikuwa balishatumikia mu mainchi ingine. Balituonyesha ma picha na balizungumuzia magumu na baraka yenye balipata mu ile migao yabo. Ile ilituchochea na siye tupende kazi ya umisionere. Kwa hiyo tulijiwekea muradi wa kuwa bamisionere.

Fasi ya kuwekea magari ku Jumba ya Ufalme kisha teluji mingi kuanguka.

Ku jumba ya Ufalme mu Colombie Britanique, 1983

Juu ya kufikia muradi wetu, mu 1984 tulihamia Quebec kwenye banazungumuza kifaransa. Ilikuwa ku 4000 kilometre na Colombie Britanique kwenye tulikuwa. Tulipaswa kujifunza luga ya mupya na kuzoea desturi ya mupya. Tatizo ingine yenye tulipata ni kwamba mara mingi hatukukuwa na makuta ya mingi. Wakati fulani chakula yote yenye tulikuwa nayo ni viazi vyenye mwenye shamba alituruhusu tuchukue mu shamba yake. Bibi yangu Debbie alikuwa napika vile viazi mu njia tofauti-tofauti. Hata kama tulipata ile magumu yote hatukupoteza furaha yetu. Na zaidi ya yote tuliona namna Yehova alikuwa natuhangaikia.—Zb. 64:10.

Siku moya, bila kutazamia balituita ku telefone. Balituomba tuende kutumikia ku Beteli ya Kanada. Hata kama tulifurahia ile mwaliko tulichanganikiwa kidogo sababu mbele ya pale tulijaza ombi ya kuenda ku Masomo ya Gileadi. Hata vile tulikubali kuenda ku Beteli. Wakati tulifika tulimuuliza hivi ndugu Kenneth Little, mwenye alikuwa mu Halmashauri ya Tawi: “Kama banatualika ku Gileadi tutafanya nini?” Alitujibu hivi: “Tutafikiria ile jambo kama munaalikwa.”

Kisha juma moya wakati ya kufikiria ile jambo ilifika. Miye na Debbie tulialikwa ku Masomo ya Gileadi. Kwa hiyo tulipaswa kuamua ikiwa tutabakia ku Beteli ao tutaenda ku masomo. Ndugu Little alituambia hivi: “Uamuzi wowote wenye mutakamata ni wa muzuri. Ikuwe mutachagua nini, Yehova atabariki.” Kwa hiyo tulikubali mwaliko ya kuenda Gileadi. Kisha miaka tulifikia kuelewa kama shauri ya ndugu Little ilikuwa ya kweli. Na siye tunaambiaka bengine ileile maneno wakati banapaswa kuamua kati ya migao mbili mu kazi ya Yehova.

MAISHA YA UMISIONERE

(Kushoto) Ulysses Glass

(Kuume) Jack Redford

Tulikuwa kati ya banafunzi 24 benye balisoma darasa ya 83 ya Masomo ya Gileadi. Tulianza masomo mu Mwezi wa 4, 1987 mu Brooklyn, New York. Ndugu Ulysses Glass na Jack Redford balikuwa baalimu yetu. Miezi tano ilipita mbio. Tarehe 6, Mwezi wa 9, 1987 tulipewa diplome. Balitutuma Haiti, pamoya na John na Marie Goode.

Franco na Debbie mu mahubiri pembeni ya bahari mu Haiti.

Tuko Haiti, 1988

Balifukuzaka bamisionere benye balikuwaka Haiti mu 1962, na tangu ile mwaka tengenezo ilikuwa haiyatumaka tena bamisionere bengine mu ile inchi. Majuma tatu kisha kumaliza masomo ya Gileadi tulifika Haiti, tukaanza kutumikia mu eneo ya milima mu kutaniko ya kidogo ya bahubiri 35. Tulikuwa vijana, tulikuwa na mambo mingi ya kujifunza, na tulikuwa naishi siye peke mu nyumba ya bamisionere. Batu ya mu ile eneo balikuwa maskini na bamingi habakujua kusoma. Wakati tulikuwa kule kulitokea mivurugo juu ya mambo ya politike. Batu balijaribu kunyanganya serikali mamlaka na kulikuwa maandamano. Wakati tulikuwa kule kulitokea pia upepo mukali.

Bandugu na dada ba Haiti balikuwa na furaha na balikuwa na uvumilivu. Mufano wao ulitufundisha mambo mingi. Bamingi balikuwa na maisha ya nguvu lakini balimupenda Yehova na balipenda mahubiri. Dada moya wa kuzeeka hakukuwa najua kusoma lakini alijua mu kichwa maandiko karibu 150. Kuona namna batu balikuwa na maisha ya nguvu kulituchochea tuendelee kubahubiria habari njema ya Ufalme, juu ni Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza magumu yote ya banadamu. Tunafurahi juu batu fulani benye tulijifunzaka nabo ile wakati balifikia kuwa mapainia wa kawaida, mapainia wa pekee na Wazee.

Wakati nilikuwa Haiti, nilikutana na Trevor, kijana mwenye alikuwa misionere wa Bamormoni. Tulizungumuza naye juu ya Biblia zaidi ya mara moya. Kisha miaka fulani aliniandikia barua. Mu ile barua alisema hivi: “Nitabatizwa ku mukusanyiko yenye iko nakuya! Napenda nirudie Haiti na nikuwe painia wa pekee mu ileile eneo yenye nilikuwaka misionere wa Bamormoni.” Na ni vile alifanya kwa miaka mingi pamoya na bibi yake.

ULAYA KISHA AFRIKA

Franco iko natumika mu biro.

Natumikia Slovenia, 1994

Balitutuma mu eneo ya Ulaya kwenye ilianza kuwa mwepesi kuhubiri. Mu 1992 tulifika Ljubljana, Slovenia, karibu na kwenye bazazi yangu balikomaliaka mbele bahamie Italia. Kulikuwaka kungali vita mu maeneo ya Yugoslavia ya zamani. Tawi ya Vienna, mu inchi ya Autriche, tawi ya Zagreb mu inchi za Kroasia, na tawi ya Belgrade mu inchi ya Serbia, njo ilikuwa nasimamia kazi mu eneo ya Yugoslavia ya zamani. Sasa kila inchi ilipaswa kuwa na biro yake ya tawi.

Wakati tulihamia Serbia, iliomba tujifunze luga ya mupya na desturi ya mupya. Batu ya kule balikuwa nasema, “Jezik je težek,” maana yake “luga iko nguvu.” Na kweli, luga yabo ilikuwa nguvu! Tulifurahia ushikamanifu wa ndugu wa kule wenye walikuwa tayari kukubali mabadiliko yenye tengenezo ilifanya, na tuliona namna Yehova alibabariki. Tulijionea tena namna Yehova anarekebishaka mambo kwa upendo na kwa wakati wenye kufaa. Mambo yenye tulikuwa tulishajifunza ilitusaidia kuvumilia magumu yenye tulipata kule, lakini tulijifunza mambo ingine ya maana wakati tulikuwa kule.

Lakini mabadiliko ingine ilikuwa natungoya. Mu 2000 tulitumwa Côte d’Ivoire, mu Afrika ya mangaribi. Kisha, kwa sababu ya vita ya wenyewe kwa wenyewe, mu Mwezi wa 11, 2002, tulilazimika kutoka Côte d’Ivoire na kuenda Sierra Leone. Mu Sierra Leone, vita ya wenyewe kwa wenyewe yenye ilifanya miaka 11 ilikuwa tu inamalizika. Haikukuwa mwepesi kutoka mu Côte d’Ivoire haraka-haraka vile. Lakini mambo yenye tulikuwa tumejifunza ilitusaidia tuendelee kuwa na furaha.

Tulikazia akili matokeo ya muzuri yenye tulipata mu mahubiri, na tulifurahia bandugu na dada benye upendo benye balivumilia vita kwa miaka mingi. Balikuwa maskini lakini balichangia na bengine kidogo yenye balikuwa nayo. Dada moya alipatia Debbie manguo. Wakati Debbie alitaka kukatala, ule dada alimuomba aitike. Alimuambia hivi: “Wakati ya vita bandugu ba mu mainchi ingine balitusaidia, na siye hii ni wakati yetu ya kusaidia bengine.” Tulijiambia kama na siye tutafuata mufano yao.

Kisha wakati tulirudia Côte d’Ivoire, lakini kulitokea tena fujo kwa sababu ya mambo ya politike. Kwa hiyo, mu Mwezi wa 11, 2004, balitutosha mu ile inchi na elikoptere, na kila mutu alibeba tu sakoshi moya ya kilo 10. Tulilala chini mu kambi ya maaskari Wafaransa na siku ya kufuata tulipelekwa Uswisi. Tulifika katikati ya busiku, na bandugu ya mu Halmashauri ya Tawi na baalimu ba Shule ya Mazoezi ya Kihuduma pamoya na babibi yabo balitukaribisha na kutukumbatia. Bakatupatia chakula ya moto na chocolat za mingi. Ile ilitugusa sana.

Ku Jumba ya Ufalme mu Côte d’Ivoire, Franco iko ku jukwaa anatoa hotuba.

Niko natolea bakimbizi hotuba mu Côte d’Ivoire, 2005

Balitutuma kwa wakati fulani Ghana na tulirudia Côte d’Ivoire kisha fujo kupunguka. Haikukuwa mwepesi kuhama na kubadilisha mugawo kila wakati. Lakini tuliweza kuvumilia juu bandugu balituonyesha upendo. Miye na Debbie tunajua kama ni jambo ya kawaida kwa batu ya Mungu kuonyeshana upendo, lakini tuliamua kama tunapaswa kuendelea kukamata ile jambo kwa uzito. Kwa kweli, hata mu vile vipindi vya nguvu, tulijifunza mambo ya maana sana.

MASHARIKI YA KATI

Franco na Debbie banatembelea mabomoko ya zamani mu Mashariki ya Kati.

Tuko Mashariki ya Kati, 2007

Mu 2006 tulipata barua kutoka ku makao makubwa yenye ilitujulisha kama mugao wetu wa mupya itakuwa mu Mashariki ya Kati. Tena tungekutana na mambo ya mupya na matatizo ingine. Iliomba tena tujifunze luga na desturi ya mupya. Tulikuwa na mambo mingi ya kujifunza mu ile eneo yenye ilikuwa na matatizo ya mingi kwa sababu ya mambo ya politike na mambo ya dini. Tulifurahia kuona vile mu makutaniko mulikuwa ndugu na dada wa desturi na luga mbalimbali, na tuliona namna balikuwa na umoja juu balifuata muongozo wa tengenezo. Kwa uhodari, bandugu na dada ba mingi balivumilia upinzani kutoka kwa batu ya familia, banafunzi benzabo, bafanyakazi benzabo, na majirani. Ile ilitugusa sana moyo.

Mu 2012 tulihuzuria mukusanyiko wa pekee mu Tel Aviv, Israeli. Ilikuwa mara ya kwanza batu ba Yehova ba mu ile eneo banakusanyika ba mingi vile tangu Pentekoste ya mwaka wa 33. Hatuwezi kusaabu ule mukusanyiko!

Mu ile miaka, balitutuma tutembelee inchi fulani kwenye kazi yetu ilikuwa imetiliwa vizuizi. Tulienda na vichapo fulani, tulihubiri, na tulifanya mikusanyiko ya kidogo-kidogo. Maaskari walikuwa na silaha za mingi na ma barrière ilikuwa fasi yote. Lakini tulijisikia salama wakati tulikuwa napita wale maaskari juu tulikuwa pamoya na bahubiri fulani na tulikuwa baangalifu.

TUNARUDIA AFRIKA

Franco iko naandika ku ordinatere.

Niko natayarisha hotuba mu Congo, 2014

Mu 2013 tulipewa mugao wa mupya. Tulitumwa ku tawi ya Congo Kinshasa. Congo ni inchi kubwa yenye kupendeza lakini batu mingi ni maskini na mara mingi kumekuwa vita. Ku mwanzo tulisema, “Tunajua vile maisha inakuwaka mu Afrika; tuko tayari.” Lakini tulikuwa tungali na mambo mingi ya kujifunza, zaidi sana wakati iliomba tusafiri mu mabarabara ya mubaya sana. Tulijionea mambo mingi ya muzuri yenye tulipaswa kukazia akili. Kwa mufano, tuliona namna bandugu baliendelea kuvumilia na kuwa na furaha hata kama balikuwa na magumu ya kupata makuta, namna balipenda sana kazi ya kuhubiri, na namna balijikaza sana kuenda ku mikutano na ku mikusanyiko. Tulijionea namna, kwa musaada wa Yehova na baraka yake, batu mingi balikuwa nakubali kweli. Mu miaka yenye tulitumikia Congo Kinshasa, tulijifunza mambo mingi ya maana na tulipata barafiki benye bamekuwa sawa batu ya familia yetu.

Franco iko mu mahubiri, biko naenda mu kijiji pamoya na bandugu na dada.

Mu mahubiri Afrika ya Kusini, 2023

Mu 2017, Tulipata mugao wa mupya. Tulitumwa Afrika ya Kusini. Ilikuwa mara yetu ya kwanza kutumikia mu Beteli ya munene vile, na balitupatia kazi yenye tulikuwa hatuyafanyaka. Tena, tulikuwa na mambo mingi ya kujifunza. Lakini mambo yenye tulijifunzaka zamani ilitusaidia sana. Tunapenda sana bale bandugu na dada ba mingi benye bamevumilia kwa miaka mingi. Na inafurahisha kuona namna familia ya Beteli inatumika kwa umoja hata kama kuko batu ya rangi na desturi tofauti-tofauti. Ni wazi kama Yehova iko nabariki batu yake kwa kubapatia amani juu biko najikaza kuvala utu mupya na kutumikisha kanuni za Biblia.

Mu miaka mingi yenye imepita, miye na Debbie tumepata migao mingi ya kufurahisha, tumejifunza kuzoea desturi za mupya na tumejifunza luga za mupya. Wakati fulani mambo haikukuwa mwepesi, lakini kila wakati Yehova ametuonyesha upendo wake mushikamanifu kupitia ndugu na dada na tengenezo yake. (Zb. 144:2) Tuko hakika kama mambo yenye tumejifunza mu utumishi wa wakati wote imetusaidia tukuwe watumishi wazuri zaidi wa Yehova.

Niko mwenye shukrani sana juu ya namna bazazi yangu balinifundisha, namna bibi yangu Debbie amenitegemeza, na juu ya mambo yenye nimejifunza kupitia mufano wa bandugu na dada ba mu dunia yote. Hata mu siku zenye zitakuya, miye na bibi yangu tunaazimia kuendelea kujifunza mambo mingi zaidi kutoka kwa Mufundishaji wetu Mukubwa

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine