Waamuzi
7 Kisha Yerubaali, ni kusema, Gideoni,+ na watu wote wenye walikuwa pamoja naye wakaamuka asubui sana na kupiga kambi karibu na Chemchemi ya Harodi, na kambi ya Midiani ilikuwa upande wa kaskazini wa kambi ya Gideoni kwenye kilima cha More katika bonde tambarare.* 2 Yehova akamuambia Gideoni: “Watu wenye uko nao ni wengi sana ili nitie Midiani katika mukono wao.+ Nikifanya vile, Israeli wanaweza kujisifu na kuniambia, ‘Mukono wangu mwenyewe ndio uliniokoa.’+ 3 Na sasa tafazali, tangaza mbele ya watu: ‘Kila mutu mwenye kuogopa na kutetemeka, arudie nyumbani.’”+ Basi Gideoni akawajaribu. Kwa hiyo, watu elfu makumi mbili na mbili (22 000) wakarudia nyumbani, na watu elfu kumi (10 000) wakabakia.
4 Lakini Yehova akamuambia Gideoni: “Watu hao wangali wengi sana. Uwateremushe kwenye maji ili niwajaribu kule kwa ajili yako. Wakati nitakuambia, ‘Huyu ataenda pamoja na wewe,’ basi ataenda pamoja na wewe, lakini wakati nitakuambia, ‘Huyu hataenda pamoja na wewe,’ basi hataenda.” 5 Kwa hiyo Gideoni akateremusha watu kwenye maji.
Kisha Yehova akamuambia Gideoni: “Tia pembeni kila mutu mwenye analambula maji kwa ulimi wake kama vile imbwa analambula, na watu wenye wanapiga magoti ili kunywa maji.” 6 Hesabu ya wale wenye wanalambula maji, wakipandisha mukono wao kwenye kinywa chao, ilikuwa wanaume mia tatu (300). Wengine wote walipiga magoti ili kunywa maji.
7 Yehova akamuambia Gideoni: “Nitakuokoa kupitia wanaume hawa mia tatu (300) wenye walikunywa maji kwa ulimi wao, na nitatia Midiani katika mukono wako.+ Lakini acha wale wengine warudie nyumbani.” 8 Kwa hiyo wakakamata vyakula na baragumu kutoka kwa watu, akarudisha wanaume wengine wote wa Israeli nyumbani, na akabakia na wale wanaume mia tatu (300) tu. Kambi ya Midiani ilikuwa chini ya kambi ya Gideoni katika bonde tambarare.+
9 Usiku huo, Yehova akamuambia: “Simama, shambulia kambi, kwa maana nimeitia katika mukono wako.+ 10 Lakini ikiwa unaogopa kuishambulia, teremuka kwenye kambi pamoja na Pura mutumishi wako. 11 Sikiliza mambo yenye wanasema, na kisha utapata uhodari wa* kushambulia kambi.” Basi yeye na Pura mutumishi wake wakateremuka mupaka kwenye mwisho wa jeshi lenye kupiga kambi.
12 Sasa Wamidiani na Waamaleki na watu wote wa Mashariki+ walikuwa wamejaa katika bonde tambarare na walikuwa wengi kama kundi la nzige, na ngamia wao walikuwa bila hesabu,+ wengi kama chembe za muchanga pembeni ya bahari. 13 Basi Gideoni akakuja, na mutu fulani alikuwa anamuelezea mwenzake ndoto yake, kwa kusema: “Hii ndiyo ndoto yenye niliota. Kulikuwa mukate wa shayiri wa muviringo wenye ulikuwa unaenda ukizunguka-zunguka mupaka ndani ya kambi ya Midiani. Ulifika kwenye hema na kuipiga kwa nguvu sana na hema hiyo ikaanguka.+ Ndiyo, ulipindua hema hiyo, na ikaanguka chini.” 14 Basi mwenzake akasema: “Bila shaka huo ni upanga wa Gideoni+ mwana wa Yoashi, mwanaume wa Israeli. Mungu ametia Midiani na kambi yote katika mukono wake.”+
15 Wakati tu Gideoni alimusikia akieleza ndoto hiyo na mafasirio yake,+ akainama ili kuabudu. Kisha akarudia katika kambi ya Israeli na kusema: “Musimame, kwa maana Yehova ametia kambi ya Midiani katika mukono wenu.” 16 Kisha akagawa wale wanaume mia tatu (300) katika vikundi tatu (3) na kuwapatia wote baragumu+ na mitungi mikubwa yenye kuwa wazi pamoja na mienge ndani ya mitungi hiyo. 17 Kisha akawaambia: “Muniangalie na mufanye sawasawa na vile nitafanya. Wakati nitafika kwenye mwisho wa kambi, mufanye kama vile nitafanya. 18 Wakati nitapiga baragumu, mimi na wote wenye kuwa pamoja na mimi, ninyi pia munapaswa kupiga baragumu kuzunguka kambi pande zote na kusema kwa sauti kubwa, ‘Kwa ajili ya Yehova na kwa ajili ya Gideoni!’”
19 Gideoni na wale wanaume mia moja (100) wenye walikuwa pamoja naye wakakuja kwenye mwisho wa kambi kwenye mwanzo wa kesha la katikati ya usiku,* kisha tu walinzi kuwekwa. Wakapiga zile baragumu+ na kuvunja-vunja ile mitungi mikubwa ya maji yenye ilikuwa katika mikono yao.+ 20 Basi vile vikundi tatu (3) vikapiga zile baragumu na kuvunja-vunja ile mitungi mikubwa. Wakashika mienge kwa mikono yao ya kushoto na zile baragumu kwa mikono yao ya kuume na kuzipiga, na walisema kwa sauti kubwa: “Upanga wa Yehova na wa Gideoni!” 21 Wakati huo wote kila mutu alisimama mahali pake kuzunguka ile kambi pande zote, na jeshi lote likakimbia, likafanya makelele wakati lilikuwa linakimbia.+ 22 Na wale mia tatu (300) wakaendelea kupiga baragumu, na Yehova akafanya watu waanze kuuana kwa upanga kila mutu na mwenzake katika kambi;+ na jeshi likakimbia mupaka Bet-shita, likafika Serera, kufikia kwenye sehemu za pembeni-pembeni ya Abel-mehola+ karibu na Tabati.
23 Na wanaume wa Israeli wakakusanywa pamoja kutoka Naftali, Asheri, na Manase wote,+ na wakafuatilia Midiani. 24 Gideoni akatuma wajumbe katika eneo lote lenye milima la Efraimu, akisema: “Mushuke mushambulie Midiani, na muwazuie wasifike kwenye maji mupaka Bet-bara na Yordani.” Basi watu wote wa Efraimu wakakusanyika pamoja, na wakakamata maji mupaka Bet-bara na Yordani. 25 Pia wakakamata wale wakubwa wawili wa Midiani, Orebu na Zeebu; wakamuua Orebu juu ya mwamba wa Orebu,+ na wakamuua Zeebu kwenye kikamulio cha divai cha Zeebu. Wakaendelea kufuatilia Midiani,+ na wakamuletea Gideoni kichwa cha Orebu na cha Zeebu katika eneo la Yordani.