Waamuzi
5 Siku hiyo Debora+ pamoja na Baraka+ mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu:+
2 “Kwa sababu ya kuacha nywele bila kuzifunga* katika Israeli,
Kwa sababu watu wamejitolea,+
Mumusifu Yehova!
3 Musikilize, ninyi wafalme! Mutege sikio, ninyi watawala!
Nitamuimbia Yehova.
Nitamuimbia Yehova sifa,*+ Mungu wa Israeli.+
4 Yehova, wakati ulitoka Seiri,+
Wakati ulipiga mwendo kutoka eneo la Edomu,
Dunia ilitikisika, na mbingu zikamwanga maji,
Mawingu pia yakamwanga maji.
6 Katika siku za Shamgari+ mwana wa Anati,
Katika siku za Yaeli,+ barabara hazikukuwa na watu;
Wenye kusafiri walipita katika barabara za kidogo-kidogo.
7 Wakaaji wa vijiji vya Israeli hawakukuwa tena;
Hawakukuwa mupaka wakati mimi, Debora,+ nilitokea,
Mupaka wakati nilitokea kama mama katika Israeli.+
Hakuna ngao yenye ilionekana, wala mukuki,
Kati ya elfu makumi ine (40 000) katika Israeli.
Mumusifu Yehova!
10 Ninyi wenye kupanda juu ya punda wa rangi ya kahawa,
Ninyi wenye kukaa juu ya mazulia* ya muzuri,
Na ninyi wenye kutembea katika barabara,
Mufikirie mambo haya!
11 Sauti za watu wenye kugawa maji zilisikiwa mahali pa kushotea maji;
Walikuwa wanazungumuzia pale matendo yenye haki ya Yehova,
Matendo yenye haki ya wakaaji wake wa vijiji katika Israeli.
Kisha watu wa Yehova wakaenda kwenye milango mikubwa.
12 Amuka, amuka, Ee Debora!+
Amuka, amuka, imba wimbo!+
Simama, Baraka!+ Chukua watu wako wenye walikamatwa mateka, wewe mwana wa Abinoamu!
13 Basi wenye waliokoka wakashuka kuenda kwa watu wenye vyeo;
Watu wa Yehova wakashuka kuja kwangu ili kupigana na wanaume wenye nguvu.
14 Walitoka Efraimu, wale wenye kuwa katika bonde;*
Wanakufuata, Ee Benyamini, kati ya vikundi vyako vya watu.
Kutoka Makiri+ makamanda walishuka,
Na kutoka Zabuloni wale wenye kubeba fimbo ya wale wenye kuandika watu katika jeshi.*
15 Wakubwa wa Isakari walikuwa pamoja na Debora,
Kama vile Isakari alikuwa, ni vile pia Baraka alikuwa.+
Alitumwa kwa miguu katika bonde tambarare.*+
Kati ya vikundi vya Rubeni kulikuwa uchunguzi mukubwa wa moyo.
16 Sababu gani ulikaa katikati ya mifuko mbili yenye kuwekwa juu ya mugongo wa munyama wa mizigo,
Ukiwasikiliza wakipigia makundi zumari?+
Kwa maana watu walisita-sita sana kwa ajili ya vikundi vya Rubeni.
18 Zabuloni ni kikundi cha watu wenye walitia maisha yao katika hatari karibu kufa;*
19 Wafalme walikuja, wakapigana vita;
Wafalme wa Kanaani walipigana vita+
Kule Taanaki, pembeni ya maji ya Megido.+
Hawakuchukua feza yoyote katika vita.+
20 Nyota zilipigana zikiwa mbinguni;
Zikiwa katika njia zake za muzunguko zilipigana na Sisera.
Ulikanyanga wenye nguvu, Ee nafsi* yangu.
22 Kisha kwato* za farasi zilikanyanga kwa kishindo
Kwa sababu farasi-dume wake walikimbia mbio sana.+
23 ‘Mulaani Merozi,’ ni vile malaika wa Yehova alisema,
‘Ndiyo, mulaani wakaaji wake,
Kwa sababu hawakukuja kumusaidia Yehova,
Kumusaidia Yehova pamoja na wanaume wenye nguvu.’
24 Yaeli amebarikiwa zaidi ya wanamuke wote+
Bibi ya Heberi+ Mukeni;
Amebarikiwa zaidi ya wanamuke wote wenye kukaa katika mahema.
25 Aliomba maji; akamupatia maziwa.
Alimupatia maziwa ya kuganda katika bakuli kubwa la karamu.+
26 Alinyoosha mukono wake akakamata musumari wa hema,
Na kwa mukono wake wa kuume alikamata nyundo* ya fundi.
27 Aliporomoka katikati ya miguu yake; alianguka na kulala kimya;
Aliporomoka katikati ya miguu yake na kuanguka;
Pale aliporomokea, ni pale aliangukia akiwa ameshindwa.
28 Kupitia dirisha mwanamuke aliangalia inje,
Mama ya Sisera aliangalia kupitia kayungio ya dirisha,
‘Sababu gani gari lake limechelewa kuja?
Sababu gani vishindo vya kwato za magari yake vimechelewa sana?’+
29 Wenye hekima zaidi kati ya wanamuke wake wenye vyeo walimujibu;
Ndiyo, yeye pia alikuwa anajiambia mwenyewe,
30 ‘Wanapaswa kuwa wanagawana vitu vyenye walichukua katika vita,
Mutoto mumoja mwanamuke,* watoto wawili wanamuke,* kwa kila mupiganaji-vita,
Nguo yenye ilichukuliwa katika vita na yenye kutiwa rangi kwa ajili ya Sisera, nguo yenye ilichukuliwa katika vita na yenye kutiwa rangi,
Nguo yenye michoro ya uzi imeshonewa juu yake, nguo yenye ilitiwa rangi, nguo mbili zenye michoro ya uzi imeshonewa juu yazo
Kwa ajili ya shingo za wanyanganyi.’
31 Na maadui wako wote waangamie vile,+ Ee Yehova,
Lakini wenye kukupenda wangae kama jua wakati linatokea katika utukufu wake.”
Na inchi ikapata pumuziko kwa miaka makumi ine (40).+