Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 46
  • Je, Shetani Iko Kabisa?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Shetani Iko Kabisa?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu la Biblia
  • Mawazo ya uongo kuhusu Shetani
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Shetani
    Amuka!—2013
  • Maulizo juu ya habari za Biblia yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Ona Habari Zaidi
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 46

Je, Shetani Iko Kabisa?

Jibu la Biblia

Ndiyo, Shetani iko kabisa. Biblia inasema kwamba yeye ni ‘mutawala wa ulimwengu huu,’ kiumbe cha kiroho aliyejifanya muovu na kumuasi Mungu. (Yohana 14:30; Waefeso 6:11, 12) Biblia inamufunua waziwazi kupitia majina fulani na maana ya majina hayo:

  • Shetani, jina linalomaanisha “Mupingaji.”—Ayubu 1:6.

  • Ibilisi, jina linalomaanisha “Musingiziaji.”—Ufunuo 12:9.

  • Nyoka, jina linalotumiwa katika Biblia ili kumaanisha “Mujanja.”—2 Wakorintho 11:3.

  • Mwenye kujaribu.—Mathayo 4:3.

  • Muongo.—Yohana 8:44

Shetani si kanuni fulani ao tabia fulani ya ubaya

Watu fulani wanafikiri kwamba Shetani Ibilisi ni kanuni fulani tu ao tabia fulani mbaya inayopatikana ndani yetu. Lakini, Biblia inazungumuzia mazungumuzo kati ya Mungu na Shetani. Mungu ni mukamilifu, kwa hiyo haingewezekana azungumuze na sehemu moja ya ubaya iliyo ndani mwake. (Kumbukumbu 32:4; Ayubu 2:1-6) Pia, Shetani alimujaribu Yesu, ambaye hana zambi. (Mathayo 4:8-10; 1 Yohana 3:5) Kwa hiyo, Biblia inaonyesha kwamba Shetani iko kabisa wala si ubaya tu ulio katika wanadamu.

Watu wengi hawaamini kwamba Shetani iko, je, hilo litushangaze? Hapana, kwa kuwa Biblia inasema kwamba Shetani anatumia ujanja ili kutimiza makusudi yake. (2 Wathesalonike 2:9, 10) Ujanja anaotumia sana ni ule wa kupofusha watu ili wasiamini kwamba yeye iko.—2 Wakorintho 4:4.

Mawazo ya uongo kuhusu Shetani

Wazo la kutunga: Lusifero ni jina lingine la Shetani.

Ukweli ni kwamba: Neno la Kiebrania ambalo Biblia fulani zinatafsiri kuwa “Lusifero” linamaanisha “mwenye kungaa.” (Isaya 14:12) Maandiko yanayozunguka andiko hilo yanazungumuzia wafalme wa Babiloni, ambao Mungu alinyenyekeza kwa sababu ya kiburi chao. (Isaya 14:4, 13-20) Maneno “mwenye kungaa” yalitumiwa ili kuchekelea mufalme wa Babiloni kisha kuanguka kwake.

Ukweli ni kwamba: Shetani si mutumishi wa Mungu, lakini adui wake. Shetani Ibilisi anapinga watumishi wa Mungu na kuwasingizia.​—1 Petro 5:8; Ufunuo 12:10.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine