Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 8
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 1 Samweli

      • Israeli wanaomba mufalme (1-9)

      • Samweli anaonya watu (10-18)

      • Yehova anakubali ombi la kutaka mufalme (19-22)

1 Samweli 8:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 6:28

1 Samweli 8:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kata-midomo.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 18:21
  • +Kut 23:8; Kum 16:19; Zab 15:5; Mez. 29:4
  • +Kum 24:17

1 Samweli 8:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 17:14, 15; 1 Sa. 12:13; Mdo 13:21

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Tuige Imani Yao, uku. 72-73

    Munara wa Mulinzi,

    1/1/2011, uku. 27

1 Samweli 8:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “jambo hilo lilikuwa mubaya katika macho ya Samweli.”

1 Samweli 8:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 8:23; 1 Sa. 10:19; 12:12; Isa 33:22

1 Samweli 8:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 9:24
  • +Amu 2:19

1 Samweli 8:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 10:25
  • +1 Sa. 14:52
  • +1 Fal. 9:22; 10:26
  • +1 Fal. 4:26

1 Samweli 8:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 18:1; 1Nya 27:1
  • +2 Fal. 1:14
  • +1Nya 27:26
  • +1 Fal. 4:7
  • +1 Fal. 4:26

1 Samweli 8:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “watengenezaji wa marashi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 4:22

1 Samweli 8:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 27:28, 31

1 Samweli 8:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 5:15, 16

1 Samweli 8:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 4:22, 23

1 Samweli 8:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 12:3, 4

1 Samweli 8:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 8:7; Ho 13:11

Maandiko ingine

1 Sam. 8:21Nya 6:28
1 Sam. 8:3Kut 18:21
1 Sam. 8:3Kut 23:8; Kum 16:19; Zab 15:5; Mez. 29:4
1 Sam. 8:3Kum 24:17
1 Sam. 8:5Kum 17:14, 15; 1 Sa. 12:13; Mdo 13:21
1 Sam. 8:7Amu 8:23; 1 Sa. 10:19; 12:12; Isa 33:22
1 Sam. 8:8Kum 9:24
1 Sam. 8:8Amu 2:19
1 Sam. 8:111 Sa. 10:25
1 Sam. 8:111 Sa. 14:52
1 Sam. 8:111 Fal. 9:22; 10:26
1 Sam. 8:111 Fal. 4:26
1 Sam. 8:122 Sa. 18:1; 1Nya 27:1
1 Sam. 8:122 Fal. 1:14
1 Sam. 8:121Nya 27:26
1 Sam. 8:121 Fal. 4:7
1 Sam. 8:121 Fal. 4:26
1 Sam. 8:131 Fal. 4:22
1 Sam. 8:141Nya 27:28, 31
1 Sam. 8:161 Fal. 5:15, 16
1 Sam. 8:171 Fal. 4:22, 23
1 Sam. 8:181 Fal. 12:3, 4
1 Sam. 8:221 Sa. 8:7; Ho 13:11
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
1 Samweli 8:1-22

Cha Kwanza cha Samweli

8 Wakati Samweli alikuwa amezeeka, aliweka wana wake kuwa waamuzi wa Israeli. 2 Jina la mwana wake wa kwanza lilikuwa Yoeli, na jina la wa pili, Abiya;+ walikuwa waamuzi katika Beer-sheba. 3 Lakini wana wake hawakutembea katika njia zake; walikuwa na muelekeo wa kufuatilia faida yenye haiko ya haki,+ walipokea rushwa,*+ na walipotosha haki.+

4 Kisha wakati fulani wazee wote wa Israeli walikusanyika pamoja na kuja kumuona Samweli kule Rama. 5 Wakamuambia: “Angalia! Umezeeka, lakini wana wako hawatembee katika njia zako. Sasa uweke mufalme kwa ajili yetu ili atuhukumu kama vile mataifa mengine yote.”+ 6 Lakini Samweli hakufurahi* wakati walisema: “Utupatie mufalme ili atuhukumu.” Kwa hiyo Samweli akasali kwa Yehova, 7 na Yehova akamuambia Samweli: “Sikiliza mambo yote yenye watu wanakuambia; kwa maana haiko wewe ndiye wamekataa, lakini mimi ndiye wamekataa kuwa mufalme wao.+ 8 Wanatenda kama vile wametenda tangu siku niliwatosha Misri mupaka leo; wanaendelea kuniacha+ na kutumikia miungu mingine,+ na ni vile wanakutendea wewe. 9 Sasa uwasikilize. Lakini, unapaswa kuwaonya kwa uzito; uwaambie mambo yenye mufalme mwenye atatawala juu yao atakuwa na haki ya kuomba.”

10 Kwa hiyo Samweli akaambia watu wenye walikuwa wanamuomba awapatie mufalme maneno yote ya Yehova. 11 Akasema: “Mufalme mwenye atatawala juu yenu atakuwa na haki ya kuomba mambo haya:+ Atachukua wana wenu+ na kuwatia katika magari yake+ na kuwafanya wakuwe wapanda-farasi wake,+ na wamoja watalazimika kukimbia mbele ya magari yake. 12 Na atajichagulia wakubwa wa maelfu+ na wakubwa wa makumi tano,+ na wamoja watamulimia mashamba yake,+ watavuna mavuno yake,+ na kutengeneza silaha zake za vita na vyombo vya magari yake.+ 13 Atachukua watoto wenu wanamuke ili wakuwe watu wa kuchanganya mafuta yenye marashi,* wapishi, na watengenezaji wa mikate.+ 14 Atachukua mashamba yenu ya muzuri sana, mashamba yenu ya muzuri sana ya mizabibu,+ na mashamba yenu ya muzuri sana ya mizeituni na kuyapatia watumishi wake. 15 Atakamata sehemu moja ya kumi (1/10) ya mashamba yenu ya mbegu na mashamba yenu ya mizabibu, na ataipatia maofisa wa makao yake na watumishi wake. 16 Na atachukua watumishi wenu wanaume na watumishi wenu wanamuke, wanyama wazuri sana wa mifugo yenu, na punda wenu, na atawatumia kufanya kazi yake.+ 17 Atakamata sehemu moja ya kumi (1/10) ya makundi yenu,+ na mutakuwa watumishi wake. 18 Siku itafika wakati mutalia kwa sababu ya mufalme mwenye mumejichagulia wenyewe,+ lakini Yehova hatawajibu siku hiyo.”

19 Lakini, watu wakakataa kusikiliza mambo yenye Samweli aliwaambia, na wakasema: “Hapana, tumeazimia kuwa na mufalme juu yetu. 20 Kisha tutakuwa kama mataifa mengine yote, na mufalme wetu atatuhukumu na kutuongoza na kupigana vita zetu.” 21 Kisha Samweli kusikia maneno yote ya watu, akayarudilia katika masikio ya Yehova. 22 Yehova akamuambia Samweli: “Uwasikilize, na uweke mufalme atawale juu yao.”+ Basi Samweli akawaambia wanaume wa Israeli: “Kila mumoja wenu arudie katika muji wake.”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine