JenkoAtaman/stock.adobe.com
MUENDELEE KUKESHA!
Juu ya Nini Tunapaswa Kuwa na Mawazo ya Muzuri mu 2023—Biblia Inasema Nini?
Tuko sasa mu mwaka wa 2023. Siye wote tunatumainia kama mambo itakuwa muzuri kwetu na kwa familia zetu. Juu ya nini tunapaswa kuwa na mawazo ya muzuri juu ya wakati wenye kuya?
Biblia inatupatia tumaini
Mu Biblia muko habari njema yenye inaonyesha kama magumu yenye tuko napata leo ni ya wakati mufupi na kama hivi karibuni itaisha. Kusema kweli, Biblia ‘iliandikwa ili kutufundisha, ili kupitia. . . faraja kutoka katika Maandiko tukuwe na tumaini.’—Waroma 15:4.
Juu ya kujua mambo mingi zaidi juu ya ahadi zenye kuwa mu Biblia, ona habari “Tumaini Bora la Wakati Ujao.”
Tumaini yenye inaweza kukusaidia sasa
Tumaini yenye kuwa mu Biblia inaweza kuwa sawa vile “nanga ya uzima wetu.” (Waebrania 6:19, maelezo ya chini) Ile tumaini inaweza kufanya tutulie, tuvumilie magumu yenye tuko napata leo, tukuwe na mawazo ya muzuri, na inaweza kutusaidia tupate furaha yenye haina mwisho. Kwa mufano:
Ona namna tumaini yenye kuwa mu Biblia ilisaidia mwanaume moya mwenye alikuwa mutumwa wa tabia fulani ya mubaya. Uangalie video Maisha Yangu Yalinichokesha.
Ona namna tumaini yenye kuwa mu Biblia inaweza kutusadia wakati mutu mwenye tunapenda anakufa. Uangalie video Faraja kwa Wenye Kufiwa.
Tia nguvu tumaini yako
Watu wengi wanatazamia kama mambo ya muzuri itafanyika, lakini hawako hakika kabisa kama itafanyika. Tumaini yenye kuwa mu Biblia iko tofauti. Juu ya nini? Juu ahadi zenye kuwa mu Biblia zinatoka kwa Yehova Mungua, “mwenye hawezi kusema uongo.” (Tito 1:2) Ni Yehova tu njo mwenye kuwa na nguvu ya kutimiza ahadi zake zote; anaweza kufanya “kila kitu chenye anapenda kufanya.”—Zaburi 135:5, 6.
Tunakutia moyo ufaidike na tumaini yenye kutegemeka yenye kuwa mu Biblia. Unaweza kutia nguvu tumaini yako kwa ‘kuchunguza Maandiko kwa uangalifu.’ (Matendo 17:11) Juu ya kujua namna ya kufanya vile, omba mutu fulani akufundishe Biblia bila kulipa. Uanze mwaka wa 2023 na mawazo ya muzuri juu ya wakati wenye kuya!
a Yehova njo jina ya pekee ya Mungu.—Zaburi 83:18.