Cha Kwanza cha Samweli
17 Na Wafilisti+ wakakusanya majeshi yao* kwa ajili ya vita. Walikusanyika kule Soko,+ muji wa Yuda, na walipiga kambi katikati ya Soko na Azeka,+ kule Efes-damimu.+ 2 Sauli na watu wa Israeli wakakusanyika na kupiga kambi katika Bonde* la Ela,+ na wakajipanga kwa ajili ya vita ili kukutana na Wafilisti. 3 Wafilisti walikuwa upande mumoja wa mulima, na Waisraeli walikuwa upande mwingine wa mulima, na bonde lilikuwa katikati yao.
4 Kisha shujaa mumoja akatoka katika kambi za Wafilisti; jina lake lilikuwa Goliati,+ wa muji wa Gati,+ na urefu wake ulikuwa mikono sita (6) na shubiri moja.* 5 Alikuwa na kofia ya shaba juu ya kichwa chake, na alikuwa anavaa koti ya chuma yenye magamba yenye kuingiana-ingiana. Uzito wa koti hiyo ya chuma+ ya shaba ulikuwa shekeli elfu tano (5 000).* 6 Alikuwa na mabamba ya shaba yenye yalilinda miguu yake na mukuki mudogo+ wa shaba ulininginia katikati ya mabega yake. 7 Mupini wa muti wa mukuki wake ulikuwa kama muti wa wasukaji wa nguo,+ na kichwa cha chuma cha mukuki wake kilikuwa na uzito wa shekeli mia sita (600);* na mubeba-ngao wake alitembea mbele yake. 8 Basi akasimama na kuita kikundi cha wapiganaji cha Israeli+ na kuwaambia: “Sababu gani mumekuja kujipanga kwa ajili ya vita? Je, mimi siko Mufilisti, na ninyi je, hamuko watumishi wa Sauli? Mujichagulie mwanaume, na ashuke kuja kwangu. 9 Kama anaweza kupigana na mimi na anipige na kuniua, basi tutakuwa watumishi wenu. Lakini kama ninamushinda na kumupiga na kumuua, mutakuwa watumishi wetu na mutatutumikia.” 10 Kisha Mufilisti huyo akasema: “Ninachokoza* kikundi cha wapiganaji cha Israeli+ leo. Munipatie mwanaume, na tupigane naye!”
11 Wakati Sauli na Israeli wote walisikia maneno hayo ya Mufilisti huyo, wakakuwa na hofu na wakaogopa sana.
12 Sasa Daudi alikuwa mwana wa Mwefrati+ wa muji wa Betlehemu+ wa Yuda mwenye aliitwa Yese,+ mwenye alikuwa na wana munane (8)+ na mwenye alikuwa tayari amezeeka katika siku za Sauli. 13 Wana watatu (3) wakubwa zaidi wa Yese walikuwa wamemufuata Sauli katika vita.+ Majina ya wana wake watatu wenye walienda katika vita yalikuwa Eliabu+ muzaliwa wa kwanza, mwana wake wa pili Abinadabu,+ na wa tatu Shamma.+ 14 Daudi ndiye alikuwa mudogo zaidi,+ na wale watatu (3) wakubwa zaidi walimufuata Sauli.
15 Daudi alikuwa anaenda na kurudia kutoka kwa Sauli ili kuchunga kondoo+ wa baba yake kule Betlehemu. 16 Wakati huo, Mufilisti huyo alikuwa anakuja mbele na kusimama mahali pake kila asubui na kila mangaribi kwa siku makumi ine (40).
17 Kisha Yese akamuambia Daudi mwana wake: “Tafazali, kamata efa* hii ya nafaka yenye kukaangwa na mikate hii kumi (10), na uvipelekee haraka ndugu zako katika kambi. 18 Na umupelekee mukubwa wa elfu mafungu haya kumi (10) ya jibini;* pia, utaangalia hali ya ndugu zako na uniletee alama fulani kutoka kwao.” 19 Walikuwa pamoja na Sauli na wanaume wengine wote wa Israeli katika Bonde* la Ela,+ wakipigana na Wafilisti.+
20 Kwa hiyo Daudi akaamuka asubui sana na kuacha kondoo katika mikono ya mutu fulani; kisha akapakiza vitu hivyo na kuenda kama vile Yese alikuwa amemuamuru. Wakati alifika katika kiwanja cha kambi, jeshi lilikuwa likienda kwenye kiwanja cha mapigano, likifanya makelele ya vita. 21 Israeli na Wafilisti wakajipanga kwa ajili ya vita ili kikundi kimoja cha wapiganaji kielekee kikundi kingine cha wapiganaji. 22 Mara moja Daudi akaacha mizigo yake katika mikono ya muchunga-mizigo na akakimbia kuenda kwenye kiwanja cha mapigano. Wakati alifika, akaanza kuuliza hali ya ndugu zake.+
23 Wakati alikuwa anazungumuza nao, kukatokea ule Mufilisti shujaa mwenye aliitwa Goliati,+ wa Gati. Alitoka katika kikundi cha wapiganaji Wafilisti, na akasema maneno yaleyale yenye alisema mbele,+ na Daudi akamusikia. 24 Wakati wanaume wote wa Israeli walimuona mwanaume huyo, wakaogopa sana na kumukimbia.+ 25 Wanaume wa Israeli walikuwa wanasema: “Je, munamuona ule mwanaume mwenye iko* anakuja? Anakuja kuchokoza* Israeli.+ Mufalme atamupatia utajiri mwingi mutu mwenye atamuua mwanaume huyo, atamupatia pia binti yake mwenyewe,+ na ataondoa masharti juu ya nyumba ya baba yake katika Israeli.”
26 Daudi akaanza kuambia wanaume wenye walikuwa wamesimama karibu naye: “Mutu mwenye ataua ule Mufilisti na kuondoa haya juu ya Israeli atafanyiwa nini? Kwa kweli huyu Mufilisti mwenye hatahiriwe ni nani ili achokoze* kikundi cha wapiganaji cha Mungu mwenye kuishi?”+ 27 Basi watu hao wakamuambia jambo lilelile lenye lilisemwa mbele: “Ni hivi atafanyiwa mwanaume mwenye atamuua.” 28 Wakati Eliabu ndugu yake mukubwa zaidi+ alimusikia Daudi akizungumuza na wanaume hao, akamukasirikia Daudi na kusema: “Sababu gani umeshuka? Na wale kondoo kidogo katika jangwa uliwaachia nani?+ Ninajua muzuri kimbelembele chako na nia mubaya ya moyo wako; umeshuka tu ili kuangalia mapigano.” 29 Basi Daudi akamuambia: “Sasa nimefanya nini? Nilikuwa tu ninauliza ulizo!” 30 Kwa hiyo Daudi akamuacha na kugeuka kuelekea mutu mwingine na akamuuliza jambo lilelile lenye aliuliza mbele,+ na watu wakamupatia jibu lilelile lenye alipewa mbele.+
31 Maneno yenye Daudi alikuwa amesema yalisikiwa na yaliripotiwa kwa Sauli. Kwa hiyo Sauli akamuitisha. 32 Daudi akamuambia Sauli: “Mutu yeyote asivunjike moyo* kwa sababu yake. Mutumishi wako ataenda kupigana na Mufilisti huyo.”+ 33 Lakini Sauli akamuambia Daudi: “Hauwezi kuenda kupigana na Mufilisti huyo, kwa sababu wewe ni kijana tu,+ naye amekuwa askari* tangu ujana wake.” 34 Kisha Daudi akamuambia Sauli: “Mutumishi wako amekuwa muchungaji wa kundi la baba yake, na simba+ akakuja, na pia dubu, na kila mumoja wao akabeba kondoo katika kundi. 35 Nilimufuata na nikamupiga na kumuua na kumuokoa kondoo katika kinywa chake. Wakati aliruka ili kunishambulia, nilimukamata kwa manyoya yake,* na kumupiga na kumuua. 36 Mutumishi wako alipiga na kuua simba na dubu pia, na huyu Mufilisti mwenye hatahiriwe atakuwa kama mumoja wao, kwa sababu amechokoza* vikundi vya wapiganaji vya Mungu mwenye kuishi.”+ 37 Kisha Daudi akaongeza: “Yehova, mwenye aliniokoa kutoka katika makucha ya simba na ya dubu, ndiye ataniokoa kutoka katika mukono wa Mufilisti huyu.”+ Basi Sauli akamuambia Daudi: “Uende, na Yehova akuwe pamoja na wewe.”
38 Basi Sauli akamuvalisha Daudi nguo zake. Akatia kofia ya shaba juu ya kichwa chake, kisha akamuvalisha koti ya chuma. 39 Kisha Daudi akafunga upanga wake juu ya nguo zake na akajaribu kutembea lakini hakuweza kwa sababu hakukuwa amevizoea. Daudi akamuambia Sauli: “Siwezi kuenda nikiwa nimevaa vitu hivi, kwa maana sivizoee.” Kwa hiyo Daudi akavitosha. 40 Kisha akakamata fimbo yake katika mukono wake na akajichagulia majiwe laini tano (5) katika sehemu ya chini ya muto mudogo* na kuyatia katika kifuko cha mufuko wake wa muchungaji, na kombeo lake+ lilikuwa katika mukono wake. Na akaanza kumukaribia Mufilisti huyo.
41 Mufilisti huyo akaanza kumukaribia Daudi zaidi na zaidi, na mubeba-ngao wake alikuwa mbele yake. 42 Wakati Mufilisti huyo aliangalia na kumuona Daudi, akamuchekelea kwa zarau kwa sababu alikuwa tu kijana mwekundu na mwenye sura ya muzuri.+ 43 Kwa hiyo Mufilisti huyo akamuambia Daudi: “Je, mimi niko imbwa,+ ndiyo maana unakuja na fimbo ili kupigana na mimi?” Basi Mufilisti huyo akamulaani Daudi kwa jina la miungu yake. 44 Mufilisti huyo akamuambia Daudi: “Nikaribie tu, na nyama yako nitaipatia ndege wa mbinguni na wanyama wa pori.”
45 Daudi akamujibu Mufilisti huyo: “Unakuja kupigana na mimi ukiwa na upanga na mukuki mukubwa na mukuki mudogo,+ lakini mimi nakuja kupigana na wewe katika jina la Yehova wa majeshi,+ Mungu wa kikundi cha wapiganaji cha Israeli, mwenye umechokoza.*+ 46 Leo hii Yehova atakutia wewe katika mukono wangu,+ na nitakupiga na kukuua na kukata kichwa chako; na siku ya leo nitapatia ndege wa mbinguni na wanyama wa pori wa dunia maiti za kambi ya Wafilisti; na watu wa dunia yote watajua kwamba kuko Mungu katika Israeli.+ 47 Na watu wote wenye kukusanyika hapa* watajua kwamba Yehova haokoe kwa upanga wala kwa mukuki,+ kwa sababu vita ni ya Yehova,+ na atawatia ninyi wote katika mukono wetu.”+
48 Kisha Mufilisti huyo akasimama na akaendelea kukaribia ili akutane na Daudi, lakini Daudi akakimbia haraka kuelekea kwenye kiwanja cha mapigano ili kukutana na Mufilisti huyo. 49 Daudi akaingiza mukono wake ndani ya mufuko wake na kukamata ndani jiwe na kulitupa kwa kombeo. Akamupiga Mufilisti huyo katika paji la uso, na jiwe hilo likaingia katika paji la uso wake na akaanguka uso chini kwenye udongo.+ 50 Kwa hiyo Daudi akamushinda Mufilisti huyo kwa kutumia kombeo na jiwe; alimupiga Mufilisti huyo na kumuua, hata kama upanga wowote haukukuwa katika mukono wa Daudi.+ 51 Daudi akaendelea kukimbia na akasimama juu yake. Kisha akashika upanga wa Mufilisti huyo+ na kuutosha katika mufuko wake wa upanga na akahakikisha kwamba amekufa kwa kumukata kichwa na upanga huo. Wakati Wafilisti waliona kwamba mupiganaji wao mwenye nguvu amekufa, wakakimbia.+
52 Basi wanaume wa Israeli na Yuda wakasimama na kuanza kufanya makelele na kufuatilia Wafilisti katika njia yote kuanzia bonde+ mupaka kwenye milango mikubwa ya Ekroni,+ na maiti za Wafilisti wenye waliuawa zilikuwa zimeanguka kwenye barabara kuanzia Shaaraimu,+ mupaka Gati na Ekroni. 53 Wakati Waisraeli walikuwa wamerudia kisha kufuatilia kwa ukali Wafilisti, walinyanganya vitu katika kambi zao.
54 Kisha Daudi akakamata kichwa cha Mufilisti huyo na kukileta Yerusalemu, lakini akaweka silaha za Mufilisti huyo ndani ya hema yake mwenyewe.+
55 Wakati Sauli alimuona Daudi akienda kupigana na Mufilisti huyo, alimuambia Abneri,+ mukubwa wa jeshi: “Abneri, kijana huyu ni mwana wa nani?”+ Abneri akajibu: “Kama vile hakika unaishi,* Ee mufalme, mimi sijue!” 56 Mufalme akasema: “Tafuta kujua kama kijana huyu mwanaume ni mwana wa nani.” 57 Kwa hiyo wakati tu Daudi alirudia kisha kumupiga na kumuua Mufilisti huyo, Abneri alimuchukua na kumupeleka mbele ya Sauli akiwa na kichwa cha Mufilisti huyo+ katika mukono wake. 58 Basi Sauli akamuambia: “Wewe kijana, uko mwana wa nani?” Daudi akasema: “Mwana wa mutumishi wako Yese+ Mubetlehemu.”+