Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 24
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 1 Samweli

      • Daudi hamuue Sauli (1-22)

        • Daudi anamuheshimia mutiwa-mafuta wa Yehova (6)

1 Samweli 24:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “eko.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 23:28, 29

1 Samweli 24:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.

  • *

    Tnn., “afunike miguu yake.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 57:utangulizi; 142:utangulizi

1 Samweli 24:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 26:8, 23

1 Samweli 24:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “zamiri ya Daudi ikaendelea.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 24:10

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    15/10/2007, uku. 22

1 Samweli 24:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 22:28; 1 Sa. 26:11; 2 Sa. 1:14; 1Nya 16:22

1 Samweli 24:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao pengine, “akasambaza.”

1 Samweli 24:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 26:17

1 Samweli 24:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 26:19

1 Samweli 24:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 24:4
  • +1 Sa. 9:16; 10:1; 26:9; Zab 105:15

1 Samweli 24:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “nafsi yangu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 26:18; Zab 35:7
  • +1 Sa. 23:14

1 Samweli 24:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 26:23
  • +Kum 32:35
  • +1 Sa. 26:11

1 Samweli 24:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Kiroboto ni kidudu kidogo chenye kuruka ambacho kinaishi katika mavumbi na kwenye wanyama.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 26:20

1 Samweli 24:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 25:39; Zab 35:1

1 Samweli 24:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 26:17

1 Samweli 24:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 26:21

1 Samweli 24:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 24:4, 10

1 Samweli 24:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 26:25; Zab 18:20

1 Samweli 24:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 13:14; 15:28; 18:8; 20:31; 23:17

1 Samweli 24:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mbegu yangu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 19:12; Kum 6:13
  • +2 Sa. 9:1; 21:7

1 Samweli 24:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 15:34
  • +1 Sa. 23:29

Maandiko ingine

1 Sam. 24:11 Sa. 23:28, 29
1 Sam. 24:3Zab 57:utangulizi; 142:utangulizi
1 Sam. 24:41 Sa. 26:8, 23
1 Sam. 24:52 Sa. 24:10
1 Sam. 24:6Kut 22:28; 1 Sa. 26:11; 2 Sa. 1:14; 1Nya 16:22
1 Sam. 24:81 Sa. 26:17
1 Sam. 24:91 Sa. 26:19
1 Sam. 24:101 Sa. 24:4
1 Sam. 24:101 Sa. 9:16; 10:1; 26:9; Zab 105:15
1 Sam. 24:111 Sa. 26:18; Zab 35:7
1 Sam. 24:111 Sa. 23:14
1 Sam. 24:121 Sa. 26:23
1 Sam. 24:12Kum 32:35
1 Sam. 24:121 Sa. 26:11
1 Sam. 24:141 Sa. 26:20
1 Sam. 24:151 Sa. 25:39; Zab 35:1
1 Sam. 24:161 Sa. 26:17
1 Sam. 24:171 Sa. 26:21
1 Sam. 24:181 Sa. 24:4, 10
1 Sam. 24:191 Sa. 26:25; Zab 18:20
1 Sam. 24:201 Sa. 13:14; 15:28; 18:8; 20:31; 23:17
1 Sam. 24:21Law. 19:12; Kum 6:13
1 Sam. 24:212 Sa. 9:1; 21:7
1 Sam. 24:221 Sa. 15:34
1 Sam. 24:221 Sa. 23:29
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
1 Samweli 24:1-22

Cha Kwanza cha Samweli

24 Wakati tu Sauli alirudia kisha kufuatilia Wafilisti, walimuambia: “Angalia! Daudi iko* katika jangwa la En-gedi.”+

2 Kwa hiyo Sauli akachukua wanaume elfu tatu (3 000) wenye walichaguliwa katika Israeli yote na akaenda kumutafuta Daudi na watu wake kwenye miteremuko mikali yenye miamba ya mbuzi wa milima. 3 Sauli akafika kwenye mazizi* ya majiwe ya kondoo pembeni ya barabara, mahali kwenye kulikuwa pango, na akaingia ndani ili ajisaidie,* wakati huo Daudi na watu wake walikuwa wamekaa katika sehemu za ndani kabisa nyuma ya pango hilo.+ 4 Watu wa Daudi wakamuambia: “Hii ndiyo siku yenye Yehova anakuambia, ‘Angalia! Ninamutia adui yako katika mukono wako,+ na unaweza kumutendea jambo lolote lenye linaonekana kuwa la muzuri kwako.’” Kwa hiyo Daudi akasimama na kukata kimya-kimya upindo wa koti ya Sauli yenye haina mikono. 5 Lakini kisha wakati fulani, moyo wa Daudi ukaendelea* kumulaumu+ kwa sababu alikuwa amekata upindo wa koti ya Sauli yenye haina mikono. 6 Akaambia watu wake: “Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwa maoni ya Yehova kwamba nimutendee jambo kama hilo bwana wangu, mutiwa-mafuta wa Yehova, kwa kuinua mukono wangu juu yake, kwa kuwa yeye ni mutiwa-mafuta wa Yehova.”+ 7 Kwa hiyo Daudi akazuia* watu wake kwa maneno hayo, na hakuwaruhusu wamushambulie Sauli. Kuhusu Sauli, alisimama kutoka katika pango na kuenda zake.

8 Kisha Daudi akasimama na kutoka katika pango na kumuita Sauli: “Bwana wangu mufalme!”+ Wakati Sauli aliangalia nyuma, Daudi aliinamisha uso wake mupaka chini na kuinama uso chini. 9 Daudi akamuuliza Sauli: “Sababu gani unasikiliza maneno ya watu wenye wanasema, ‘Angalia! Daudi anataka kukufanya mubaya’?+ 10 Siku hii ya leo macho yako mwenyewe yameona namna Yehova alikutia katika mukono wangu ndani ya pango. Lakini wakati mutu fulani alisema nikuue,+ nilikusikilia huruma na kusema, ‘Sitainua mukono wangu juu ya bwana wangu, kwa maana yeye ni mutiwa-mafuta wa Yehova.’+ 11 Na angalia, baba yangu, ndiyo, ona upindo wa koti yako yenye haina mikono katika mukono wangu; kwa sababu wakati nilikata upindo wa koti lako lenye halina mikono, sikukuua. Sasa unaweza kuona na kuelewa kwamba sikusudie kukufanya mubaya wala kukuasi, na sijakutendea zambi,+ lakini wewe unaniwinda ili uondoe uzima wangu.*+ 12 Yehova ahukumu katikati yangu na wewe,+ na Yehova akulipize kisasi kwa ajili yangu,+ lakini mukono wangu hautakuja juu yako.+ 13 Kama vile mezali ya zamani inasema, ‘Uovu unatoka kwa waovu,’ lakini mukono wangu hautakuja juu yako. 14 Mufalme wa Israeli ametoka ili kumutafuta nani? Unamufuatilia nani? Imbwa mwenye kufa? Kiroboto* mumoja?+ 15 Yehova akuwe muamuzi, na atahukumu katikati yangu na wewe, na ataona na kutetea kesi yangu ya hukumu+ na kunihukumu na kuniokoa katika mukono wako.”

16 Wakati Daudi alimaliza kumuambia maneno hayo, Sauli akasema: “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwana wangu?”+ Na Sauli akaanza kulia kwa sauti kubwa. 17 Akamuambia Daudi: “Wewe ni mwenye haki kuliko mimi, kwa maana umenitendea muzuri na mimi nimekulipa uovu.+ 18 Ndiyo, leo umeniambia kuhusu mema yenye ulitenda kwa kukosa kuniua wakati Yehova alinitia katika mukono wako.+ 19 Kwa maana ni mutu gani anamupata adui yake na kumuacha aende zake bila kumufanya mubaya? Yehova atakupatia zawabu ya mema+ kwa sababu ya mambo yenye umenifanyia leo. 20 Na sasa angalia! Ninajua hakika kwamba utatawala ukiwa mufalme+ na kwamba ufalme wa Israeli utadumu katika mukono wako. 21 Sasa uniapie katika jina la Yehova+ kwamba hautafuta wazao wangu* kisha mimi na kwamba hautaharibu jina langu kutoka katika nyumba ya baba yangu.”+ 22 Kwa hiyo Daudi akamuapia Sauli, kisha Sauli akaenda kwenye nyumba yake.+ Lakini Daudi na watu wake wakapanda kuenda kwenye ngome.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine