Maelezo ya Chini
b Tafsiri ya Biblia ya Septante inasema Yona alikuwa anakoroma ili kuonyesha kwamba alikuwa mwenye kulala fofofo. Hata hivyo, hatupaswe kuwaza mara moja kwamba alifanya hivyo kwa sababu hakuwa mwenye kuhangaikia wengine; tunapaswa kukumbuka kwamba wakati mwengine watu wanaovunjika moyo wanapatwa na usingizi muzito. Wakati Yesu alikuwa na uchungu mwingi katika bustani ya Gethsemane, Petro, Yakobo, na Yohana walikuwa wenye ‘kusinzia kwa huzuni.’—Lu. 22:45.