Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 6
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 1 Samweli

      • Wafilisti wanarudishia Israeli Sanduku (1-21)

1 Samweli 6:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 4:11; 5:1; Zab 78:61

1 Samweli 6:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 18:9, 10; Isa 2:6

1 Samweli 6:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 6:4, 17

1 Samweli 6:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “bawasiri.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 13:2, 3; 1 Sa. 6:16

1 Samweli 6:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “bawasiri.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 6:18
  • +1 Sa. 5:6, 11

1 Samweli 6:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 7:13; 8:15; 14:17
  • +Kut 9:14, 16; Rom. 9:17, 18
  • +Kut 6:1; 11:1; 12:33

1 Samweli 6:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 6:3, 4

1 Samweli 6:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 15:10, 12; 21:8, 16; 2Nya 28:18

1 Samweli 6:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.

1 Samweli 6:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “bawasiri.”

1 Samweli 6:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 6:8, 9

1 Samweli 6:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “eneo tambarare la chini.”

1 Samweli 6:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 6:7

1 Samweli 6:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 3:30, 31
  • +Yosh. 21:8, 16

1 Samweli 6:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “bawasiri.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 6:4
  • +1 Sa. 5:1
  • +1 Sa. 5:8
  • +Amu 1:18; 1 Sa. 5:10

1 Samweli 6:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “watu 70, watu 50 000.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 4:15, 20; 1Nya 13:10

1 Samweli 6:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 11:45
  • +Hes 17:12, 13; 2 Sa. 6:8, 9; Zab 76:7

1 Samweli 6:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 18:14; 1Nya 13:5, 6
  • +1Nya 16:1; 2Nya 1:4

Maandiko ingine

1 Sam. 6:11 Sa. 4:11; 5:1; Zab 78:61
1 Sam. 6:2Kum 18:9, 10; Isa 2:6
1 Sam. 6:31 Sa. 6:4, 17
1 Sam. 6:4Yosh. 13:2, 3; 1 Sa. 6:16
1 Sam. 6:51 Sa. 6:18
1 Sam. 6:51 Sa. 5:6, 11
1 Sam. 6:6Kut 7:13; 8:15; 14:17
1 Sam. 6:6Kut 9:14, 16; Rom. 9:17, 18
1 Sam. 6:6Kut 6:1; 11:1; 12:33
1 Sam. 6:81 Sa. 6:3, 4
1 Sam. 6:9Yosh. 15:10, 12; 21:8, 16; 2Nya 28:18
1 Sam. 6:121 Sa. 6:8, 9
1 Sam. 6:141 Sa. 6:7
1 Sam. 6:15Hes 3:30, 31
1 Sam. 6:15Yosh. 21:8, 16
1 Sam. 6:171 Sa. 6:4
1 Sam. 6:171 Sa. 5:1
1 Sam. 6:171 Sa. 5:8
1 Sam. 6:17Amu 1:18; 1 Sa. 5:10
1 Sam. 6:19Hes 4:15, 20; 1Nya 13:10
1 Sam. 6:20Law. 11:45
1 Sam. 6:20Hes 17:12, 13; 2 Sa. 6:8, 9; Zab 76:7
1 Sam. 6:21Yosh. 18:14; 1Nya 13:5, 6
1 Sam. 6:211Nya 16:1; 2Nya 1:4
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
1 Samweli 6:1-21

Cha Kwanza cha Samweli

6 Sanduku+ la Yehova lilikuwa katika eneo la Wafilisti kwa miezi saba (7). 2 Wafilisti wakaita makuhani na waaguzi+ na kuuliza: “Tufanyie nini Sanduku la Yehova? Mutuambie namna tunapaswa kulirudisha mahali pake.” 3 Wakajibu: “Kama munarudisha sanduku la agano la Yehova, Mungu wa Israeli, musilirudishe bila toleo. Musikose kulirudisha kwake pamoja na toleo la hatia.+ Ni kwa kufanya vile tu ndio mutaponyeshwa, na mutajulishwa sababu gani mukono wake haujatoka juu yenu.” 4 Kwa hiyo wakauliza: “Tunapaswa kumutumia toleo gani la hatia?” Wakasema: “Kulingana na hesabu ya mabwana wa Wafilisti,+ mutume emoroide* tano (5) za zahabu na panya tano wa zahabu, kwa maana kila mumoja wenu pamoja na mabwana wenu wamepatwa na pigo lilelile. 5 Munapaswa kutengeneza sanamu za emoroide* zenu na sanamu za panya wenu+ wenye wanaharibu inchi, na munapaswa kumuheshimia Mungu wa Israeli. Pengine atapunguza uzito wa mukono wake wenye uko juu yenu na juu ya mungu wenu na juu ya inchi yenu.+ 6 Sababu gani mufanye moyo wenu kuwa mugumu kama vile Misri na Farao walifanya mioyo yao kuwa migumu?+ Wakati Yeye aliwatendea kwa ukali,+ walilazimika kuruhusu Israeli waende, nao wakaondoka.+ 7 Sasa mutayarishe gari la mupya la kukokotwa na ngombe wawili wenye wako na vitoto-dume na wenye hawajakuwa hata siku moja chini ya nira. Kisha mufungie ngombe hao kwenye gari hilo, lakini murudishe vitoto-dume hivyo nyumbani, mbali na ngombe hao. 8 Muchukue Sanduku la Yehova na kulitia juu ya gari hilo, na mutie ndani ya sanduku lingine pembeni yake vitu vya zahabu vyenye munamutumia kuwa toleo la hatia.+ Kisha mulitume 9 na muangalie: Kama linapanda kwenye barabara yenye inaelekea Bet-shemeshi,+ kwenye eneo lake, basi yeye ndiye ametutendea uovu huu mukubwa. Lakini kama halipande kule, tutajua kwamba haiko mukono wake ndio ulitupiga; ni jambo lenye lilitokea tu.”

10 Watu hao wakafanya vile. Wakachukua ngombe wawili wenye kuwa na vitoto-dume na wakawafungia kwenye gari hilo, na vitoto-dume vya ngombe hao wakavifungia nyumbani ndani ya zizi.* 11 Kisha wakatia Sanduku la Yehova juu ya gari hilo, pamoja na sanduku lenye panya wa zahabu na sanamu za emoroide* zao. 12 Na ngombe hao wakaenda moja kwa moja kwenye barabara yenye inaelekea Bet-shemeshi.+ Walibakia kwenye barabara hiyo kubwa, na walikuwa wanalia wakati walikuwa wanaenda; hawakugeukia kuume wala kushoto. Wakati huo wote mabwana wa Wafilisti walikuwa wanatembea nyuma yao kufikia kwenye mupaka wa Bet-shemeshi. 13 Watu wa Bet-shemeshi walikuwa wanavuna mavuno ya ngano katika bonde tambarare.* Wakati waliinua macho yao na kuona lile Sanduku, wakashangilia sana kuliona. 14 Gari hilo likafika kwenye shamba la Yoshua Mubet-shemeshi na likasimama pale karibu na jiwe kubwa. Kwa hiyo wakapasua mbao za gari hilo, na wakatoa ngombe hao+ kuwa toleo la kuteketezwa kwa Yehova.

15 Walawi+ wakashusha Sanduku la Yehova na sanduku lenye lilikuwa pamoja nalo, lenye ndani yake mulikuwa vile vitu vya zahabu, na wakavitia juu ya lile jiwe kubwa. Watu wa Bet-shemeshi+ wakamutolea Yehova matoleo ya kuteketezwa na kumufanyia zabihu siku hiyo.

16 Wakati mabwana tano (5) wa Wafilisti waliona hayo, wakarudia Ekroni siku hiyo. 17 Basi hizi ndizo emoroide* za zahabu zenye Wafilisti walimutumia Yehova kuwa toleo la hatia:+ moja kwa ajili ya Ashdodi,+ moja kwa ajili ya Gaza, moja kwa ajili ya Ashkeloni, moja kwa ajili ya Gati,+ moja kwa ajili ya Ekroni.+ 18 Na hesabu ya panya wa zahabu ililingana na hesabu ya miji yote ya Wafilisti yenye ilikuwa ya mabwana tano (5)⁠—​miji yenye ngome na vijiji vya eneo la mashamba.

Na jiwe kubwa lenye waliweka Sanduku la Yehova juu yake ni ushahidi mupaka leo katika shamba la Yoshua Mubet-shemeshi. 19 Lakini Mungu akapiga na kuua watu wa Bet-shemeshi, kwa sababu walikuwa wameangalia Sanduku la Yehova. Alipiga na kuua elfu makumi tano na makumi saba (50 070)* kati ya watu, na watu wakaanza kuomboleza kwa sababu Yehova alikuwa amewapiga na kuwaua kwa mauaji makubwa.+ 20 Kwa hiyo watu wa Bet-shemeshi wakauliza: “Ni nani ataweza kusimama mbele ya Yehova, huyu Mungu mutakatifu,+ na ataenda kwa nani wakati atatoka kwetu?”+ 21 Kwa hiyo wakatuma wajumbe kwa wakaaji wa Kiriat-yearimu,+ na kusema: “Wafilisti wamerudisha Sanduku la Yehova. Mushuke na kupanda nalo.”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine