Waamuzi
21 Basi watu wa Israeli walikuwa wameapa kiapo hiki kule Mispa:+ “Hakuna mutu kati yetu mwenye atapatia mwanaume wa Benyamini binti yake ili akuwe bibi yake.”+ 2 Kwa hiyo watu wakakuja Beteli+ na wakakaa pale mbele ya Mungu wa kweli mupaka mangaribi, wakapandisha sauti na kulia kwa uchungu. 3 Na walikuwa wanasema: “Ee Yehova Mungu wa Israeli, sababu gani jambo hili limetokea katika Israeli? Sababu gani kabila moja likosekane leo katika Israeli?” 4 Siku yenye ilifuata, watu wakaamuka asubui sana na kujenga mazabahu pale ili kutoa matoleo ya kuteketezwa na matoleo ya ushirika.+
5 Kisha watu wa Israeli wakasema: “Ni nani kati ya makabila yote ya Israeli mwenye hakukuja kukusanyika mbele ya Yehova?” kwa maana walikuwa wamefanya kiapo kikubwa kwamba mutu yeyote mwenye hakukuja Mispa mbele ya Yehova anapaswa kuuawa. 6 Basi watu wa Israeli wakahuzunika kwa sababu ya kile kilimupata Benyamini ndugu yao. Wakasema: “Leo kabila moja limeondolewa katika Israeli. 7 Kwa kuwa tumeapa mbele ya Yehova+ kwamba hatutawapatia mabinti wetu wakuwe bibi zao, tutafanya nini ili kupata bibi kwa ajili ya wale wenye walibakia?”+
8 Wakauliza: “Ni nani kati ya makabila ya Israeli mwenye hakukuja mbele ya Yehova katika Mispa?”+ Ikaonekana kwamba hakuna mutu wa Yabesh-gileadi mwenye alikuja katika kambi mahali kutaniko lilikuwa. 9 Wakati watu walihesabiwa, wakaona kwamba hakuna mukaaji hata mumoja wa Yabesh-gileadi mwenye alikuwa pale. 10 Basi mukusanyiko ukatuma kule wanaume elfu kumi na mbili (12 000) kati ya wanaume wenye nguvu zaidi. Wakawaamuru: “Muende na mupige na kuua wakaaji wa Yabesh-gileadi kwa upanga, muue hata wanamuke na watoto.+ 11 Munapaswa kufanya hivi: Munapaswa kuangamiza kila mwanaume, na pia kila mwanamuke mwenye amekwisha kufanya ngono na mwanaume.” 12 Kati ya wakaaji wa Yabesh-gileadi, walipata watoto wanamuke mia ine (400) wenye walikuwa mabikira, wenye walikuwa hawajafanya ngono na mwanaume hata siku moja. Basi wakawaleta katika kambi kule Shilo,+ yenye kuwa katika inchi ya Kanaani.
13 Kisha mukusanyiko wote ukatuma ujumbe kwa Wabenyamini kwenye mwamba wa Rimoni+ na kuwatakia amani. 14 Basi Wabenyamini wakarudia wakati huo. Wakawapatia wale wanamuke wenye hawakuua kati ya wale wanamuke wa Yabesh-gileadi,+ lakini hawakupata wanamuke wa kuwaenea. 15 Na watu wakahuzunika juu ya kile kilimupata Benyamini+ kwa sababu Yehova alikuwa ameleta mugawanyiko kati ya makabila ya Israeli. 16 Wazee wa mukusanyiko wakasema: “Tutafanya nini ili kupata wanamuke kwa ajili ya wanaume wenye walibakia, kwa kuwa wanamuke wote waliharibiwa katika Benyamini?” 17 Wakajibu: “Kunapaswa kuwa uriti kwa ajili ya watu wa Benyamini wenye waliokoka, ili kabila moja lisifutwe katika Israeli. 18 Lakini haturuhusiwe kuwapatia bibi kati ya mabinti wetu, kwa sababu watu wa Israeli wameapa: ‘Alaaniwe mutu yeyote mwenye anamupatia Mubenyamini bibi.’”+
19 Kisha wakasema: “Angalia! Kuko sikukuu ya Yehova kila mwaka kule Shilo,+ muji wenye kuwa upande wa kaskazini wa Beteli na upande wa mashariki wa barabara kubwa yenye inapanda kuanzia Beteli mupaka Shekemu na upande wa kusini wa Lebona.” 20 Kisha wakaamuru watu wa Benyamini: “Muende na muvizie katika mashamba ya mizabibu. 21 Na wakati mutaona vijana wanamuke* wa Shilo wakitoka ili kucheza dansi za muzunguko, kila mumoja wenu atatoka katika mashamba ya mizabibu na kuchukua bibi kati ya vijana wanamuke wa Shilo, na mutarudia katika inchi ya Benyamini. 22 Na baba zao ao ndugu zao wakikuja kutoa malalamiko juu yetu, tutawaambia, ‘Mutuonyeshe wema kwa kuwasaidia, kwa sababu hatukuweza kupatia kila mumoja wao bibi kupitia vita,+ na kama mungewapatia bibi, mungekuwa na hatia.’”+
23 Basi wale wanaume wa Benyamini wakafanya vile, na kila mumoja akajichukulia bibi kati ya wanamuke wenye walikuwa wanacheza dansi. Kisha wakarudia katika uriti wao na wakajenga tena miji yao+ na kukaa ndani.
24 Na wakati huo Waisraeli wakatoka pale na kusambaa, kila mumoja akaenda kwenye kabila lake na kwenye familia yake, na wakaondoka pale, kila mumoja akaenda kwenye uriti wake.
25 Katika siku hizo hapakukuwa mufalme katika Israeli.+ Kila mutu alikuwa anafanya jambo lenye lilikuwa sawa mbele ya macho yake.*