Maelezo ya Chini
a Vitabu vya Injili na vitabu vingine vya Biblia vinazungumuzia wakati mbalimbali wenye Yesu alitokea batu kisha kufufuliwa kwake. Kwa mufano, alitokea Maria Magdalene (Yoh. 20:11-18); alitokea banamuke bengine (Mt. 28:8-10; Lu. 24:8-11); alitokea banafunzi 2 (Lu. 24:13-15); alitokea Petro (Lu. 24:34); alitokea mitume kutosha tu Tomasi (Yoh. 20:19-24); alitokea mitume na Tomasi naye alikuwa (Yoh. 20:26); alitokea banafunzi 7 (Yoh. 21:1, 2); alitokea banafunzi zaidi ya 500 (Mt. 28:16; 1 Ko. 15:6); alitokea ndugu yake Yakobo (1 Ko. 15:7); alitokea mitume wote (Mdo. 1:4); na alitokea mitume karibu na Betania. (Lu. 24:50-52) Pengine Biblia haizungumuzie mara zingine zenye Yesu alitokea batu.—Yoh. 21:25.