Waamuzi
19 Katika siku hizo, wakati hapakukuwa mufalme katika Israeli,+ Mulawi mumoja mwenye alikuwa anaishi katika sehemu ya mbali ya eneo lenye milima la Efraimu+ alichukua suria* mumoja wa Betlehemu+ katika Yuda akuwe bibi yake. 2 Lakini suria* wake hakukuwa muaminifu kwake, akamuacha na kuenda kwenye nyumba ya baba yake kule Betlehemu katika Yuda. Akabakia kule miezi ine (4). 3 Kisha bwana yake akamufuata ili kumushawishi arudie; alikuwa na mutumishi wake mwanaume na punda wawili. Basi suria* huyo akamupeleka katika nyumba ya baba yake. Wakati baba yake alimuona, akafurahi kukutana naye. 4 Basi baba-mukwe wake, baba ya ule kijana mwanamuke, akamushawishi akae pamoja naye siku tatu (3); walikuwa wanakula na kunywa, na alikuwa analala pale usiku.
5 Siku ya ine (4), wakati waliamuka asubui sana ili waende, baba ya ule kijana mwanamuke akamuambia mwana-mukwe wake: “Kula chakula kidogo ili upate nguvu,* na kisha munaweza kuenda.” 6 Basi wakakaa, na wote wawili wakakula na kunywa pamoja; kisha baba ya ule kijana mwanamuke akamuambia huyo mwanaume: “Tafazali, lala hapa usiku na ujifurahishe.”* 7 Wakati mwanaume huyo alisimama ili aende, baba-mukwe wake akaendelea kumuomba abakie, basi akalala tena usiku huo.
8 Wakati aliamuka asubui sana siku ya tano (5) ili aende, baba ya ule kijana mwanamuke akasema: “Tafazali, kula chakula kidogo ili upate nguvu.”* Na wakakawia mupaka mangaribi, na wote wawili wakaendelea kula. 9 Wakati ule mwanaume alisimama ili aende pamoja na suria* wake na mutumishi wake, baba-mukwe wake, baba ya ule kijana mwanamuke, akamuambia: “Angalia, sasa! Mangaribi inakaribia. Tafazali, mulale usiku wote. Muchana unakaribia kuisha. Lala hapa usiku na ujifurahishe. Kesho munaweza kuamuka asubui sana kwa ajili ya safari yenu na kuenda kwenye nyumba* yenu.” 10 Lakini, mwanaume huyo hakutaka kulala usiku mwingine, basi akasimama na kusafiri mupaka Yebusi, ni kusema, Yerusalemu.+ Alikuwa na punda wake wawili wenye kutandikwa, suria* wake, na mutumishi wake.
11 Wakati walikuwa karibu na Yebusi, mwangaza wa muchana ulikuwa umeanza kupotea. Basi ule mutumishi akamuuliza bwana wake: “Tunaweza kuingia katika muji huu wa Wayebusi na kulala ndani usiku?” 12 Lakini bwana wake akamuambia: “Hatupaswe kuingia katika muji wa wageni wenye hawako Waisraeli. Tutaendelea mupaka Gibea.”+ 13 Kisha akamuambia mutumishi wake: “Kuja na tujaribu kufika katika moja la maeneo yale; tutalala usiku katika Gibea ao katika Rama.”+ 14 Kwa hiyo wakaendelea na safari yao, na jua likaanza kushuka wakati walikuwa karibu na Gibea, muji wa Benyamini.
15 Basi wakasimama pale na kuingia ili walale katika Gibea usiku huo. Wakati waliingia ndani, wakakaa katika kiwanja cha watu wote cha muji, lakini hakuna mutu mwenye aliwakaribisha ndani ya nyumba yake ili walale usiku.+ 16 Mwishowe mangaribi hiyo, mwanaume fulani muzee mwenye alikuwa anatoka katika kazi yake ya mashamba akaingia katika muji. Alikuwa wa eneo lenye milima la Efraimu,+ na alikuwa amekaa muda mufupi katika Gibea; lakini wakaaji wa muji huo walikuwa Wabenyamini.+ 17 Wakati aliinua macho na kuona ule musafiri katika kiwanja cha watu wote cha muji, mwanaume huyo muzee akamuuliza: “Unaenda wapi, na unatoka wapi?” 18 Akajibu: “Tunatoka Betlehemu katika Yuda na tunaenda katika sehemu moja ya mbali ya eneo lenye milima la Efraimu; niko wa kule. Nilienda Betlehemu katika Yuda,+ na ninaenda kwenye nyumba ya Yehova,* lakini hakuna mutu ameniingiza katika nyumba yake. 19 Tuko na nyasi na chakula cha kuenea kwa ajili ya punda wetu,+ na mukate+ na divai kwa ajili yangu, mwanamuke huyu, na mutumishi wetu. Hatukose kitu.” 20 Hata hivyo, ule mwanaume muzee akasema: “Ukuwe na amani! Nitawapatia kila kitu chenye muko nacho lazima. Lakini tu usilale katika kiwanja cha watu wote.” 21 Basi akamupeleka katika nyumba yake na kupatia punda hao chakula.* Kisha wakanawa miguu yao, wakakula, na kunywa.
22 Wakati walikuwa wanajifurahisha, watu fulani wa muji wenye hawana mafaa yoyote wakazunguka nyumba na walikuwa wanagonga-gonga mulango, na waliendelea kumuambia ule mwanaume muzee, mwenye nyumba: “Umulete inje ule mwanaume mwenye aliingia katika nyumba yako, ili tufanye ngono naye.”+ 23 Basi mwenye nyumba akatoka inje na kuwaambia: “Hapana, ndugu zangu, musifanye uovu huo. Tafazali, mutu huyu ni mugeni katika nyumba yangu. Musifanye jambo hili la haya sana. 24 Niko hapa na binti yangu bikira na suria* wa mwanaume huyu. Muache niwalete inje, na munaweza kuwafezehesha kama munataka.*+ Lakini hamupaswe kumutendea mwanaume huyu jambo hili la haya sana.”
25 Lakini wanaume hao wakakataa kumusikiliza, basi ule mwanaume akachukua suria* wake+ na kumupeleka inje kwa watu hao. Wakamulala kinguvu na kumutendea mubaya usiku wote mupaka asubui. Kisha wakamuacha aende wakati kulipambazuka.* 26 Asubui sana, mwanamuke huyo akakuja na kuanguka kwenye muingilio wa nyumba ya ule mwanaume mahali bwana wake alikuwa, na akalala pale mupaka wakati kulikuwa mwangaza. 27 Wakati bwana wake aliamuka asubui na kufungua milango ya nyumba ili atoke inje na kuendelea na safari yake, akaona ule mwanamuke, suria* wake, amelala kwenye muingilio wa nyumba na mikono yake ilikuwa juu ya kizingiti.* 28 Basi akamuambia: “Simama; tuende.” Lakini hakujibu kitu. Kwa hiyo mwanaume huyo akamuweka juu ya punda na akaenda kwake.
29 Wakati alifika kwenye nyumba yake, akakamata kisu cha kuchinjia na kumushika suria* wake na kumukata-kata kiungo kwa kiungo vipande kumi na mbili (12) na kupeleka kipande kimoja katika kila eneo la Israeli. 30 Wote wenye waliona jambo hilo wakasema: “Jambo kama hili halijatokeaka ao kuonekana tangu siku Waisraeli walipanda kutoka Misri mupaka leo. Mufikirie jambo hili,* mupatiane mawazo,+ na mutuambie jambo la kufanya.”