Waamuzi
1 Kisha kifo cha Yoshua,+ Waisraeli* walimuuliza Yehova:+ “Ni nani kati yetu atapanda kwanza ili kupigana na Wakanaani?” 2 Yehova akajibu: “Yuda atapanda.+ Angalia! Nitatia* inchi hiyo katika mukono wake.” 3 Basi Yuda akamuambia Simeoni ndugu yake: “Panda pamoja na mimi katika eneo lenye nilipewa*+ ili tupigane na Wakanaani. Kisha nitaenda na wewe katika eneo lenye ulipewa.” Basi Simeoni akaenda pamoja naye.
4 Wakati Yuda alipanda, Yehova alitia Wakanaani na Waperizi katika mikono yao,+ wakashinda watu elfu kumi (10 000) katika Bezeki. 5 Wakakuta Adoni-bezeki katika Bezeki, wakapigana naye kule na wakashinda Wakanaani+ na Waperizi.+ 6 Wakati Adoni-bezeki alikimbia, walimufuatilia na kumukamata na wakakata vidole vyake vikubwa vya mikono na vidole vyake vikubwa vya miguu. 7 Kisha Adoni-bezeki akasema: “Kuko wafalme makumi saba (70) wenye walikatwa vidole vikubwa vya mikono na vya miguu na wenye kuokota chakula chini ya meza yangu. Mungu amenilipa kulingana na vile nimefanya.” Kisha wakamupeleka Yerusalemu,+ na akakufia kule.
8 Kisha, wanaume wa Yuda wakapigana na muji wa Yerusalemu+ na kuukamata; wakapiga wakaaji wake kwa upanga na kuteketeza muji huo kwa moto. 9 Kisha, wanaume wa Yuda wakashuka kupigana na Wakanaani wenye walikuwa wanakaa katika eneo lenye milima na katika Negebu na Shefela.+ 10 Basi Yuda akaenda kupigana na Wakanaani wenye walikuwa wanakaa Hebroni (zamani muji wa Hebroni uliitwa Kiriat-arba), na wakamupiga na kumuua Sheshai, Ahimani, na Talmai.+
11 Wakatoka kule na kuenda kupigana na wakaaji wa Debiri.+ (Zamani muji wa Debiri uliitwa Kiriat-seferi.)+ 12 Kisha Kalebu+ akasema: “Mutu mwenye atashambulia na kukamata muji wa Kiriat-seferi, nitamupatia Aksa binti yangu akuwe bibi yake.”+ 13 Na Otnieli+ mwana wa Kenasi,+ ndugu mudogo ya Kalebu, akakamata muji huo. Kwa hiyo Kalebu akamupatia Aksa binti yake akuwe bibi yake. 14 Wakati alikuwa anaenda kwake, akamuchochea bwana yake aombe baba yake* shamba. Kisha akashuka kutoka juu ya punda wake.* Kalebu akamuuliza: “Unataka nini?” 15 Akamuambia: “Tafazali unibariki, kwa maana umenipatia shamba upande wa kusini;* unipatie pia Gulot-maimu.”* Basi Kalebu akamupatia Guloti ya Juu na Guloti ya Chini.
16 Na wazao wa ule Mukeni,+ baba-mukwe wa Musa,+ wakapanda kutoka katika muji wa miti ya mitende+ pamoja na watu wa Yuda na kuenda katika jangwa la Yuda, upande wa kusini wa Aradi.+ Wakaenda kule na kukaa kati ya watu hao.+ 17 Lakini Yuda akaendelea mbele pamoja na Simeoni ndugu yake, na wakashambulia Wakanaani wenye walikuwa wanakaa katika muji wa Sefati na kuuharibu.+ Kwa hiyo wakaita muji huo Horma.*+ 18 Kisha Yuda akakamata Gaza+ na eneo lake, Ashkeloni+ na eneo lake, na Ekroni+ na eneo lake. 19 Yehova alikuwa pamoja na Yuda, na wakakamata eneo lenye milima, lakini hawakuweza kufukuza watu wenye walikuwa wanakaa katika bonde,* kwa sababu walikuwa na magari ya vita yenye miundu ya chuma.*+ 20 Wakamupatia Kalebu Hebroni, kama vile Musa alikuwa ameahidi,+ na akafukuza ndani wale wana watatu wa Anaki.+
21 Lakini Wabenyamini hawakufukuza Wayebusi wenye walikuwa wanakaa Yerusalemu, kwa hiyo Wayebusi wanaendelea kukaa Yerusalemu pamoja na Wabenyamini mupaka leo.+
22 Wakati huohuo, watu wa nyumba ya Yosefu+ wakapanda ili kupigana na Beteli, na Yehova alikuwa pamoja nao.+ 23 Watu wa nyumba ya Yosefu walikuwa wanapeleleza Beteli (zamani muji huo uliitwa Luzi),+ 24 na wapelelezi hao wakaona mwanaume mumoja akitoka katika muji. Wakamuambia: “Tafazali utuonyeshe njia ya kuingia katika muji, na tutakutendea kwa fazili.”* 25 Basi akawaonyesha njia ya kuingia katika muji, kisha wakaua watu wa muji huo kwa upanga, lakini wakamuacha mwanaume huyo pamoja na familia yake yote waende.+ 26 Mwanaume huyo akaenda katika inchi ya Wahiti, akajenga muji na kuuita Luzi. Hilo ndilo jina la muji huo mupaka leo.
27 Manase hakukamata Bet-sheani na miji yake ya pembeni-pembeni,* Taanaki+ na miji yake ya pembeni-pembeni, Dori na miji yake ya pembeni-pembeni, Ibleamu na miji yake ya pembeni-pembeni, na Megido na miji yake ya pembeni-pembeni.+ Wakanaani walikataa kutoka katika inchi hiyo. 28 Wakati Waisraeli walipata nguvu zaidi, walifanyisha Wakanaani kazi ya kulazimishwa,+ lakini hawakuwafukuza kabisa.+
29 Wala Efraimu hakufukuza Wakanaani wenye walikuwa wanakaa Gezeri. Wakanaani waliendelea kukaa kati yao katika Gezeri.+
30 Zabuloni hakufukuza wakaaji wa Kitroni na wakaaji wa Nahaloli.+ Wakanaani waliendelea kukaa kati yao na walifanyishwa kazi ya kulazimishwa.+
31 Asheri hakufukuza wakaaji wa Ako na wakaaji wa Sidoni,+ Alabu, Akzibu,+ Helba, Afiki,+ na Rehobu.+ 32 Basi Waasheri wakaendelea kukaa kati ya Wakanaani wenye walikuwa wanakaa katika inchi, kwa sababu hawakuwafukuza.
33 Naftali hakufukuza wakaaji wa Bet-shemeshi na wakaaji wa Bet-anati,+ lakini waliendelea kukaa kati ya Wakanaani wenye walikuwa wanakaa katika inchi.+ Wakaaji wa Bet-shemeshi na wa Bet-anati wakakuwa wafanyakazi wao wa kulazimishwa.
34 Waamori walizuia Wadani katika eneo lenye milima, kwa maana hawakuwaruhusu kushuka katika bonde.*+ 35 Basi Waamori walikataa kutoka katika Mulima Heresi, Aiyaloni,+ na Shaalbimu.+ Lakini wakati nguvu ya* nyumba ya Yosefu iliongezeka,* waliwafanyisha kazi ya kulazimishwa. 36 Na eneo la Waamori lilikuwa kuanzia mupando wa Akrabimu,+ kuanzia Sela kuenda juu.